TANGA: INAVYOKUA KIVUTIO CHA UTALII NCHINI TANZANIA

Na Jumia Travel Tanzania Miongoni mwa mikoa maarufu nchini Tanzania ni pamoja na Tanga. Ukiachana na ukaribu wake na jiji la Dar e...




Na Jumia Travel Tanzania


Miongoni mwa mikoa maarufu nchini Tanzania ni pamoja na Tanga. Ukiachana na ukaribu wake na jiji la Dar es Salaam, mkoa wa Tanga una utajiri wa utamaduni wa Waswahili wanaopatikana katika pwani ya bahari ya Hindi, makumbusho ya kihistoria, shughuli za uchumi na kibiashara, pamoja na wanasiasa na wanasanaa mbalimbali mashuhuri wanaolipeperusha vema jina la mkoa huu.   

Hivi karibuni mkoa wa Tanga umekuwa ni eneo mojawapo la kitalii linalokua kwa kasi na kuwavutia watalii wengi ndani na nje ya Tanzania. Watalii wengi kupendelea kwenda Tanga kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa zikiwemo miongoni mwao tayari wamekwishatembelea sehemu zingine, kupata simulizi kutoka kwa watu wao wa karibu pamoja na vivutio vingine ambavyo havipatikani sehemu zingine isipokuwa Tanga.

Jumia Travel imekukusanyia baadhi ya sababu ambazo zimepelekea watu wengi kupendelea kwenda kutalii mkoa wa Tanga:  

Jiografia. Asilimia kubwa ya watalii hupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere uliopo katika jiji la Dar es Salaam. Umbali uliopo kati ya jiji hili na mkoa wa Tanga sio mkubwa, huchukua muda wa takribani masaa 6 kitu ambacho watalii wengi huweza kumudu. Hii imerahisisha shughuli za kitalii kwa urahisi kwa sababu watalii wanaweza kwenda na kurudi kwa urahisi. 

Vivutio vya kitalii. Mkoa wa Tanga umebarikiwa kuwa na vivutio mbalimbali ambavyo haviwezi kupatikana sehemu nyingine. Tanga inazo mbuga kama vile Saadani, Mkomazi, na Jozani ambazo unaweza kujionea wanyama, ndege na mimea ya aina mbalimbali lakini pia ina maeneo kama vile mapango ya Amboni na makumbusho ya kale ambayo yamebeba historia na urithi wa mkoa huo tangu enzi za wakoloni.   

Hali ya hewa. Miongoni mwa mji mashuhuri kwa shughuli za kitalii hivi sasa mkoani Tanga na Tanzania kwa ujumla ni Lushoto. Hali ya hewa nzuri, mandhari ya kuvutia na hoteli za kitalii katika eneo hili zimekuwa ni hamasa kubwa kwa wasafiri wengi. Eneo la Lushoto ambalo linapatikana kwenye safu ya milima ya Usambara limejizolea umaarufu kutokana na shughuli tofauti za kitalii kama vile matembezi na kupanda milima, shughuli za uvuvi, kuendesha baiskeli, kutembelea makumbusho ya kale, nakadhalika. Na kwa kuongezea eneo hili limewekezwa kwa hoteli za kisasa za kitalii.   


Hoteli za kitalii. Kutokana na kuwepo kwa shughuli nyingi za kitalii, kumekuwa na uwekezaji mkubwa katika huduma ya malazi. Miongoni mwa changamoto kubwa inayoikumba sekta ya utalii nchini na duniani kote ni huduma ya malazi. Malazi ni huduma ambayo huwa ghali ukilinganisha na huduma nyingine kama vile usafiri wa kwenda na kurudi, viingilio na makato mengineyo. 

Mkoa wa Tanga umejitahidi kwa hilo, wafanyabiashara wengi wamejenga hoteli ili kuweza kukidhi haja ya kila aina ya mtalii. Si jambo la kushangaza kukuta hoteli za kitalii karibu na vivutio vya kitalii.        

Gharama nafuu. Miundombinu kama vile barabara imewavutia watu wengi kwenda kwa urahisi kutalii vivutio vya mkoa wa Tanga kwani imerahisisha gharama za usafiri. Ukiachana na usafiri wa mabasi yanayokwenda na kurudi kila siku, watu wengi siku za hivi karibuni wamekuwa wakitumia usafiri wao binafsi. Unafuu pia upo kwenye huduma ya malazi ambayo kila mtu anaweza kumudu pamoja na gharama za kuishi kwenye jiji hilo kwa ujumla.  

Ukarimu wa watu wake. Watu wa Tanga wanasifika kuwa na haiba ya ukarimu kama walivyo watanzania wengi nchini. Hiki nacho kimekuwa ni kivutio kingine kwa watalii wengi kutembelea eneo hilo. Ukarimu huwavuta watalii wengi, kuwajengea hali ya usalama na kujifunza mengi kutoka kwa wenyeji wao. Wakazi wa Tanga wanatoa mchango mkubwa katika kulitangaza jiji lao kitalii kwa kuwapokea wageni na kuwafunza mambo yanayopatikana mkoani mwao.  

Kama ulikuwa unafikiria sehemu ya kwenda kutalii tofauti na sehemu ulizozizoea, Tanga itakuwa ni chaguo sahihi kwa hivi sasa. Ni miongoni mwa sehemu zinazofikika kwa urahisi na unaweza kufanya shughuli nyingi ndani ya muda mfupi na kurejea kwenye majukumu yako ya kawaida.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TANGA: INAVYOKUA KIVUTIO CHA UTALII NCHINI TANZANIA
TANGA: INAVYOKUA KIVUTIO CHA UTALII NCHINI TANZANIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiy8-DjRFQZFY9sda4qnn36BYGw8MnwlI4ywjLHVgUAwnNGbFZH5SPs07LMR2-gVZPVtYsCzJez1AvlEsQTWLuVezLyRr3TXLmxJTdZ4u8_ZQT9IW-utnxJkInLlNpF9IsFuQ7SsYvf9nRB/s640/001.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiy8-DjRFQZFY9sda4qnn36BYGw8MnwlI4ywjLHVgUAwnNGbFZH5SPs07LMR2-gVZPVtYsCzJez1AvlEsQTWLuVezLyRr3TXLmxJTdZ4u8_ZQT9IW-utnxJkInLlNpF9IsFuQ7SsYvf9nRB/s72-c/001.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/04/tanga-inavyokua-kivutio-cha-utalii.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/04/tanga-inavyokua-kivutio-cha-utalii.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy