MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA HASSAN LEO AMEMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE MKUTANO WA SADC
HomeJamii

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA HASSAN LEO AMEMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE MKUTANO WA SADC

Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika   (SADC)  umefunguliwa rasmi leo na Mwenyekiti w...

GAZETI LA HABARILEO LAADHIMISHA MIAKA 10 TANGU KUANZISHWA KWAKE,WAZIRI NAPE ALIPONGEZA
ZIARA YA NAIBU WAZIRI MASAUNI MPAKANI TUNDUMA KUKAGUA SHUGHULI ZA UINGIAJI NA UTOKAJI WA WAGENI NA RAIA
RAIS MAGUFULI KUWA MGENI RASMI SIKU YA SHERIA NCHINI
Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umefunguliwa rasmi leo na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mfalme Mswati III wa Swaziland ukumbi wa Grand- Lozitha mjini Mbababe –Swaziland.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dakta John Pombe Magufuli anawakilishwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan katika mkutano huo.
Katika mkutano huo, Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) watajadili mambo mbalimbali yanayolenga kuimarisha utendaji kazi wa Jumuiya hiyo hasa katika sekta za viwanda, elimu, miundombinu, mtangamano wa masoko, ulinzi na usalama pamoja na kuweka mfumo wa kushirikisha sekta binafsi katika ngazi zote za utekelezaji wa mipango ya maendeleo kwenye jumuiya hiyo.
Akifungua Mkutano mkutano huo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika Mfalme Mswati III wa Swaziland amezitaka nchi wanachama wa jumuiya hiyo kuimarisha mipango na mikakati inayolenga kuhakikisha wananchi wa nchi za jumuiya hiyo wanapata huduma bora za kijamii.
Mfalme Mswati III amesema nchi wanachama wa SADC zikishirikiana kwa pamoja katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Jumuiya hiyo anaimani kuwa tatizo la uhaba wa ajira na umaskini litapungua kwa kiasi kikubwa kwenye nchi hizo.
Ameeleza kuwa ili nchi wanachama wa SADC ziweze kuimarisha shughuli za uchumi ni muhimu kwa mkakati wa kuendeleza na kujenga viwanda ukatiliwa mkazo kwa sababu nchi hizo zina rasilimali nyingi ikiwemo madini, mifugo na masuala ya utalii.
Katika mkutano huo, Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) watajadili mambo mbalimbali yanayolenga kuimarisha utendaji kazi wa Jumuiya hiyo hasa katika sekta za viwanda, elimu, miundombinu, mtangamano wa masoko, ulinzi na usalama pamoja na kuweka mfumo wa kushirikisha sekta binafsi katika ngazi zote za utekelezaji wa mipango ya maendeleo kwenye jumuiya hiyo.
Kabla ya kufanyika kwa mkutano huo ulitanguliwa na mikutano ya wataalamu, Makatibu Makuu na Mawaziri wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Ujumbe wa Tanzania katika ngazi ya Mawaziri unaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Augustine Mahiga akisaidiana na Waziri wa Viwanda na Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage pamoja na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Amina Salum Ali.
Katika ngazi ya Makatibu Wakuu ujumbe wa Tanzania unaongozwa na Balozi Aziz Mlima Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mbabane- Swaziland.




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zambia, Edgar Lungu (kushoto) na Waziri Mkuu wa Swaziland, Dkt. Barnabas Sibusiso Dlamin na Rais wa Afrika Kusini wakiwa wamesimama wakati wa kuimbwa nyimbo za mataifa wakati wa kuanza kwa mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC  ulioanzana leo mjini Mbambane Swaziland.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zambia, Edgar Lungu (kushoto) Waziri Mkuu wa Swaziland, Dkt. Barnabas Sibusiso Dlamin (wa pili kulia) na Rais wa Afrika Kusini na Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma wakiwa wamesimama wakati wa kuimbwa nyimbo za mataifa wakati wa kuanza kwa mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC  ulioanzana leo mjini Mbambane Swaziland.

Mgeni rasmi na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mfalme Mswati wa III wa Swaziland mjini Mbabane Swaziland akifungua mkutano huo ambapo amezitaka Nchi wanachama wa SADC kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya jumuiya hiyo kama hatua ya kuwakwamua  wananchi na umasikini. Kushoto ni Katibu Mkuu wa SADC, Dkt. Stagomena Taxi.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo Macih 18,2017 amehudhuria mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya kusini mwa Afrika SADC  akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli. Pamoja naye (katikati) ni Waziri Mkuu wa Swaziland, Dkt. Barnabas Sibusiso Dlamin na Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)


Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA HASSAN LEO AMEMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE MKUTANO WA SADC
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA HASSAN LEO AMEMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE MKUTANO WA SADC
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifRVvOE89Fn-EbD0l5s0866DKSKPr0MKiB4S9qssRH747ZuofMq2V9dbJhVDqWL_mEzk9BtOM1Qc1qoIKMZqLhtxnjNKfvmlXqRJa_R1wq7QRM-xNQ770Vi0__Zr6vQVBfJ88nrUtRr7k/s640/5R7A4617.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifRVvOE89Fn-EbD0l5s0866DKSKPr0MKiB4S9qssRH747ZuofMq2V9dbJhVDqWL_mEzk9BtOM1Qc1qoIKMZqLhtxnjNKfvmlXqRJa_R1wq7QRM-xNQ770Vi0__Zr6vQVBfJ88nrUtRr7k/s72-c/5R7A4617.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/makamu-wa-rais-mhe-samia-hassan-leo.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/makamu-wa-rais-mhe-samia-hassan-leo.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy