JUKWAA LA NISHATI TANZANIA KUTOA SEMINA KWA WABUNGE
HomeJamii

JUKWAA LA NISHATI TANZANIA KUTOA SEMINA KWA WABUNGE

Na Mwandishi Wetu JUKWAA la Nishati Tanzania linatarajia kutoa semina kwa wabunge ili wapate uelewa wa nishati na changamoto zake...

RAIS DKT MAGUFULI ATOA MKONO WA POLE KWA FAMILIA YA MRISHO GAMBO
TGGA WAMUAGA BOSS WA GIRL GUIDES AFRIKA KWA HAFLA KABAMBE
MZALISHAJI MBEGU APATA TUZO YA UJASIRIAMALI YA CITI FOUNDATION




Na Mwandishi Wetu

JUKWAA la Nishati Tanzania linatarajia kutoa semina kwa wabunge ili wapate uelewa wa nishati na changamoto zake, watakapokuwa wanajibu maswali ama kuuliza wafanye hivyo kwa manufaa ya taifa.

Mratibu wa Jukwaa hilo nchini ambaye ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Hudson Nkotagu alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu shughuli wanazozifanya.

Profesa Nkotagu alisema wanaamini wabunge wakipata uelewa kuhusu nishati pale watakapokuwa wakijadili masuala hayo bungeni watakuwa na uelewa mpana, na maamuzi yake yatakuwa kwa manufaa ya taifa.

Pia alisema semina hizo zitatolewa kwa viongozi wakuu, watendaji wa serikali kutoka sekta za viwanda, mazingira, serikali za mitaa, wawekezaji pamoja na wafanya biashara mbalimbali.

Alisisitiza kuwa wananchi wengi hawana uelewa wa nishati kwamba kuna za aina mbili, aina ya kwanza inatokana na vyanzo vya nishata ambavyo vikitumika vinapoisha havirudi tena mfano gesi, mafuta, mkaa wa mawe pamoja na urani.

Na aina nyingine ni ile inayotokana na vitu ambavyo vinajiendeleza vyenyewe kiasili kwa mfano nishati ya sola, upepo, maji, mawimbi ya bahari na kuni.

“Nishati hizi zinajiendeleza kiasili. Kwa bahati nzuri zote tunazo katika nchi yetu. Tanzania imejaliwa kuwa na vyanzo vyote vya nishati, vinahitajika tu kuendelezwa,” alisema.

Alisema jukwaa hilo linashirikisha UDSM, Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT), Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST), pamoja na vyuo vikuu vine kutoka nchini Uholanzi ambavyo ni Twente, Ultreacht, Hanze na Delft.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: JUKWAA LA NISHATI TANZANIA KUTOA SEMINA KWA WABUNGE
JUKWAA LA NISHATI TANZANIA KUTOA SEMINA KWA WABUNGE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhfFK4MdiXetFEbKPF9eePWQCvv6tNjABwR_IO3ascyVNsS0jAJ7bk2ge-o7ZHbG6M8rHqER2RUzqeYRxeXrs3q6c6tE_58WVw2fXsuVFdF85X9m6i2_6fziAcoLNGQjkrK7ewCtpiwEiQd/s640/picha%252Bbunge.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhfFK4MdiXetFEbKPF9eePWQCvv6tNjABwR_IO3ascyVNsS0jAJ7bk2ge-o7ZHbG6M8rHqER2RUzqeYRxeXrs3q6c6tE_58WVw2fXsuVFdF85X9m6i2_6fziAcoLNGQjkrK7ewCtpiwEiQd/s72-c/picha%252Bbunge.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/02/jukwaa-la-nishati-tanzania-kutoa-semina.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/02/jukwaa-la-nishati-tanzania-kutoa-semina.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy