SERIKALI YA AWAMU YA TANO INAONGOZWA KWA NGUVU ZA MUNGU - LUHAGA MPINA
HomeJamii

SERIKALI YA AWAMU YA TANO INAONGOZWA KWA NGUVU ZA MUNGU - LUHAGA MPINA

  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira pamoja na wachungaji, wakiinua mikono wakati wa ibada ya Kuli...

WAKIMBIZI WA BURUNDI KUANZA KUREJEA KWAO SEPTEMBA 7 MWAKA HUU
KOREA KASKAZINI YATENGENEZA TETEMEKO KUBWA KULIKO LILE LA KAGERA
DKT. HARRISON MWAKYEMBE AMPONGEZA BALOZI WA CHINA, DKT. LU




 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira pamoja na wachungaji, wakiinua mikono wakati wa ibada ya Kuliombea Taifa Kinziga, Salasala Jijini Dar es Salaam.
 
 
 Mwimbaji Alfonsina Samweli wa kanisa la Assemblies of God la Kinziga Salasala Jijini Dar es Salaam akimpa Mkono Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina, baada ya kumkabidhi kabrasha lenye DVDs zenye nyimbo za Injili wakati wa ibada ya Kuliombea Taifa.
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akikata Utepe katika CD kuashiria kuzinduliwa kwa Abum ya Nyimbo za Injili za mwimbaji Alfonsina Samweli.
 
 
Sehemu ya waumini wa kanisa la Assemblies of God la Salasala wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muugano na Mazingira Mhe. Luhaga  Mpina Hayupo Pichani wakati wa ibada maalumu ya kuiombea Taifa iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
 (Picha na Evelyn Mkokoi wa OMR)
Na Evelyn Mkokoi – Salasala DSM.
NAIBU  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina amesema Serikali ya awamu ya Tano inaongozwa na Nguvu za Mungu katika kuwatumikia wananchi wake na si vinginevyo.
Pia amesema  Serikali ya awamu ya Tano kamwe haitayumbishwa wala kuyumba katika kutenda yaliyomema kwa maendeleo ya nchi  kwa kuogopa maneno ya watu ya kuwakatisha tamaa.
Akizungumza Dar es Salaam jana wakati wa Uzinduzi wa Tamasha la Kusifu  na Kuabudu na kuliombea Taifa la Kanisa la Tanzania Assemblies  of God lililopo katika eneo la Kinzugi Salasala, alisema  Serikali itaendelea kusimamia misingi yake bila kuogopa maneno ya watu wanaoyoikatisha tamaa kwani Sheria na Katiba za nchi zinatokana na maneno yaliyopo  katika vitabu vya Mungu.
Alisema watumishi wa Mungu wanatakiwa kuwaombea viongozi katika kutenda kazi zao kwani uongozi waliokuwa nao ni uchaguzi kutoka kwa Mungu na sio kwa nguvu za mtu yeyote.
" Uongozi unatokana na  Mungu,Mimi Mpina sikujua kama ningekuwa Waziri nilimaliza siku mbili sikujua kama niliteuliwa kuwa Naibu Waziri kipindi hicho  nilikuwa shambani nikafatwa na kuambia kuwa nimechaguliwa ,nikasema ni uweza wa Mungu,"alisema na kuongeza kuwa 
"Utawala wa awamu ya tano tunemtanguliza mbele Mungu,tunaomba muendelee kutuombea tutekeleze majukumu yetu licha ya kuwepo kwa vikwazo mbalimbali katika kutekeleza majukumu yetu,"alisema Mpina
Aidha aliziomba familia za wakristo kuwa mfano wa kuigwa katika utunzaji wa mazingira kwani bila kuwepo kwa mazingira safi magonjwa yatapata nafasi katika jamii.
"Familia za Kikristo lazima  ziwe mfano wa kuigwa katika utunzaji wa mazingira, hizi faini tunazowapiga watu kutokana na ukiukwaji wa sheria za mazingira kwa uchafuzi  wa Mazingira, sio kama tunawaonea bali kuwakumbusha wajibu wao "alisema.
Kwa Upande wake,Mchungaji wa Kanisa la Assembly of God , Deusi Sabuni alisema  watahakikisha wanaendele kufanya Maombi kuiombea serikali ya awamu ya tano na viongozi wake.
Alisema roho za uadui zilizopo na watu kusema vibaya na kuwakatisha tamaa kusiwavunje mioyo kwa kusikiliza  maneno ya watu katika kuleta maendeleo ya nchi kwa manufaa ya taifahili na watu wake."Makanisa na Misikiti tupo pamoja nanyi katika kuwaombea na kama serikali hii ikiendelea hivi ndani ya miaka mitatu nchi yetu itabadilika,"alisema Mch.Sabuni.
Ibada maalum ya Kuliombea Taifa, kusifu pamoja na kuimba, ilienda sambamba na uzinduzi wa Ablum ya nyimbo za injili za mwimbaji Alfonsina Samweli pamoja na mnadawa kuuza DVDs zenye nyimbo za injili.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI YA AWAMU YA TANO INAONGOZWA KWA NGUVU ZA MUNGU - LUHAGA MPINA
SERIKALI YA AWAMU YA TANO INAONGOZWA KWA NGUVU ZA MUNGU - LUHAGA MPINA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-ijaZ1PZj_ffT8p0wwT4tdUaDLWwEajL1abGQp0YbCOfoIR5zMFTzz7uHHgBXF52Fe4oNdPFZ03Cw7-6N1Nr4kyWP43ZtoKY8Ud_LDZRvGCWynRzZpmRV4vSYJPcYgq5816YUhzKAek8-/s640/unnamed+%252853%2529.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-ijaZ1PZj_ffT8p0wwT4tdUaDLWwEajL1abGQp0YbCOfoIR5zMFTzz7uHHgBXF52Fe4oNdPFZ03Cw7-6N1Nr4kyWP43ZtoKY8Ud_LDZRvGCWynRzZpmRV4vSYJPcYgq5816YUhzKAek8-/s72-c/unnamed+%252853%2529.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/serikali-ya-awamu-ya-tano-inaongozwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/serikali-ya-awamu-ya-tano-inaongozwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy