KIJIJI CHA MWANZENGA MKOA WA PWANI KUPATA UMEME WA REA
HomeJamii

KIJIJI CHA MWANZENGA MKOA WA PWANI KUPATA UMEME WA REA

Na Mwandishi Wetu, Mkuranga KIJIJI cha Wasanii cha Mwanzega kimechaguliwa kuwemo kwenye orodha ya vijiji saba ambavyo vimepang...

TRA YAENDELEA KUWABAMBA WASIOTOA RISITI ZA MACHINE ZA KIELEKRONIKI
MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ATEMBELEA BANDA LA PROPERTY INTERNATIONAL, MAONYESHO YA SABASABA
RAIS DK. SHEIN AONDOKA NCHINI LEO NA KUELEKEA UINGEREZA KWA ZIARA MAALUM


KIJIJI CHA MWANZENGA MKOA WA PWANI KUPATA UMEME WA REA
Na Mwandishi Wetu, Mkuranga
KIJIJI cha Wasanii cha Mwanzega kimechaguliwa kuwemo kwenye orodha ya vijiji saba ambavyo vimepangiwa kupata umeme wa Serikali wa Mamlaka ya Umeme Vijijini (REA).

Mtendaji wa kijiji cha Mwanzega, Kitwana Kambangwa aliwaomba wanakijiji wasipuuzie fursa hiyo kwa vile serikali imeona umuhimu wa kijiji hicho kupata umeme ili kurahisisha maendeleo.

Akiwasomea wananchi taarifa ya Mratibu wa Vijiji na Kata wa Utawala bora na maboresho wa wilaya ya Mkuranga kuhusu mradi huo, Mtendaji wa kijiji, Kambangwa alisema wananchi wewe tayari kutoa miti yao ya mazao na mimea bila fidia ili kupisha kazi ya kupitisha nguzo za umeme wa REA.

'Ndugu zangu Serikali ya Rais John Magufuli imetusikia kilio chetu sisi watu wa vijijini, tunaletewa umeme ili tuwe na maendeleo kama wenzetu wa mjini, tusiipuzie nafasi hii kubalini kupisha nguzo zipite bila kulalamikia fidia' alisema Mtendaji Kambangwa.

Alisema sambamba na kijiji cha Mwanzega, vijiji vingine vitakavyonufaika na mradi wa REA ni Mbezi, Msorwa, Shungubweni, Boza, Kuruti na Mbonga ambavyo mradi huo utapelekwa moja kwa moja kwenye shule za Msingi, Zahanati, Viwanda na Shule za Sekondari.

Awali wakichangia kuhusu mradi huo Dkt.Frederick Mwakibinga alisema umeme ukishaingia kijijini baada ya muda mfupi kutakuwa na maendeleo ambayo yatawanufaisha wananchi wote na kaongeza ajira kwa vijana.
Mwanakijiji mwingine Ramadhani Mwanehekwa alisema wao wako tayari kuruhusu mazao yao kukatwa bila kudai fidia lakini Serikali nayo iwakumbuke katika kuwaletea wananchi huduma za jamii, kama zahanati, barabara, maji na elimu.

Mkutano huo uliohudhuriwa na wanakijiji wengi waume, wanawake na vijana, Ali Ndambwe aliwashauri wanakijiji wenzake wasifikirie kulipwa  fidia kwa ajili ya mazao zitakapopita nguzo waangalie faida watakayoipata vijana wao na majukuu baada ya kuingia umeme na kujengewa viwanda.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA), Cassim Taalib aliwapongeza wanakijiji wenzake kukubali kutoa mazao na mimea yao bure kwa wale ambao mradi wa umeme utawapitia.

Katika mkutano huo Mwenyekiti wa kijiji, Abdallah Mwangira aliwataarifu wananchi hao kuwa serikali imewaandalia wananchi wa vijiji hivyo mambo makubwa ya maendeleo ambayo aliahidi kuyasema kikao kijacho.
Kijiji cha Mwanzega ndipo kilipo kijiji cha wasanii ambacho mpaka sasa zimejengwa nyumba 250 za kisasa as wasanii ambazo zitaingia kwenye mradi wa REA.

Mkazi wa Mwanzega Dkt. Frederick Mwakibinga akichangia mada kwa wanakijiji watakaonufaika na mradi huo baada ya kuukubali.



Wanakijiji wa kijiji cha Wasanii Mwanzega Mkuranga wakiwa kwenye mkutano wa kuidhinisha mradi wa Ilene wa REA kupita kijijini hali jana.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KIJIJI CHA MWANZENGA MKOA WA PWANI KUPATA UMEME WA REA
KIJIJI CHA MWANZENGA MKOA WA PWANI KUPATA UMEME WA REA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgxscatwOjjoUSpzERiBT-CB46qKyI80N4LzBaclskDXhK_wzzqAMi-WWPXHzPIu5S1Tmbtg8h-aIhziHpinnPpmjiXTyX7ODmsPUcV7TooWHz_Lo_UsnHa9DEiuUazg5_CG8uBm7jW1h2/s640/20170123_111038.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgxscatwOjjoUSpzERiBT-CB46qKyI80N4LzBaclskDXhK_wzzqAMi-WWPXHzPIu5S1Tmbtg8h-aIhziHpinnPpmjiXTyX7ODmsPUcV7TooWHz_Lo_UsnHa9DEiuUazg5_CG8uBm7jW1h2/s72-c/20170123_111038.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/01/kijiji-cha-mwanzenga-mkoa-wa-pwani.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/01/kijiji-cha-mwanzenga-mkoa-wa-pwani.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy