TAARIFA YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KWA UMMA-KUHUSU TUKIO LA MOTO KWENYE UKUMBI WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
HomeJamii

TAARIFA YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KWA UMMA-KUHUSU TUKIO LA MOTO KWENYE UKUMBI WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

                            JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA    WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI ...

NAIBU WAZIRI MPINA AKUTANA NA KAMATI YA ARDHI NA MAWASILIANO YA BARAZA LA WAWAKILISHI KUTOKA ZANZIBAR
SHULE YA GENIUS KINGS YAJIPANGA KUWA SHULE BORA KITAALUMA TANZANIA
WAZIRI MKUU AWATAKA WATANZANIA KUIMARISHA UZALENDO




             
             JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
   WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI


Simu ya maandishi: “ZIMAMOTO KUU”
Simu Nambari:  +255-22-2113537
Nukushi:          + 255-22-2184569
Tovuti : www.frr.go.tz


 

    TAARIFA KWA UMMA
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linapenda kutoa taarifa kwa umma kufuatia tukio la moto kwenye ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililotokea mnamo tarehe 09 Aprili, 2018 majira ya saa 1:28 usiku mkoani Dodoma.
Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa moto huo ulisababishwa na shoti iliyotokana na Power bank iliyokuwa inatumiwa kuchaji simu. Shoti hiyo ilisababisha kuungua kwa simu, Power bank, sehemu ya meza na kapeti kitendo kilicholeta moshi mkubwa na taharuki miongoni mwa Wabunge. Ukiachilia mbali taharuki kwa Waheshimiwa Wabunge hakuna madhara kwa binadamu yaliyotokana na moto huo.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji anatoa rai kwa Watanzania wote kuchukua tahadhari kubwa hasa wanapokua wanatumia vifaa vya kieletroniki ambavyo kwa sasa vipo katika matumizi hadi katika ngazi ya familia. Moto huzuka tu endapo kitapatikana chakula cha moto, joto la kutosha na hewa ya oksijeni (fuel, heat and oxygen).
Sambamba na hayo Kamishna Jenerali anahimiza uzingatiaji wa kinga na tahadhari ya moto katika maeneo yote. Wamiliki wa maeneo ya umma, binafsi na biashara wanapaswa kufunga vizimia moto kwa kuzingatia ushauri unaotolewa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lipo imara na litaendelea kuwaelimisha Watanzania kuzingatia kinga na tahadhari ya moto ili kuhakikisha maisha na mali vinakuwa salama.
Imetolewa na;


  


CGF. Thobias Andengenye
Kamishna Jenerali
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji

10 Aprili, 2018



Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TAARIFA YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KWA UMMA-KUHUSU TUKIO LA MOTO KWENYE UKUMBI WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TAARIFA YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KWA UMMA-KUHUSU TUKIO LA MOTO KWENYE UKUMBI WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
https://docs.google.com/drawings/u/0/d/sYcNSJUs_sDi7sJNTr6cIgg/image?w=263&h=88&rev=1&ac=1
https://lh6.googleusercontent.com/AMgy3p8-Z2rDOmDwtJMFu8J4drS9XtHDFMWl6CzmTXWToUoENqHd0ntM0imVEIxR4kDHDzNEK19gS7eXBb1tGflR7Yv2FOMgc4FiILjGWsBwGdNu5-SrvdnV0Mk4eZGfLN7rI3dy54maz663GQ=s72-c
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/04/taarifa-ya-jeshi-la-zimamoto-na-uokoaji.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/04/taarifa-ya-jeshi-la-zimamoto-na-uokoaji.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy