MAKAMU WA RAIS AZINDUA CHANJO YA KUKINGA SARATANI YA KIZAZI JIJINI DAR ES SALAAM.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa ameshikilia chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) wakati wa uzinduzi wa chanjo hiyo kwenye viwanja vya Mbagala Zakhem, wengine pichani ni mabinti waliokuwa wa kwanza kupatiwa chanjo hiyo wakati wa uzinduzi, kushoto ni Neema Felix (14) mkazi wa Mbagala na mwingine ni Hadija Bakari (14) mkazi wa Kigamboni. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
HomeJamii

MAKAMU WA RAIS AZINDUA CHANJO YA KUKINGA SARATANI YA KIZAZI JIJINI DAR ES SALAAM.

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewaagiza Waganga Wakuu na W...

RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK SHEIN AFUNGUZI WA MKUTANO WA KUPIGA VITA UTAKASISHAJI WA FEDHA HARAMU NA UGAIDI ZANZIBAR.
POLEPOLE AFURAHISHWA NA MPANGO WA UCHANGIAJI WA HIARI PSS WA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF
MATUKIO MBALIMBALI BUNGENI LEO 8.9.2017







Na Mwandishi Wetu
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewaagiza Waganga Wakuu na Wilaya kuandaa kambi za wazi angalau mara tatu kwa mwaka ili kutoa fursa kwa wanawake wengi zaidi kupima saratani ya matiti nay a mlango wa kizazi.
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi mkoani Dar es Salaam ambapo hafla ya uzinduzi zilifanyika kwenye viwanja vya Zakhem Mbagala, wilaya ya Temeke.
Makamu wa Rais amesema Utoaji wa Chanjo dhidi ya Saratani ya mlango wa kizazi pamoja na uchunguzi wa awali kwa pamoja vitasaidia kuwakinga mabinti na kubaini mapema ugonjwa wa saratani kwa wanawake na hivyo kuepusha maumivu makali ama vifo vinavyoweza kuzailika
“ Tunatakiwa hadi Desemba, 2018 tuwe tumewafikia wanawake milioni tatu. Hii itawezekana endapo kila mmoja wetu ataweka kipaumbele katika kufikia lengo hilo.” Alisisitiza Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais amesema kuwa Serikali itatoa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi bila malipo yoyote katika vituo vinavyotoa huduma za chanjo vya Serikali, Mashirika ya Dini na Taasisi Binafsi.
Makamu wa Rais aliendelea kusema kuwa wasichana wote wenye umri wa miaka 14 ni walengwa wa kupata chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi  kwa mwaka huu 2018 ambapo jumla ya wasichana 6,16,734.
Makamu wa Rais ambaye aliwaeleza wananchi waliojitokeza kwenye hafla hiyo ya uzinduzi kuwa anaunga mkono uwepo wa chanjo hiyo huku akitoa sababu mbili moja ikiwa ni kulinda jeshi la wanawake nchini Tanzania kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha yao kwa sababu ya Saratani na sababu ya pili ni kwamba Mama yake Mzazi alifariki kwa kansa hiyo ya saratani ya mlango wa kizazi.

Wakati huo huo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia  Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa Tanzania imeandika historia nyingine katika sekta ya afya kwa kuzindua chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa Kizazi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) kwenye viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Aprili 10 2018. Kulia ni mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (wa pili kulia) na wageni maalum waliohudhuria wa tukio hilo 







Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua chanjo ya saratani ya kizazi (HPV Vaccine), jijini Dar es Salaamleo. Pamoja naye (kulia kwake) ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu na wageni maalum waliohudhuria wa tukio hilo. 

24: Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishuhudia Binti mwenye umri wa miaka 14 anayefahamiaka kwa jina Hadija Bakari mkazi wa Kigamboni akichomwa chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) wakati wa uzinduzi wa chanjo hiyo kwenye viwanja vya Mbagala Zakhem wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi mkazi wa Kigamboni na Neema Felix (14) mkazi wa Mbagala kijarida  alipozindua chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine), jijini Dar es Salaam leo. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu na wahudhuriaji wa tukio hilo.  

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi kipeperushi Hadija Bakari (14)  mmoja wa mabinti wa kwanza kupata chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine), jijini Dar es Salaam leo.  


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na mabinti wa kwanza kupata chanjo ya ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine), aliyesimama (kushoto) ni Hadija Bakari (14) mkazi wa Kigamboni na Neema Felix (14) mkazi wa Mbagala. 




Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAKAMU WA RAIS AZINDUA CHANJO YA KUKINGA SARATANI YA KIZAZI JIJINI DAR ES SALAAM.
MAKAMU WA RAIS AZINDUA CHANJO YA KUKINGA SARATANI YA KIZAZI JIJINI DAR ES SALAAM.
https://i.ytimg.com/vi/1b6sld5yftE/hqdefault.jpg
https://i.ytimg.com/vi/1b6sld5yftE/default.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/04/makamu-wa-rais-azindua-chanjo-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/04/makamu-wa-rais-azindua-chanjo-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy