CHUO CHA SANAA BAGAMOYO HATARINI KUMEZWA NA BAHARI
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina Pamoja na ujumbe wake na Viongozi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo wakiangalia eneo la fukwe la chuo icho ilivyoliwa na bahari ikiwa ni athari zitokanano na mabadiliko ya tabia nchi. Mpina alitembelea taasisi hiyo leo.
HomeJamii

CHUO CHA SANAA BAGAMOYO HATARINI KUMEZWA NA BAHARI

Na Evelyn Mkokoi - Bagamoyo SERIKALI imeiagiza Baraza la hifadhi ya Mazingira  (NEMC ) na Idara ya Mazingira   Ofisi ya Makamu wa R...

WAZIRI MKUU AZINDUA MAABARA YA KUPIMA MADINI
MAJALIWA ATEMBELEA OFISI ZA MPIGA CHAPA WA SERIKALI, PIA KITUO CHA ZIMAMOTO NA UOKOAJI JIJINI DAR ES SALAAM
SPIKA NDUGAI AKUTANA NA WATENDAJI WAKUU KUTOKA BOT, MAKAMU WA RAIS BUNGE LA AFRIKA NA UMOJA WA WACHIMBAJI MADINI TANZANIA.




Na Evelyn Mkokoi - Bagamoyo
SERIKALI imeiagiza Baraza la hifadhi ya Mazingira  (NEMC ) na Idara ya Mazingira  Ofisi ya Makamu wa Rais kufanya tathimini ya awali ya kuangalia ni namna gani itaweza  kuzuia maji ya bahari kuingia katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)  na kuharibu miundombinu yake ambapo hadi sasa takribani mita
70 hadi 100 ya bahari imeisogelea taasisi hiyo.

Akizungumza  jana wilayani Bagamoyo, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na
Mazingira Luhaga Mpina wakati wa ziara ya kutembelea Taasisi hiyo na kujionea ni namna gani bahari inavyosogea katika taasisi hiyo na kuanza kuathiri baadhi ya majengo.

Alisema  kutokana na hali hiyo kuwa ya dharura ameziagiza mamlaka hizo kufanya tathimini ya awali
ambapo kufikia Januari 30 mwakani  watapaswa kukabidhi ripoti ya awali kwa  serikali na kujua nini
kifanyike katika kunusuru taasisi hiyo na kuifanya mahala pazuri pa kujifunzia masuala ya utamaduni.
Mpina alisema ripoti hiyo itaweza kupelekwa serikalini ili mipango madhubuti  ianze kufanyika ya

kuhakikisha taasisi hiyo inakuwepo na inaendelea kutoa mafunzo yake kama kawaida bila kuathiriwa
na usogelewaji wa bahari katika maeneo hayo.
"Januari 30 mwakani tutapata hiyo ripoti na kuipeleka serikalini na kuangalia ni namna gani
tutakavyonusuru taasisi hiyo na kama kutahitajika utafiti mwingine wa kina kuhusiana na jambo hili
utaweza kufanyika na kujua nini  kifanyike katika maeneo haya kama kutengeneza Makinga maji au
Ukuta,"alisema Mpina
Alisema hali ya bahari kuhamia katika maeneo ya nchi kavu  inatokana na kuwepo kwa mabadiliko ya
tabia nchi yanayotokea baharini ambapo kwa sasa  kina cha bahari kimeweza kuongezeka kufikia

Sentimita 19 na kusababisha madhara ya maji kusogea katika maeneo ya nchi kavu.
 Mpina alisema takribani majengo matatu ya taasisi hiyo yapo hatarini  kuathirika ambayo  yanajumla
ya thamani ya kiasi cha sh. Bilioni 1.6 ambapo yatasababisha hasara kubwa kwa majengo pamoja na
taasisi hiyo.

Aidha  mpaka sasa kuna  baadhi ya fukwe tayari zimeanza kufanyiwa utaratibu wa kujengwa kwa 
kingo zikiwemo fukwe za Pangani Tanga, Kilimani Zanzibar, Kisiwa Panza Pemba, pamoja na fukwe za 
Ocean road Dar es Salaam. 

Kwa Upande wake Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, Dkt. Herbert Makoye
alisema taasisi yao inatatizo kubwa ya kusogelewa na bahari na kusababisha athari kubwa katika
baadhi ya madarasa.
Alisema kwa sasa bahari inazidi kusogelea chuo hali inayotishia uwepo wa chuo hicho endapo jitihada
dhabiti hazitaweza kuchukuliwa kwani hadi sasa uoto wa asili umeanza kutoweka kidogo kidogo.
Wakati huohuo,  Kufuatia malalamiko ya wakazi wa kata ya Bunju, Naibu Waziri Mpina alitembelea maeneo hayo yanayoathiriwa kwa kiasi kikubwa na maji ya mvua, na kuharibu miundombinu na mazingira na kupelekea afya za wakazi wa maeneo hayo kuwa hatarini kuathiriwa na magonjwa, Hali ambayo ilimlazimu Mpina kutoa agizo kwa NEMC, Idra ya Mazingira Ofisi ya Makmu wa Rais na Manispaa ya Kinondoni kufanya Tathnini ya mazingira katika eneo hilo na kuja na mpango mkakati wa muda mfupi na mrefu ili kuweza kunusuru hali hiyo.
Mpina aliwaasa wakazi wa eneo hilo pia kuzingatia ujenzi wa mipango miji na kuacha njia za maji na maeneo oevu.


Katika Picha Eneo la Fukwe ya Bagamoyo upande wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni linavyotishiwa kuharibika vibaya kutokana na athari za mabadiliko ya Tabianchi.

Dkt Herbert Makoye  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni ya Bagamoyo akiongea na vyombo vya habari kuhusu uhabifu wa fukwe utokanao na athari za mabadiliko ya tabia nchi.


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina Kiongea na Vyombo vya Habari katika fukwe ya Bagamoyo upande wa Taasisi ya Sanaa,namna ambayo majengo matatu ya chuo hicho yapo hatarini kumezwa na bahari kutokana na athari za mabadiliko a tabia nchi na kuomba msaada wa kitaalam kwa serikali hususan Ofii ya Makamu wa Rais. (Picha na Evelyn Mkokoi OMR).









Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: CHUO CHA SANAA BAGAMOYO HATARINI KUMEZWA NA BAHARI
CHUO CHA SANAA BAGAMOYO HATARINI KUMEZWA NA BAHARI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiY2JbFNdSjYFX_aFVZ5Vz2FQhpeQD01iWQXSzdHOjw12qZ6WhLMGoIW3RQNT2IN8ZyY4CyjiH_F2xJjsRrfAXZyj_WPzhLkmTcO1rrU4cbcHmcQNzm4zHfso4xEvOBgZ0IhWJXOM9IB74/s640/DSC_2704.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiY2JbFNdSjYFX_aFVZ5Vz2FQhpeQD01iWQXSzdHOjw12qZ6WhLMGoIW3RQNT2IN8ZyY4CyjiH_F2xJjsRrfAXZyj_WPzhLkmTcO1rrU4cbcHmcQNzm4zHfso4xEvOBgZ0IhWJXOM9IB74/s72-c/DSC_2704.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/chuo-cha-sanaa-bagamoyo-hatarini.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/chuo-cha-sanaa-bagamoyo-hatarini.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy