MENEJA WA DIAMOND APELEKWA MAHABUSU
HomeJamii

MENEJA WA DIAMOND APELEKWA MAHABUSU

Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imeamuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Tip Top Connect...

UN YAADHIMISHA MIAKA 71, YAAHIDI KUWEZESHA VIJANA
AJALI ZA BARABARANI ZAENDELEA KUUA NA KUACHA MAJERUHI MKOANI MWANZA.
WAZIRI MKUU MAJALIWA ATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MSAIDIZI WA MTENDAJI MKUU WA OFISI YAKE LEO


Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imeamuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Tip Top Connection ya jijini Dar es Salaam, Hamis Taletale a.k.a Babu Tale,  kurudishwa Mahabusu ya polisi mpaka Msajili wa Mahakama hiyo atakaporudi kutoka Dodoma.

Amri hiyo imetolewa leo na Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Lucy Massam baada ya Babu Tale na Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde kushindwa kufikia makubaliano licha ya msajili kuwapa muda wa dakika 10 pande zote wajadiliane namna ya kulimaliza suala hilo.

Babu Tale ambaye pia ni Meneja wa mwanamuziki maarufu wa Bongo Fleva Nassib Abdul 'Diamond Platnumz', amefikishwa mahakamani hapo leo akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi kusikiliza kesi inayomkabili.

Babu Tale, amekamatwa kutokana na amri iliyotolewa Februari 16 mwaka huu na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam Wilbard Mashauri iliyoamuru mtuhumiwa huyo na ndugu yake, Idd Taletale wakamatwe.

Amri hiyo pia, ilielekeza watuhimiwa hao wakikamatwa wapelekwe Gereza la Ukonga wakiwa wafungwa wa kesi ya madai, hadi hapo Mahakama hiyo itakapotoa maelekezo mengine.Hata hivyo, mtuhumiwa Babu Tale baada ya kufikishwa mahakamani hapo jana kesi yake ilishindikana kusikilizwa kwa kuwa Msajili Mashauri yuko Dodoma kikazi.

Kutokana na kushindwa kufikia muafaka baada ya dakika hizo kumi kuisha, Msajili Massam ameamuru babu Tale arudishwe mahabusu ya polisi mpaka Msajili Mashauri atakaporudi kwa ajili ya maelekezo mengine.

Hata hivyo kipindi chote cha majadiliano Babu Tale alikuwa katika mahabusu ya mahakama hiyo wakati ndugu zake wanajadiliana na mdai wake kabla ya kuieleza mahakama muafaka watakaofikia na kisha mahakama kutoa maelekezo.

Awali Mahakama hiyo iliwaamuru watuhumiwa hao kumlipa Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde kiasi cha Sh.milioni 250 baada ya kupatikana na makosa ya ukiukwaji wa haki za hakimiliki kwa kutumia masomo yake kibiashara bila ridhaa yake kinyume cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki.

Katika kesi ya msingi, Sheikh Mbonde alikuwa akidai kuwa aliingia mkataba na kampuni ya kina Babu Tale (Tiptop Connection) ili wamrekodi mahubiri yake kisha wayauze na kugawana mapato.Hata hivyo baada ya kurekodi masomo saba, walimkatia mawasiliano na alipowatafuta na kukutana nao wakamweleza kuwa wameamua kuachana na mpango huo.

Sheikh Mbonde alidai kuwa akiwa kwenye mahubiri Dodoma ndipo akakutana na mikanda ya video katika mfumo wa DVD yenye mahubiri yake huku kukiwa na namba za simu za viongozi hao wa Tiptop.

Sheikh Mbonde alidai baada ya kufanya uchunguzi alibaini kuwa DVD hizo zilikuwa zikiuzwa katika mikoa mbalimbali, ndipo akawafungulia kesi ya madai ya fidia kutokana ukiukwaji wa Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MENEJA WA DIAMOND APELEKWA MAHABUSU
MENEJA WA DIAMOND APELEKWA MAHABUSU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEipX_04pcX3pKJdNQGs1WsW09wyec-2GucwQz1UOU5sD76WJfJSzvD3WkWUHK16DOk1-DIq6eNns1tagN6cVrrAoHQwtMpXX9qV5xv1LzZiqfkcB2lp3fJ2RSOmfizie0932Jwkeb7xzZOc/s640/IMG_3183.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEipX_04pcX3pKJdNQGs1WsW09wyec-2GucwQz1UOU5sD76WJfJSzvD3WkWUHK16DOk1-DIq6eNns1tagN6cVrrAoHQwtMpXX9qV5xv1LzZiqfkcB2lp3fJ2RSOmfizie0932Jwkeb7xzZOc/s72-c/IMG_3183.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/05/meneja-wa-diamond-apelekwa-mahabusu.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/05/meneja-wa-diamond-apelekwa-mahabusu.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy