OPERESHENI YA VIROBA YAENDELEA JIJINI DAR ES SALAAM
HomeJamii

OPERESHENI YA VIROBA YAENDELEA JIJINI DAR ES SALAAM

Na Lilian Lundo – MAELEZO Serikali inaendelea na operesheni ya kukagua viwanda vinavyotengeneza pombe zilizo kwenye vifungashio vya mi...

WITO KWA WALIOKUWA WAFANYAKAZI WA ULIOKUWA MGODI WA DHAHABU BULYANHULU UPIMAJI ULIOFANYIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI
MAKAMU WA RAIS WA BENKI YA DUNIA KANDA YA AFRIKA AWASILI KUSHIRIKI UZINDUZI WA MABASI YA MWENDO KASI-BRT
KIJIJI CHA MWANZENGA MKOA WA PWANI KUPATA UMEME WA REA

Na Lilian Lundo – MAELEZO

Serikali inaendelea na operesheni ya kukagua viwanda vinavyotengeneza pombe zilizo kwenye vifungashio vya mifuko ya plastiki maarufu kama  “viroba” ili kujiridhisha kama viwanda hivyo vimesitisha uzalishaji wa pombe hizo pamoja na kuzuia utokaji wa pombe ambazo bado zipo katika maghala.

Hayo yamesemwa na Mwanasheria wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Manchale Heche alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wakati wa operesheni hiyo ambayo inaendelea Jijini Dar es Salaam.

“Zoezi linaendelea kama lilivyoanza jana ambapo tunakagua viwanda vinavyozalisha viroba, na mpaka sasa tumeshatembelea viwanda vitatu ambavyo ni kiwanda cha Kibo Spirit kinachotengeneza pombe ya kiroba aina ya Double Panch, Kiwanda che Blue Nile kinachotengeneza  viroba vya Kitoko na Rivella pamoja na kiwanda cha True Bell kinachotengeneza viroba vya Bonanza na Suke,” alifafanua Heche.

Aliendelea kwa kusema kuwa lengo la operesheni ni kukagua viwanda vyote vinavyozalisha pombe aina ya viroba ili kujiridhisha ikiwa viwanda hivyo vimetekeleza agizo la Serikali la kusimamisha uzalishaji wa pombe hizo kuanzia Machi 01, mwaka huu.

Heche amesema kuwa operesheni hiyo pia inahusisha ukaguzi kutambua idadi ya pombe zilizobaki katika maghala mbalimbali na kuzuia pombe hizo kutotolewa katika maghala hayo mpaka hapo Serikali itakapotoa agizo ya namna ya kuziharibu pombe hizo.

Aidha amesema kuwa agizo limetoka katika mipaka yote ya nchi kuzuia uingizaji wa pombe hizo na kuzirudisha nchi zilizotoka kwa gharama za muhusika aliyesafirisha pombe hizo.

Kwa upande wake Meneja Uendeshaji wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited  kilichopo Shekilango, Godwin Mungere amesema kuwa kiwanda hicho bado kilikuwa katika majaribio lakini kutokana na agizo la Serikali wamesitisha uzalishaji wa pombe za viroba ambapo wao walikuwa wakizalisha viroba aina ya Bonanza na Suke.

Ameeleza kuwa akiba ya pombe za viroba vilivyobaki katika ghala lao ni katoni 166 za viroba vya Bonanza na katoni 165 za viroba vya Suke ambapo wanasubiri maelekezo kutoka Serikalini namna ya kuharibu pombe hizo.

Nae, Mkurugenzi wa Kibo Spirit kilichopo Sinza kwa Remmy Muhid Mwacha amesema kuwa kiwanda hicho kilikuwa bado kipo kwenye majaribio ya kutengeneza viroba aina ya Double Panch lakini kwa sasa hawaendelei na uzalishaji wa pombe hizo ila kiwanda hicho kwa sasa kinazalisha maji ya kunywa ya Kibo Cool.

Operesheni ya viroba ilianza rasmi jana kwa mkoa mzima wa Dar es Salaam ambapo ni utekelezaji wa agizo la Serikali la kuzuia uzalishaji, usambazaji na utumiaji wa pombe hizo kuanzia Machi 1, mwaka huu. Adhabu ya kutumia, kusambaza au kuzalisha pombe hizo ni faini inayoanzia shilingi elfu 50 mpaka milioni 5 na kifungo cha kuanzia miezi 3 mpaka miaka 3 jela.

Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Manchare Heche (kushoto) akikagua nyaraka toka kwa Msimamizi wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited Bw. Godwin Mungere mapema leo hii jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.



Baadhi ya Maafisa wa Serikali wakikagua ghala la Kiwanda cha True Bell (T) Limited mapema hii leo Jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika. 



Msimamizi wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited, Godwin Mungere (mwenye shati la njano) akionesha baadhi ya vifungashio vya pombe kali aina ya kiroba mapema hii leo Jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika, kulia ni Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Manchare Heche.


 
Baadhi ya shehena ya maboksi ya pombe ya viroba aina ya bonanza ikiwa imehifadhiwa katika ghala la kiwanda cha True Bell (T) Limited kilichopo Sinza Bamaga mapema leo hii jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya opereshe
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: OPERESHENI YA VIROBA YAENDELEA JIJINI DAR ES SALAAM
OPERESHENI YA VIROBA YAENDELEA JIJINI DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6FQlRDzDbFRO2BZ5Z5Ko8ORkXNZmMSzbpIstZxc7q7KAbOMl0tI3jq9IYJ6RsVhq2AJNdg1GBUy-iIRMx-3fnesbEHRlstVh709JndqduaapzhOujZBpkwioMIpOb6eah34PDCqm4faA/s640/Viroba+01.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6FQlRDzDbFRO2BZ5Z5Ko8ORkXNZmMSzbpIstZxc7q7KAbOMl0tI3jq9IYJ6RsVhq2AJNdg1GBUy-iIRMx-3fnesbEHRlstVh709JndqduaapzhOujZBpkwioMIpOb6eah34PDCqm4faA/s72-c/Viroba+01.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/operesheni-ya-viroba-yaendelea-jijini.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/operesheni-ya-viroba-yaendelea-jijini.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy