WAZIRI MKUU AZUNGUMZA NA MABALOZI, AWATAKA WAKATAFUTE WAWEKEZAJI
HomeJamii

WAZIRI MKUU AZUNGUMZA NA MABALOZI, AWATAKA WAKATAFUTE WAWEKEZAJI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka mabalozi wa Tanzania katika nchi mbalimbali kuhakikisha wanatumia uwakilishi wao kutafuta wawe...

ALIYEKUWA KIONGOZI KITENGO CHA MAGONJWA YA DHARULA CHUMBA CHA UPASUAJI MNH, AWAPIGA MSASA WAFANYAKAZI
WAZIRI MKUU AAGIZA VIONGOZI NCHINI WATOE TAARIFA
KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI DKT. MASHINGO AWATAKA WAFUGAJI KUHAKIKISHA IFIKAPO JANUARI 31 MIFUGO YOTE NCHINI IWE IMEPIGWA CHAPA


WAZIRI MKUU AZUNGUMZA NA MABALOZI, AWATAKA WAKATAFUTE WAWEKEZAJI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka mabalozi wa Tanzania katika nchi mbalimbali kuhakikisha wanatumia uwakilishi wao kutafuta wawekezaji watakaokuja kuwekeza katika sekta ya viwanda nchini.
Amesema  mkakati wa Serikali ni kuimarisha uchumi  hadi wa kati kupitia sekta ya viwanda, hivyo jukumu la mabalozi hao ni kuhakikisha jambo hilo linafanikiwa.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Februari 7, 2017) alipokutana na mabalozi wa wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi za Uturuki, Brazil, China, Italy, Ufaransa, Jamuhuri ya Kidemkrasi ya Congo (DRC) na Uswisi.
Mabalozi hao ni Balozi Dk. Emmanuel Nchini (Brazil), Balozi Elizabeth Kiondo (Uturuki), Balozi George Madafa (Italy), Balozi James Msekela (Uswisi),Balozi Samuel Shelukindo (Ufaransa), Balozi Paul Mella (DRC), Balozi Mbelwa Kairuki (China).
“Serikali inahitaji watu wa kuja kuwekeza katika viwanda ili kuongeza thamani ya mazao kabla ya kuyauza nje ya nchi, hivyo jukumu lenu ni kuhakikisha tunapata wawekezaji wenye sifa,” amesema.
Pia Waziri Mkuu amewataka mabalozi hao kutumia uwakilishi wao katika nchi hizo kwa kuhakikisha wanatangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili kuongeza idadi ya watalii wanaokuja Tanzania.
Aidha, Waziri Mkuu amewataka mabalozi hao kulinda maslahi ya Taifa katika nchi hizo ikiwa ni pamoja na kuimarisha uhusiano uliopo kati ya Tanzania na mataifa hayo.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka mabalozi hao kuhakikisha wanawatambua Watanzania wanaoishi katika mataifa hayo na kushirikiana nao katika kutafuta wawekezaji wa kuja kuwekeza nchini.
Kwa upande wake Balozi Mella ambaye alizungumza kwa niaba ya mabozi wenzake alimuhakikishia Waziri Mkuu kwamba watakwenda kutekeleza wajibu wao ipasavyo.


       
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 7, 2017.
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa akizungumza na mabalozi ambao wanaiwakilisha Tanzania nje ya nchi na wanatarajiwa kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi hivi karibuni, Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Februari 7, 2017 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa akizungumza na mabalozi ambao wanaiwakilisha Tanzania nje ya nchi na wanatarajiwa kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi hivi karibuni, Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Februari 7, 2017 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa akizungumza na mabalozi ambao wanaiwakilisha Tanzania nje ya nchi na wanatarajiwa kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi hivi karibuni, Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Februari 7, 2017 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa akizungumza na mabalozi ambao wanaiwakilisha Tanzania nje ya nchi na wanatarajiwa kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi hivi karibuni, Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Februari 7, 2017 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali baada ya kuzungumza nao Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Februari 7, 2017. Kutoka kushoto ni Samwel Shelukindo (Ufaransa), Dkt. James Msekela (Uswisi), Mbelwa Kairuki (China), Paul Mella (DRC), Dkt. Emmanuel Nchimbi (Brazil) George Madafa (Italy) na Elizabeth Kiondo (Uturuki). (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa akisalimiana na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi baada ya kuzungumza nao Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Februari 7, 2017 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa akisalimiana na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi baada ya kuzungumza nao Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Februari 7, 2017 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MKUU AZUNGUMZA NA MABALOZI, AWATAKA WAKATAFUTE WAWEKEZAJI
WAZIRI MKUU AZUNGUMZA NA MABALOZI, AWATAKA WAKATAFUTE WAWEKEZAJI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhG556H0LfJI2mjKuIbCHVK8zwtGoU02d37tIGuGb28EV8XR0874wXiUI2Zu8MG7Ggrqo3Ve20JXWxUFM5RGDaiN4N2FSvvqlCP0pVr9JQsBjpHYin5Q20kTlEp_7nYMlKdGX0IftaYdbU/s640/RG1A6025.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhG556H0LfJI2mjKuIbCHVK8zwtGoU02d37tIGuGb28EV8XR0874wXiUI2Zu8MG7Ggrqo3Ve20JXWxUFM5RGDaiN4N2FSvvqlCP0pVr9JQsBjpHYin5Q20kTlEp_7nYMlKdGX0IftaYdbU/s72-c/RG1A6025.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/waziri-mkuu-azungumza-na-mabalozi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/waziri-mkuu-azungumza-na-mabalozi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy