TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA OPEN HEART YA NCHINI AUSTRALIA YAFANYA UPASUAJI WA WAGONJWA 11 WA MOYO
HomeJamii

TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA OPEN HEART YA NCHINI AUSTRALIA YAFANYA UPASUAJI WA WAGONJWA 11 WA MOYO

Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Taasisi ya Open...

WAREMBO WAJIPANGA NA SHINDANO LA MREMBO ASILIA KUNDUCHI
MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA WAZIRI CANNON
MAMA SAMIA AHUDHURIA HAFLA YA CHAKULA CHA MCHANA NDANI YA MELI YA MFALME WA OMAN ILIYOTIA NANGA BANDARI YA DAR ES SALAAM
Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Taasisi ya Open Heart International ya nchini Australia (OHI) wakifanya upasuaji wa kuziba matundu ya moyo kwa mgonjwa wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo inayoendelea katika Taasisi hiyo. Tangu kuanza kwa kambi hiyo tarehe 12/03/2017 hadi leo tarehe 14/03/2017 jumla ya wagonjwa 11 wamefanyiwa upasuaji kati ya hao watoto ni tisa na watu wazima wawili. (PICHA NA ANNA NKINDA-JKCI).
 

Madaktari bingwa wa upasuaji wa magonjwa ya moyo  kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Taasisi ya Open Heart International ya nchini Australia (OHI) wakifanya upasuaji wa kuvuna mshipa wa damu mguuni kwa mgonjwa wa moyo na kuupandikiza katika mishipa ya moyo iliyoziba kwa jina la kitaalamu Coronary Artery Bypass Graft (CABG). Tangu kuanza kwa kambi hiyo tarehe 12/03/2017 hadi leo tarehe 14/03/2017 jumla ya wagonjwa 11 wamefanyiwa upasuaji kati ya hao watoto ni tisa na watu wazima wawili.

NA ANNA NKINDA - JKCI
JUMLA ya wagonjwa 11 wamefanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ushirikiana na madaktari wenzao wa Taasisi ya Open Heart International ya nchini Australia.
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Upasuaji wa Moyo ambaye pia ni Daktari bingwa wa upasuaji wa Moyo Bashir Nyangasa, (wakwanza kushoto pichani juu), wakati akielezea jinsi kambi hiyo ya upasuaji inavyoendelea kutoa matibabu kwa wagonjwa.
Dkt. Nyangasa alisema, “Kwa kushirikiana na washirika wetu wa OHI tulianza kambi maalum ya upasuaji kuanzia tarehe 10/03/2017 hadi leo  tarehe 17/3/2017 tumefanya  upasuaji kwa wagonjwa 11 ambao wanaendelea vizuri,  kati ya hao watoto ni tisa na watu wazima ni wawili”,.
Dkt. Nyangasa alisema  katika kambi hiyo  ambayo inamalizika tarehe 17/3/2017 walipanga kufanya upasuaji kwa wagonjwa 25 kati ya hao watoto ni 15 na watu wazima ni 10.
Kuhusu uhitaji  wa damu kwa wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa Moyo Dkt. Nyangasa alisema wagonjwa hao wanahitaji damu nyingi hivyo basi aliwaomba wananchi wajitokeze kuchangia  damu ambayo itatumika kwa wagonjwa.
“Tunaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kuchangia damu na  uchangiaji huu wa damu  usifanyike mara moja bali  uwe endelevu  kwani Taasisi inatoa huduma kwa wagonjwa wakati wote siyo wakati wa kambi maalum za matibabu ya moyo pekee yake”, alisisitiza Dkt. Nyangasa.
Tangu kuanza kwa mwaka huu  wa 2017 JKCI kwa kushirikiana na baadhi ya washirika wake wa nje ya nchi ambao ni  Madaktari  Afrika wa  Marekani, Hospitali za  Apolo Bangalore na BLK zote za nchini  India na Open Heart International ya Australia wamefanya  matibabu ya moyo ya kufungua na bila kufungua kifua kwa wagonjwa wa moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA OPEN HEART YA NCHINI AUSTRALIA YAFANYA UPASUAJI WA WAGONJWA 11 WA MOYO
TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA OPEN HEART YA NCHINI AUSTRALIA YAFANYA UPASUAJI WA WAGONJWA 11 WA MOYO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiZDPRkLItSaxpLag5wVMHW_8XZWtHPqMqvzms9Q_tgA6WMHWK_HA6wVmsmDfTmmF49k62S4ZckLNklAKEeaytDWn9RhwtAxeEp8wa_lfX6lA5ZdZiOkKqs_ZYhu8I1sVmT4PpwBBFSA7c/s640/OHI+3.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiZDPRkLItSaxpLag5wVMHW_8XZWtHPqMqvzms9Q_tgA6WMHWK_HA6wVmsmDfTmmF49k62S4ZckLNklAKEeaytDWn9RhwtAxeEp8wa_lfX6lA5ZdZiOkKqs_ZYhu8I1sVmT4PpwBBFSA7c/s72-c/OHI+3.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/taasisi-ya-moyo-jakaya-kikwete-kwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/taasisi-ya-moyo-jakaya-kikwete-kwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy