JENGO LA HOSTELI CHUO CHA MADINI DODOMA LAKAMILIKA

Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Wizara ya Nishati na Madini, Caroline Musika akikabidhiwa funguo za jengo la hosteli la...















Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Wizara ya Nishati na Madini, Caroline Musika akikabidhiwa funguo za jengo la hosteli la Chuo cha MRI na Mkandarasi  aliyejenga jengo hilo kutoka kampuni ya Chichi Engineering Construction Ltd, Shaibu Katindi. Wanaoshuhudia ni Msanifu Majengo wa SMMRP, Arch. Joseph Ringo (kulia), Mkuu wa Chuo cha MRI, Mhandisi Oforo Ngowi (wa pili kushoto), Maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini na washauri waliosimamia ujenzi wa jengo hilo.

Mkuu wa Chuo cha Madini cha Dodoma, Mhandisi Oforo Ngowi (wa pili kulia) akifafanua jambo wakati wa ukaguzi wa bwalo la wanafunzi. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Wizara ya Nishati na Madini, Caroline Musika akifuatiwa na Mkuu wa Kitengo cha Tehama, Wizara ya Nishati na Madini, Francis Fungameza. Kulia ni Mshauri Mwelekezi na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya PSM Architects Ltd, Peter Matinde.



Msanifu Majengo wa SMMRP, Arch. Joseph Ringo akitia saini Hati ya Makabidhiano mara baada ya kufanya ukaguzi na kujiridhisha. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Wizara ya Nishati na Madini, Caroline Musika.





Msanifu Majengo wa SMMRP, Joseph Ringo (mwenye shati jeupe) akifafanua jambo katika kikao na Mkuu wa Chuo cha Madini cha Dodoma, Mhandisi Oforo Ngowi (mbele katikati) mara baada ya kuwasili chuoni hapo. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo chaTehama, Wizara ya Nishati na Madini, Francis Fungameza na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala Nishati na Madini, Caroline Musika (wa pili kushoto).

Jengo jipya la hosteli ya wasichana la Chuo cha Madini Dodoma (MRI) ambalo ujenzi wake umemalizika hivi karibuni.

Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Wizara ya Nishati na Madini, Caroline Musika (kulia) akiwa sambamba na Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mkandarasi pamoja na baadhi ya washauri waliosimamia ujenzi wakimsikiliza Mshauri Mwelekezi na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya PSM Architects Ltd, Peter Matinde (hayupo pichani) wakati wa ukaguzi wa jengo la hosteli.

Jengo jipya la hosteli ya wasichana la Chuo cha Madini Dodoma (MRI) ambalo ujenzi wake umekamilika hivi karibuni.

Mshauri Mwelekezi na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya PSM Architects Ltd, Peter Matinde (kulia) akielezea jambo mara baada ya kufanyika kwa ukaguzi wa jengo la hosteli la MRI. Pamoja naye ni nae ni Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini na  Mkandarasi.

Moja ya chumba katika jengo lililokabidhiwa la hosteli ya wasichana ya Chuo cha Madini (MRI) Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Wizara ya Nishati na Madini, Caroline Musika (kushoto) akiendelea na ukaguzi katika moja ya chumba katika jengo la hosteli. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Tehama, Wizara ya Nishati na Madini, Francis Fungameza.

Bwalo la wanafunzi wa chuo cha Madini Dodoma baada ya kukarabatiwa na kupanuliwa.




Wizara ya Nishati na Madini imepokea jengo la hosteli ya wasichana ya Chuo, cha Madini cha Dodoma (MRI) kutoka kwa Mkandarasi wa Kampuni ya Chichi Engineering Construction Limited katika makabidhiano yaliyofanywa hivi karibuni, mkoani Dodoma mara baada ya ujenzi kukamilika.
Akizungumza kwa niaba ya Meneja Mradi wa  Usimamizi  Endelevu wa  Rasilimali Madini (SMMRP), Mhandisi Idrisa Yahya, wakati wa makabidhiano hayo Msanifu Majengo (Architect) wa SMMRP, Joseph Ringo alisema kuwa kukamilika kwa ujenzi huo kutapunguza uhaba wa nafasi za malazi kwa wanafunzi hususan wa kike katika chuo hicho

Mkandarasi kutoka kampuni ya Chichi Engineering Construction Ltd, Shaibu Katindi akielezea jambo kabla ya kuanza kwa ukaguzi wa jengo la hosteli. Wengine katika picha ni wakaguzi pamoja na washauri waliosimamia ujenzi wa jengo hilo.

Aidha alisema kulingana na takwimu za MRI inaonyesha kila mwaka usaili wa wanafunzi unaongezeka na kwakua chuo hicho hakina hosteli za kutosha inawalazimu wanafunzi wengi kupangisha vyumba nje ya chuo jambo ambalo alisema si jema kwa wanafunzi hao.
"Kila mwaka wanafunzi wanaongezeka, kwahiyo kupitia jengo hili jipya la hosteli ya wasichana nina imani changamoto ya malazi kwao itakua imetatuliwa," alisema.
Katika makabidhiano hayo, ilielezwa kuwa jengo hilo la hosteli linao uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 88.
Aidha, mbali na jengo hilo la hosteli, makabidhiano hayo pia yalihusu ukarabati na upanuzi wa bwalo la wanafunzi pamoja na ukarabati wa ofisi ya Mkuu wa Chuo.
Arch. Ringo alieleza kuwa makabidhiano hayo yanakamilisha Awamu ya kwanza ya Mradi wa SMMRP kwa chuo hicho na alisema matarajio ya baadaye ni kujenga miundombinu zaidi ili kukidhi mahitaji ya chuo hicho.
"Mahitaji ya chuo kuhusiana na majengo ni makubwa kuliko haya yaliyojengwa," alisema.
Akizungumzia mikakati ya utekelezaji wa Awamu ya Pili ya mradi wa SMMRP (Additional Financing), Arch.Ringo alisema hatua zote za kuanza utekelezaji zimeanza.
"Matarajio yetu ni kuwa malengo yaliyopangwa yatafikiwa kwa muda uliopangwa. Mradi huu umebeba dhima kubwa ya kuhakikisha Watanzania wananufaika zaidi na sekta  ya Madini," alisema.
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo hicho cha Madini, Mhandisi Oforo Ngowi, alisema  mradi huo wa ukarabati na ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Chuo, bwalo la wanafunzi na hosteli unao umuhimu wa kipekee katika kuboresha miundombinu pamoja na kuleta maendeleo endelevu ya chuo hicho.
"Huu ni ukombozi mkubwa sana kwa wanafunzi waliokuwa wanahangaika kutafuta malazi nje ya chuo. Kilichobaki ni hapa kusoma tu," alisema.
Mradi huo wa Chuo cha Madini uliokabidhiwa umefadhiliwa na Benki ya Dunia chini ya usimamizi wa SMMRP na ulianza Julai, 2014 na kukamilika mwaka huu 2016 na  ilielezwa kwamba umegharimu takriban milioni 997.
Aidha jengo hilo la hosteli limebuniwa na kampuni ya ubunifu Majengo ya PSM Architects Ltd kwa kushirikiana na Howard Humphreys (T) Ltd na Mas-Q Associates Ltd.
Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazotekeleza miradi mbalimbali ya sekta ya madini chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia.









COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: JENGO LA HOSTELI CHUO CHA MADINI DODOMA LAKAMILIKA
JENGO LA HOSTELI CHUO CHA MADINI DODOMA LAKAMILIKA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhILO6jMqL6cPCSm_7z2IXMvHtpTqIKCv7srUyc7QOT9ofQmD3OhLoPRerJRE5zzRVhGs_-DShVHtmO9cUFOqTGtGSgVW2cVaF_R64uf1ANw0FSkUHdEjXH2fR4l9PnjEXgFQ0GAoMJkDPi/s640/KUMI+NA+MBILI+.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhILO6jMqL6cPCSm_7z2IXMvHtpTqIKCv7srUyc7QOT9ofQmD3OhLoPRerJRE5zzRVhGs_-DShVHtmO9cUFOqTGtGSgVW2cVaF_R64uf1ANw0FSkUHdEjXH2fR4l9PnjEXgFQ0GAoMJkDPi/s72-c/KUMI+NA+MBILI+.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/02/jengo-la-hosteli-chuo-cha-madini-dodoma.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/02/jengo-la-hosteli-chuo-cha-madini-dodoma.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy