WAJENZI RELI YA TAZARA WAKUMBUKWA
HomeJamii

WAJENZI RELI YA TAZARA WAKUMBUKWA

Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO Raia wa nchi ya China wanaoishi Tanzania wamefanya kumbukumbu ya wataalam wa ujenzi wa reli inayounganish...

DK. KIGWANGALLA AWATAKA WALIOVAMIA KIWANJA CHA MAMLAKA YA HIFADHI YA NGORONGORO KILICHOPO NJIRO, JIJINI ARUSHA KUJIANDAA KISAIKOLOJIA
NECTA YATANGAZA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE
JESHI LA ZIMAMOTO NA UKOAJI HALIFANYI BAISHARA YA KUREKEBISHA VIZIMA MOTO 'FIRE EXTINGUISHER'

Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO
Raia wa nchi ya China wanaoishi Tanzania wamefanya kumbukumbu ya wataalam wa ujenzi wa reli inayounganisha nchi ya Tanzania na Zambia (TAZARA) waliofariki na kuzikwa nchini wakati wa ujenzi huo.
Kumbukumbu hiyo imefanyika leo Jijini Dar es Salaam katika eneo la Gongo la Mboto ambapo wataalaam hao walizikwa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga amesema kuwa ujenzi wa reli hiyo una umuhimu wa kipekee kwani ni sehemu ya ukombozi na itaendelea kudumu kwa manufaa ya uchumi wa nchi mbili zinazohusika.  
“Ujenzi wa reli hii ulipanda mbegu ya ushirikiano katika sekta zingine za maendeleo ambapo hadi sasa tunashuhudia miradi mingi ikiwemo ya viwanda vilivyowekezwa na Serikali ya China pamoja na kukua kwa biashara kati yetu,” alisema Balozi Mahiga.
Balozi Mahiga amempongeza Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kuona umuhimu wa kuwa na reli itakayounganisha nchi ya Tanzania na Zambia na kuamua kuomba msaada kwa Serikali ya China.
Kwa upande wake Balozi wa China nchini Tanzania, Bi Wang Ke amefafanua kuwa kumbukumbu hiyo imefanyika ikiwa ni siku ya maadhimisho ya utamaduni wa raia wa China iitwayo ‘Qingming’ yaani siku ya usafi wa makaburi ambapo raia wa China wameamua kuwaenzi wataalam wao waliozikwa nchini Tanzania.
“Zaidi ya wataalam 50,000 ambao ni raia wa nchi ya China walishiriki katika ujenzi wa reli ya TAZARA ambapo kati yao 65 walifariki, hivyo kumbukumbu hii inafanyika kwa ajili ya kuwaenzi wote waliojitolea nguvu na akili zao katika ujenzi huu,”alisema Balozi Wang Ke.
Reli hiyo yenye urefu wa kilomita 1860 ilijengwa kwa miaka sita tangu mwaka 1970 hadi 1976.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAJENZI RELI YA TAZARA WAKUMBUKWA
WAJENZI RELI YA TAZARA WAKUMBUKWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-96ikrx246tFGir_IJ0yvNA3cbMtif3GMCitL2e3AScoyrN1V57T_iVQuUu91uYu-Xo3F04dTBTu8iSRm7feeq2ivQjRHVvPD0qztbBqZWiqIgSu6VkCohz2jy8r30jkNFr7npm0uysc/s640/wachina%252Bpic.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-96ikrx246tFGir_IJ0yvNA3cbMtif3GMCitL2e3AScoyrN1V57T_iVQuUu91uYu-Xo3F04dTBTu8iSRm7feeq2ivQjRHVvPD0qztbBqZWiqIgSu6VkCohz2jy8r30jkNFr7npm0uysc/s72-c/wachina%252Bpic.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/04/wajenzi-reli-ya-tazara-wakumbukwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/04/wajenzi-reli-ya-tazara-wakumbukwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy