MAKAMU WA RAIS WA BENKI YA DUNIA KANDA YA AFRIKA AWASILI KUSHIRIKI UZINDUZI WA MABASI YA MWENDO KASI-BRT
HomeJamii

MAKAMU WA RAIS WA BENKI YA DUNIA KANDA YA AFRIKA AWASILI KUSHIRIKI UZINDUZI WA MABASI YA MWENDO KASI-BRT

  Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akiwa na Mgeni wake ambaye ni Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshugh...

MAZISHI YA SIR GEORGE CLEMENT KAHAMA JIJINI DAR ES SALAAM
RC RUGIMBANA: VYUO VITOE USHIRIKIANO WA KUTOSHA KWA HESLB
KIKOSI 841KJ MAFINGA KIMESHEREKEA MIAKA 50 TOKA KUANZISHWA KWAKE KWA KUJENGA KIWANDA CHA NAFAKA


 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akiwa na Mgeni wake ambaye ni Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika Bw. Makhtar Diop, wakiwa katika chumba cha kupumzikia wageni maalumu katika Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Nyerere, Jijini Dar es salaam. Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Burundi, Somalia na Malawi Bi. Bella Bird.
 Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika Bw. Makhtar Diop, (wa pili kushoto aliyeshika dafu) alipowasili nchini, akiwa na mwenyeji wake Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (wa tatu kushoto) ambapo anatarajiwa kushiriki katika uzinduzi wa Mradi wa mabasi yaendayo haraka BRT, Januari 25, 2017, na baadaye kufanya mazungunzo na Waziri huyo alasiri.
 Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika Bw. Makhtar Diop, (kushoto) akinywa maji ya dafu  alipowasili nchini, akiwa na mwenyeji wake Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (kulia) ambapo anatarajiwa kuungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, katika uzinduzi wa Mradi wa mabasi yaendayo haraka BRT, Januari 25, 2017.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akiteta jambo na Mkurugenzi Mkazi, baada ya mapokezi ya Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Bw. Makhtar Diop.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)
Benny Mwaipaja, WFM, Dar es salaam
24. Januari 2017

Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia masuala ya Kanda ya Afrika, Bw. Makhtar Diop, amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu ambapo pamoja na mambo mengine, anatarajia kushiriki uzinduzi wa Mradi wa Mabasi yaendayo haraka tukio linalotarajiwa kufanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Jijini Dar es Salama kesho asubuhi.

Makamu huyo wa Rais wa Benki ya Dunia,  amelakiwa na Mwenyeji wake, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango kati Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo anayehudumu katika Nchi za Tanzania, Burundi, Somalia na Malawi, Bi. Bella Bird.

Akiwa nchini, Bw. Diop atakutana na kufanya mazungumzo pia Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango,  Gavana wa Benki Kuu, Profesa Benno Ndulu, Sekta Binafsi ambapo mazungumzo yao yanatarajiwa kujikita katika Miradi kadhaa ya maendeleo inayofadhiliwa ama kugharamiwa na Benki hiyo kwa njia ya ruzuku na mikopo yenye masharti nafuu ambayo mpaka sasa inakadiriwa kufikia thamani ya Dola Bilioni 4 nukta 7 .
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAKAMU WA RAIS WA BENKI YA DUNIA KANDA YA AFRIKA AWASILI KUSHIRIKI UZINDUZI WA MABASI YA MWENDO KASI-BRT
MAKAMU WA RAIS WA BENKI YA DUNIA KANDA YA AFRIKA AWASILI KUSHIRIKI UZINDUZI WA MABASI YA MWENDO KASI-BRT
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimyoGUcKjGDdTzXWpBkv6paRR2SqcAH6QQZAY4nWdUMxsAhznHUYmoQMapbvKLH10gsMaYm1VF2GLdDJEz8t88pIcv7QImseV1bZMgaKIE5c8e6p5Zu2MIbWOwBulKVe8-JylzVhj2JjBV/s640/IMG_4738.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimyoGUcKjGDdTzXWpBkv6paRR2SqcAH6QQZAY4nWdUMxsAhznHUYmoQMapbvKLH10gsMaYm1VF2GLdDJEz8t88pIcv7QImseV1bZMgaKIE5c8e6p5Zu2MIbWOwBulKVe8-JylzVhj2JjBV/s72-c/IMG_4738.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/01/makamu-wa-rais-wa-benki-ya-dunia-kanda.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/01/makamu-wa-rais-wa-benki-ya-dunia-kanda.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy