WAZIRI MKUU AWATAKA WATANZANIA KUIMARISHA UZALENDO
HomeJamii

WAZIRI MKUU AWATAKA WATANZANIA KUIMARISHA UZALENDO

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (katikati) akizungumza na wanafunzi wanaosomea fani ya Udaktari nchini Cuba, alipokutana nao katika Hotel ya Na...

ZIARA YA MAKAMU WA RAIS WILAYA YA MEATU MKOANI SIMIYU
MAKATIBU MEZANI WA BUNGE WAPEWA MAFUNZO
VIDEO: HOTUBA YA NAIBU WAZIRI DKT. FAUSTINE NDUGULILE WAKATI WA UZINDUZI WA KLABU ZA WASICHANA KATIKA SHULE YA SEKONDARI MWENDAKULIMA KAHAMA


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (katikati) akizungumza na wanafunzi wanaosomea fani ya Udaktari nchini Cuba, alipokutana nao katika Hotel ya Nacional de Cuba, Agosti 20, 2017. kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanafunzi Cuba, Goodchance Tarimo na kulia ni Ofisa wa Ubalozi wa Tanzania Nchini Canada na Cuba, Leonce Bilauri. Waziri Mkuu yupo Havana Cuba kwa Ziara ya Kikazi.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (kulia) akisalimiana na wanafunzi wa Kitanzania anaye Soma fani ya Udaktari nchini Cuba, Eshe Hemed Rashid pamoja na Nasra Sheikhan, alipokutana nao katika Hoteli ya Nacional de Cuba, Agosti 20, 2017

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi Wakitanzania wanao someafani ya Udaktari nchini Cuba.




WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania wote wahakikishe wanaboresha mshikamano wao pamoja na kuimarisha uzalendo kwa Taifa lao.


Ametoa kauli hiyo (Jumapili, Agosti 20, 2017) wakati akizungumza na wanafunzi wa Kitanzania wanaosomea udaktari nchini Cuba.


Waziri Mkuu yuko nchini Cuba kwa ajili ya ziara ya kikazi yenye lengo la kudumisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. Alisema uzalendo kwa Taifa ni jambo muhimu.


“Uzalendo ni muhimu sana kwa sababu tumekosa fursa nyingi za kimaendeleo kutokana na baadhi ya wananchi kutokuwa wazalendo kwa Taifa lao.”


Kutokana na hali hiyo Serikali inawasisitiza Wananchi kuwa wazalendo na washirikiane kuhakikisha fursa za kimaendeleo zilizoko nchini zinaendelezwa.


Alisema Serikali inatekeleza miradi mingi kwa lengo la kukuza uchumi kutoka wa chini kwenda wa kati, ni vema wananchi wakashirikiana nayo ili kufanikisha adhma hiyo.


Pia Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwasihi wanafunzi hao kuzingatia sheria za nchini waliyoko pamoja na kukumbuka kurudi nyumbani mara wamalizapo masomo yao.


Alisema Serikali inatambua uwepo wao wa kimasomo nchini Cuba na kwamba inatarajia kupata mchango mkubwa kutoka kwao punde wamalizapo masomo yao.


“Nawaomba msome kwa bidii na mfaulu mitihani yenu. Elimu yenu iwasaidie katika ajira na muweze kurejesha mikopo mliyopewa na Serikali ili iwanufaishe wengine.”


Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu aliwataka Mabalozi wote wanaoiwakilisha Tanzania katika mataifa mbalimbali kuhakikisha wanatangaza vivutio vya utalii.


Alisema Tanzania imejaaliwa kuwa na vivutio vingi vya utalii, hivyo ni vema Mabalozi wakavitangaza jambo ambalo litasaidia kuongeza idadi ya watalii wanaokuja nchini.


Miongoni mwa vivutio vya utalii vilivyoko nchini ni pamoja na mlima Kilimanjaro, visiwa vya Zanzibar, mbuga mbalimbali zenye wanyama wa aina tofauti tofauti.


Awali Mwenyekiti wa wanafunzi hao, Bw. Goodchance Tarimo alimuhakikishia Waziri Mkuu kwamba watarejea nyumbani mara baada ya kumaliza masomo yao nchini humo.


Alisema wao wanaimani kubwa na Serikali na wanaunga mkono jitihada zinazofanywa na viongozi wa Taifa kwa lengo la kuboresha maendeleo pamoja na kukuza uchumi.


“Tunapongeza jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano katika kujenga uchumi wa viwanda, mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi na ujenzi wa miundombinu ya kisasa.”


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, AGOSTI 21, 2017.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MKUU AWATAKA WATANZANIA KUIMARISHA UZALENDO
WAZIRI MKUU AWATAKA WATANZANIA KUIMARISHA UZALENDO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiW7yWSU_ROp7kUdpB5A8CdTMX14HkteRQiOm6NwiTfExA_lYhmBDkDzCZO64SuDMXokdvAPkIMfHsbgHR5FNmpV3wFnyn40z3bJIwMiMpKwp7PwkaSG8kSGgfjgTdv9ms3z1MCTgjuOxGD/s640/PMO_9463.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiW7yWSU_ROp7kUdpB5A8CdTMX14HkteRQiOm6NwiTfExA_lYhmBDkDzCZO64SuDMXokdvAPkIMfHsbgHR5FNmpV3wFnyn40z3bJIwMiMpKwp7PwkaSG8kSGgfjgTdv9ms3z1MCTgjuOxGD/s72-c/PMO_9463.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/08/waziri-mkuu-awataka-watanzania.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/08/waziri-mkuu-awataka-watanzania.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy