UONGOZI WA MKOA RUKWA WACHANGIA MILIONI 5.7 KUMALIZIA UJENZI WA MSIKITI SUMBAWANGA

Uongozi wa Waislamu Mkoani Rukwa umepokea kwa furaha mchango wa Shilingi Milioni 5.7 uliotolewa na uongozi wa serikali ya Mkoa wa...




Uongozi wa Waislamu Mkoani Rukwa umepokea kwa furaha mchango wa Shilingi Milioni 5.7 uliotolewa na uongozi wa serikali ya Mkoa wa Rukwa ukiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo katika kikao cha maridhiano juu ya ujenzi wa msikiti uliosimama kwa muda.

Fedha hizo zilizochangwa zilijumuisha ahadi, fedha taslimu pamoja na vifaa vya ujenzi vilivyotolewa kwa umoja wa viongozi wa serikali kuonesha mshikamano uliopo kati ya serikali na wananchi bilaya kujali itikadi, dini wala rangi huku Mh. Wangabo akichangia milioni 1.5

Kabla ya maridhiano hayo Mh. Wangabo alitoa salamu za rais Dk. John Pombe Magufuli juu ya kuuendeleza msikiti huo na kunukuu kuwa Mheshimiwa Rais ametoa kibali cha kuuendeleza msikiti hio na yupo tayari kuweka jiwe la msingi ama kuuzindua msikiti huo.

“Mh. Rais ameniagiza niseme yafuatayo kuwa ametoa kibali cha kuendelea kujenga msikiti huu ahdi umalizike, ameyafikiria mambo mengi sana mpaka kuja kufikia maamuzi haya, ili yalete muskabali wa maridhiano, ilete amani, ilete utulivu, mshikamano, maoelewano na umoja ili Rukwa yetu iweze kusonga mbele kama kitu kimoja., la pili alisema kuwa yupo tayari kuweka jiwe la msingi ama la kuzindua msikiti huu,”

Kwa kuongezea hilo Mh. Wangabo aliuomba uongozi wa uislamu mkoa kuendelea kushirikiana na kudumiasha amani na kuhakikisha wanajenga Rukwa moja isiyoyumbishwa na tofauti yoyote kwani ushirikiano huo umekuwa wa muda mrefu hovyo asingependa pawepo na tofauti.

Pia alimuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga kuhakikisha vikwazo vyote vianondolewa na kumtaka kamishna wa ardhi nyanda za juu kusini kufanya haraka kupitisha kibali ili msikiti huo upatiwe hati.

Kwa upande wake Shekhe Mkuu wa mkoa wa Rukwa Rashid Akilimali amesifu maamuzi ya Rais Dk. John Pombe Magufuli na kukubali ombi lake la kutaka kuja kuweka jiwe la msingi ama kuuzindua msikiti huo na kuwa waislamu wataendelea kuungana nae na kumuombea amalize vipindi vyake salama.

“Mh. Mkuu wa Mkoa kwa niaba ya waislamu wa mkoa wa Rukwa kwanza tunatoa shukrani za dhati kwa Mh.Rais wa nchi Mh. Dk. John Magufuli, nimeamini kama alivyosema kuwa yeye ni msikivu na yeye anatuomba kila siku tumuombee dua na sisi mwisho wa khotuba yetu kila ijumaa tunadua huwa tunaiomba, Eee Mola wetu linda amani ya nchi yetu na uwalinde viongozi wetu,” Shekh Akilimali alimalizia.

Uongozi wa mkoa wa Rukwa uliowajumuisha kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa halmashauri, Mbunge wa jimbo la Sumbawanga mjini, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Sumbawanga pamoja na kaimu Kamishna wa Ardhi nyanda za juu kusini.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Wangabo akitoa salamu za Rais. Dk. John Pombe Magufuli juu ya waislamu kukubaliwa kuendelea na ujenzi wa Msikiti.
 Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Rashid Akilimali akiwasihi waislamu wanedelee kumuunga mkono Rais Dk. John Pombe Magufuli na kumshukuru kwa kuwaruhusu kuendelea na ujenzi wa msikiti. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Wangabo (kulia) akiepeana Mikono na  Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Rashid Akilimali baada ya maridhiano ya ujenzi wa Msikiti.


  Msikiti ulioruhusiwa kuendelea kujengwa.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: UONGOZI WA MKOA RUKWA WACHANGIA MILIONI 5.7 KUMALIZIA UJENZI WA MSIKITI SUMBAWANGA
UONGOZI WA MKOA RUKWA WACHANGIA MILIONI 5.7 KUMALIZIA UJENZI WA MSIKITI SUMBAWANGA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhMh2bUCNcZb5_As5NTUqnT6gmpHlQzQC-YPeZBdkgmR1S5AmzQy9sCheREu43MGV8nCKoXA2SWK-_raUx6c1FvK9GG4iMrmGZ9wb1g2BuoQDUPuTzmnb9JElDGDkAJ07A8WphbNAm2mcE/s640/P_20180305_100558_vHDR_On.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhMh2bUCNcZb5_As5NTUqnT6gmpHlQzQC-YPeZBdkgmR1S5AmzQy9sCheREu43MGV8nCKoXA2SWK-_raUx6c1FvK9GG4iMrmGZ9wb1g2BuoQDUPuTzmnb9JElDGDkAJ07A8WphbNAm2mcE/s72-c/P_20180305_100558_vHDR_On.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/03/uongozi-wa-mkoa-rukwa-wachangia-milioni.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/03/uongozi-wa-mkoa-rukwa-wachangia-milioni.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy