WIZARA YA AFYA YAZINDUA VIPINDI VYA RADIO KUPINGA UKEKETAJI
HomeJamii

WIZARA YA AFYA YAZINDUA VIPINDI VYA RADIO KUPINGA UKEKETAJI

Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma Serikali haina mamlaka ya kuweka ukomo wa riba au riba elekezi itakayotumiwa na mabenki katik...

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO AWASILI OFISINI KWAKE DODOMA
TAHADHARI KUTOKA TANESCO HIYOOOO!
SPORTPESA WAMPA CHETI CHA SHUKRANI MAKAMU WA RAIS


Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma
Serikali haina mamlaka ya kuweka ukomo wa riba au riba elekezi itakayotumiwa na mabenki katika kutoa mikopo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji ameeleza hayo leo Bungeni, Mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Baraza la Wawakilishi Machano Othman Said juu ya lini Serikali itaweka utaratibu wa kupunguza riba ya mikopo walau kufikia asilimia 10 – 12 badala ya sasa ambayo ni asilimia 17 – 20.
“Mabadiliko ya Sekta ya Fedha ya mwaka 1991 yalipelekea Serikali kujitoa katika uendeshaji wa moja kwa moja wa shughuli za kibenki nchini ili kuruhusu mfumo wa soko huria, hususan nguvu ya soko kuamua viwango vya riba za mikopo, riba za amana na gharama nyingine za huduma za kibenki,” alifafanua Dkt. Ashatu Kijaji.
Aliendelea kwa kusema kuwa viwango vya riba za mikopo na riba za amana pamoja na riba za mikopo kati ya benki na benki hupangwa kwa kuzingatia gharama za upatikanaji wa fedha, gharama za uendeshaji, riba za dhamana za Serikali, sifa za mkopaji na hatari ya mkopaji kutolipa mkopo pamoja na kasi ya mfumuko wa bei.
Aidha Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuwa kutoa maelekezo kwa mabenki kutumia viwango fulani vya riba katika biashara zao, kutaifanya Benki Kuu kukosa nguvu na mamlaka ya kuyachukulia mabenki hatua endapo yatapata hasara kwa kutumia riba ambayo Benki Kuu imeelekeza.
Vile vile amesema kuwa kiwango cha hatari ya kutolipa mkopo ni miongoni mwa vigezo vinavyotumiwa na mabenki katika kupanga viwango vya riba za mikopo, ambapo kwa sehemu kubwa gharama za riba za mikopo hutegemea zaidi gharama za upatikanaji wa fedha pamoja na gharama za uendeshaji.
Pia amesema kuwa, ni muhimu kutambua kwamba kadri riba za mikopo zinapokuwa juu, ndivyo riba za amana zinapokuwa juu pia, ambapo wastani wa riba za kukopa kwa mwaka mmoja mwezi Juni, 2016 ulikuwa asilimia 13.67 wakati wastani wa riba za amana za mwaka mmoja ulikuwa asilimia 11.52 ikiwa ni tofauti ya asilimia 2.25.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WIZARA YA AFYA YAZINDUA VIPINDI VYA RADIO KUPINGA UKEKETAJI
WIZARA YA AFYA YAZINDUA VIPINDI VYA RADIO KUPINGA UKEKETAJI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYT3Sr_VYoMlnteqm2uYNpKJZ78YvuDUIfFIZrt-Gyx_-epHQWceTQA8fEJR-1WEQ1suyAEjxA4BBug0btjzqr5lem_sT4U9j4bFdmkvqfaShNz03PbXSKyJ3H9BLWES91ns7XsB2QJTY/s1600/ashatu-Kijaji.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYT3Sr_VYoMlnteqm2uYNpKJZ78YvuDUIfFIZrt-Gyx_-epHQWceTQA8fEJR-1WEQ1suyAEjxA4BBug0btjzqr5lem_sT4U9j4bFdmkvqfaShNz03PbXSKyJ3H9BLWES91ns7XsB2QJTY/s72-c/ashatu-Kijaji.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/wizara-ya-afya-yazindua-vipindi-vya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/wizara-ya-afya-yazindua-vipindi-vya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy