UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI WA MWAKA 2016/17 KUFANYIKA DAR ES SALAAM MWISHONI MWA MWEZI MEI, 2017
Mkurugenzi Msahauri, Dkt. Cecilia Makafu kutoka Shirika la ICAP Tanzania akiwasilisha mada kuhusu Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI wa mwaka 2016/17 kwa wadau wa Utafiti huo wa Mkoa wa Dar es Salaam.
HomeJamii

UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI WA MWAKA 2016/17 KUFANYIKA DAR ES SALAAM MWISHONI MWA MWEZI MEI, 2017

Na Veronica Kazimoto Wito umetolewa kwa Wananchi wote wa mkoa wa Dar es Salaam ambao kaya zao zimechaguliwa kitaalam kwa ajili ya  Utafiti...

CRDB YATOA MSAADA KATIKA HOSPITALI YA SARATANI YA OCEAN ROAD
BAM INTERNATIONAL-AFRICA SUPPORTS INTERNATIONAL WOMEN'S DAY 2017, WHILE GRACED BY MINISTER KAIRUKI
NIMR NA CHUO CHA SAYANSI CHA NELSON MANDELA WATOA UTAFITI WA UGONJWA MARALE

Na Veronica Kazimoto
Wito umetolewa kwa Wananchi wote wa mkoa wa Dar es Salaam ambao kaya zao zimechaguliwa kitaalam kwa ajili ya  Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI wa mwaka 2016/17 kutoa ushirikiano kwa wadadisi wataokusanya taarifa za utafiti huo utakaofanyika mwishoni mwa mwezi Mei, mwaka huu.
Akizungumza hivi karibuni katika  Mkutano wa Wadau wa Utafiti huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi. Sophia Mjema amesema Utafiti huu ni muhimu sana kwani husaidia kujua hali halisi ya ugonjwa wa UKIMWI na hivyo kuongeza nguvu zaidi ya kuondokana na ugonjwa huo.
"Mimi niwaeleze tu kwamba, utafiti huu ni muhimu sana katika mkoa wetu wa Dar es Salaam kwa kuwa utatusaidia kujua hali halisi ya maambukizi ya VVU na hatimaye kupata nguvu zaidi za kuondokana na ugonjwa huu, hivyo nawaagiza kusimamia zoezi hili na kuwahimiza Wananchi wote ambao kaya zao zimechaguliwa kutoa ushirikiano kwa wadadisi watakaofanya taarifa za utafiti huu", amesema Mjema.
Mjema amefafanua kuwa, utafiti huu ni wa kwanza kukusanya taarifa zinazohusiana na maambukizi mapya ya VVU, kiwango cha VVU mwilini kwa watu wanaoishi na VVU na wastani wa maambukizi ya VVU kwa watu wa rika zote pamoja na wingi wa chembechembe za kinga mwilini (CD4 T-cell count).
Aidha,  utafiti huu utapima uwepo wa viashiria vya usugu wa dawa, kiwango cha maambukizi ya kaswende pamoja na homa ya ini (Hepatitis B).
Akizungumzia kiwango cha maambukizi ya VVU katika tafiti zilizopita, Mkuu wa Wilaya huyo ameeleza kuwa, maambukizi yamepungua kutoka asilimia 7 mwaka 2003 mpaka asilimia 5.1 mwaka 2011 na kuifanya Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi zenye kiwango cha chini cha maambukizi ya nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo nchi nyingi za ukanda huo zina kiwango cha zaidi ya aslimia 10.



Nae Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Grace Magembe amesema kuwa, kwa mkoa wa Dar es Salaam, utafiti huu utahusisha kaya zisizozidi 1,000  na Wananchi watakuwa na hiari ya kukubali kupima ambapo kwa wale watakaogundulika kuwa na maambukizi, watapata rufaa ya kwenda kupatiwa matibabu bure katika vituo vya kutolea huduma za afya.

"Utafiti huu wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI hauhusishi watu wote bali ni kaya chache tu ambazo zimechaguliwa kitaalam ili ziweze kuwakilisha kaya nyingine na kwa hapa Dar es Salaam kaya zilizochaguliwa hazizidi 1000", amesema Dkt. Magembe.

Utafiti wa aina hii ni wa mara ya nne (4) kufanyika nchini Tanzania ambapo wa kwanza ulifanyika mwaka 2003, wa pili mwaka 2007 na wa tatu mwaka 2011.

Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016 /17 unafanyika nchini, chini ya usimamizi wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya kwa Tanzania Bara, Wizara ya Afya Tanzania Zanzibar, Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS)  na Tume ya UKIMWI Zanzibar (ZAC). 



Baadhi ya Washiriki waliohudhuria Mkutano wa Wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/17 uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akizungumza hivi karibuni na  Wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/17. Kwa Dar es Salaam, utafiti huu  unatarajia kuanza mwishoni mwa mwezi Mei, 2017.







Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI WA MWAKA 2016/17 KUFANYIKA DAR ES SALAAM MWISHONI MWA MWEZI MEI, 2017
UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI WA MWAKA 2016/17 KUFANYIKA DAR ES SALAAM MWISHONI MWA MWEZI MEI, 2017
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhp3ClcbibrEmbNd8SppoGhJKL0zUNbUTN60BkmZIH8iCbYh1Kv6EqXp-lusUlI9Qpuf9qNsCUqJBi8ca7ztHzUyHLqtPFDEV3ciDNJQ4fuapggSS9EfMRARh2K80p0Qa6TEghvlvfp05w/s640/PICHA+N0.+2.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhp3ClcbibrEmbNd8SppoGhJKL0zUNbUTN60BkmZIH8iCbYh1Kv6EqXp-lusUlI9Qpuf9qNsCUqJBi8ca7ztHzUyHLqtPFDEV3ciDNJQ4fuapggSS9EfMRARh2K80p0Qa6TEghvlvfp05w/s72-c/PICHA+N0.+2.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/05/utafiti-wa-viashiria-na-matokeo-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/utafiti-wa-viashiria-na-matokeo-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy