TAA YAMLILIA MWANASHERIA DELFINE
Paroko wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Augustine, Padri Fidelis Mfaranyembo lililopo Mbezi Temboni jijini Dar es Salaam, jana akinyunyizia maji ya baraka kwenye mwili wa aliyekuwa Mwanasheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Kituo cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), marehemu Delfine Mulogo kabla ya kusafirishwa kwenda Kijiji cha Uru Kishumundu Mkoani Kilimanjaro kwa maziko
HomeJamii

TAA YAMLILIA MWANASHERIA DELFINE

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), inamlilia kwa masikitiko makubwa Mwanasheria wake marehemu Bi. Delfine Mu...

MAELEZO TV :SERIKALI KUANZA KUTOA ELIMU YA MLIPA KODI MASHULENI
WAZIRI MKUCHIKA ATETA NA BALOZI WA USWISS
SPIKA WA BUNGE, MHE. JOB NDUGAI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI KILICHOFANYIKA LEO MJINI DODOMA.

Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), inamlilia kwa masikitiko makubwa Mwanasheria wake marehemu Bi. Delfine Mulogo (32) aliyekuwa Kituo cha kazi cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) aliyefariki tarehe Desemba 25.
Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi na Ugavi, Bw. Mtengela Hanga akisoma wasifu wa marehemu katika kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Augustine Mbezi Temboni, alisema atakumbukwa kwa uchapakazi, uhodari na uadilifu wake kazini.
“Tunasikitika kumpoteza mwanasheria huyu kijana, kwa niaba ya Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, tunatoa pole kwa wafiwa kwa kuondokewa na mpendwa wao, lakini sisi kama mamlaka na taifa kwa ujumla tumempoteza mtu muhimu sana aliyekuwa mchapakazi, tutamkumbuka sana marehemu,” alisema Bw. Hanga.
Marehemu ambaye ameacha mume Bw. Alex Temba na watoto wawili Faith Temba (9) na Harieth Temba (4) alihamishiwa TAA tarehe 01/04/2016 akitokea Halmashauri ya Manispaa ya mji wa Songea alipokuwa akifanya kazi kama mwanasheria kuanzia mwaka 2012.
Naye Mwakilishi wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS), Bw. Stephen Msechu alisema marehemu alikuwa mwanachama tangu alipoapishwa kuwa Wakili mwaka 2012 na kupewa namba ya uanachama 3361 na amekuwa akishirikiana nao katika shughuli mbalimbali kwa uadilifu mkubwa.
Hata hivyo, Paroko wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Augustine lililopo Mbezi Temboni, Padri Fidelis Mfaranyembo aliwataka waombolezaji waliofika kuuaga mwili wa marehemu  Delfine kujiandaa wakati wote kwa kuwa hatujui saa wala siku watakayotwaliwa.
Padri Mfaranyembo alisema pia waombolezaji wahakikishe wanakuwa watu wa sala wakati wote ili kumuombea marehemu aweze kupokelewa na aingie katika ufalme wa mbinguni, kwani ufalme huo upo kwa kuwa kunamaisha baada ya kifo.
“Kuna mwanafalsafa mmoja wa zamani, Plato alitafakari  sana kuwa mwanadamu akifa anakwenda wapi? na akaona kila mwanadamu anabeba roho ya muumbaji  na hivyo unapokufa roho inarudi kwa yule aliyeiumba, Plato anatufundisha ya kwamba mwisho wa maisha yake hapa duniani Mwanadamu anarudi kwa Mungu wake kulingana na namna alivyokuwa akiishi na wengine hapa duniani,” alisema Padri Mfaranyembo.
Pia amemtaka mume wa marehemu Bw. Temba asifadhaike kwa kuondokewa na mkewe, bali ajikabidhi kwa Mungu kwa kumuomba hakika atamsaidia kwa kumtia nguvu na kumpa uwezo wa kuendelea kuwahudumia watoto wake kwa kadri ya uweza wake Mungu.
Marehemu alipata elimu ya msingi katika shule ya Oysterbay (1991), baadaye sekondari ya St. Mathew (1998), na baadaye elimu ya Kidato cha Tano na Sita katika shule ya Wasichana ya Kibosho (2004), na mwaka 2008 alihitimu Shahada ya Kwanza ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Tumaini.  


Alex Temba (wa pili kushoto) ambaye ni mume wa marehemu aliyekuwa Mwanasheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kituo cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bi. Delfine Mulogo akiwa na binti yake Faith Temba (mwenye gauni jeupe) wakitoa heshima za mwisho katika kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Augustine lililopo Mbezi Temboni kabla ya kusafirishwa kwa mazishi katika Kijiji cha Uru Kishumundu mkoani Kilimanjaro.

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Lawrence Thobias akitoa heshima zake kwa mwili wa aliyekuwa Mwanasheria Kituo cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bi. Delfine Mulogo aliyefariki Desemba 25. Marehemu atazikwa Kijiji cha Uru Kishumundu mkoani Kilimanjaro.

  1. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Bi. Agnes Kijazi akimpa pole Bw. Alex Temba kufuatia kifo cha Mkewe Bi. Delfine Mulogo aliyekuwa Mwanasheria kwenye Kituo cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) aliyefariki Desemba 25 na atazikwa Kijiji cha Uru Kishumundu mkoani Kilimanjaro.

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) wakijumuika na waombolezaji wengine katika misa ya kumwombea marehemu Bi. Delfine Mulogo aliyekuwa Mwanasheria kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA)

Mweka Hazina wa Klabu ya Uchukuzi, Bw. Benjamin Bikulamchi (kulia), akimfariji na kumkabidhi rambirambi aliyewahi kuwa Katibu wa Klabu hiyo, Bw. Alex Temba aliyefiwa na mkewe Bi. Delfine Mulogo aliyekuwa Mwanasheria Kituo cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA)

Viongozi wa Shirikisho la Michezo la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), Bi. Itika Mwankenja na Bi. Joyce Benjamin wakitoa rambirambi zao kwa Katibu Msaidizi wa shirikisho hilo Bw. Alex Temba (kushoto) aliyefiwa na Mkewe Bi. Delfine Mulogo wakati wa misa ya kumwombea marehemu iliyofanyika jana katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Augustine lililopo Mbezi Temboni

Mwanasheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Kituo cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), marehemu Delfine Mulogo enzi za uhai wake.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TAA YAMLILIA MWANASHERIA DELFINE
TAA YAMLILIA MWANASHERIA DELFINE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQdYzabNtkWHd3wsCAHPQQtm_1jfnBKiCRL2JD29L1d4JZZSDd8zgykgGH0K0aVSnxp1r7Z9tQfYPLPS3SjzjmstIwCtqj8YMDik5Tifo2d6RAqLbQgzsfMtIa53BAz_W6Jc_uKT0PbgY/s640/DEL1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQdYzabNtkWHd3wsCAHPQQtm_1jfnBKiCRL2JD29L1d4JZZSDd8zgykgGH0K0aVSnxp1r7Z9tQfYPLPS3SjzjmstIwCtqj8YMDik5Tifo2d6RAqLbQgzsfMtIa53BAz_W6Jc_uKT0PbgY/s72-c/DEL1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/12/taa-yamlilia-mwanasheria-delfine.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/12/taa-yamlilia-mwanasheria-delfine.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy