TANROADS YATAKIWA KUILINDA MIUNDOMBINU YAKE

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano(sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias John Kwandikwa (wa kwanza kushoto), pamoja na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakipata ufafanuzi wa namna mizani ya Itigi inavyodhibiti magari yanayozidisha uzito walipokagua barabara ya Manyoni-Itigi-Tabora KM 259.

HomeJamii

TANROADS YATAKIWA KUILINDA MIUNDOMBINU YAKE

Kamatiya Bunge ya Miundombinu imeutaka Wakalawa BarabaraNchini (TANROADS), kujipanga nakuja na mikakati bora ya kuilinda miundombinu ya ...

TANESCO KUSAFIRISHA UMEME KUPITA ARDHINI KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM
WANAHABARI WAPIGWA MSASA KUHUSU KINGATIBA YA MABUSHA, MATENDE, USUBI, KICHOCHO NA TRAKOMA
MUUGUZI HOSPITAL YA WILAYA YA MBEYA ATIWA MBARONI KWA MADAI AMESABABISHA KIFO CHA MTOTO MCHANGA


Kamatiya Bunge ya Miundombinu imeutaka Wakalawa BarabaraNchini (TANROADS), kujipanga nakuja na mikakati bora ya kuilinda miundombinu ya barabara za lami inazozijenga hapa nchini ili ziwe fursa za kiuchumi badala ya kuwa chanzo cha ajali.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi Sulemani Kakoso amesema  hayo mara baada ya kamati yake kutembelea ujenzi wa barabara ya Manyoni-Itigi-Tabora KM 259 inayojengwa kwa kiwango cha lami na kusisitiza kuwa umefika wakati kwa TANROADS kutoa elimu kwa jamii za vijijini kuzilinda barabara zinazojengwa na kuzitumia fursa za uwepo barabara za lami kujiletea maendeleo.
“Hakikisheni mnakuwa na programu endelevu za kuwaelimisha wananchi umuhimu wa barabara za lami ili badala ya kuzihujumu kwa kuharibu miundombinu ya barabara hizo wazilinde na kuzitumia kuibua fursa za kiuchumi na kijamii katika maeneo yao”, amesema Mhe. Kakoso.
Akizungumza katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anaeshughulikia sekta ya Ujenzi Mhe. Elias John Kwandikwa ameihakikishia Kamati hiyo kuwa Serikali imejipanga kuufungua mkoawa Tabora kwa kuhakikisha unafikika kwa pande zote kwa barabara za lami ili kuhuisha fursa za uzalishaji na kukuza uchumiwa wananchi wake.
“Tumeigawa barabara hii katika sehemu tatu ili kuharakisha ujenzi wake ambapo sehemu ya Manyoni- Itigi- Chaya KM 89.5 na Tabora–Nyahua KM 85, ujenzi wake kwa kiwango cha lami umekamilika na sehemu ya Chaya-Nyahua KM 85.4 mkandarasi anaendelea na ujenzi”, amesisitiza Naibu Waziri Kwandikwa.
Nae meneja wa TANROADS mkoa wa Singida Eng. Leonard Kapongo na Tabora Eng. Damian Ndabalinzi wameihakikishia Kamati ya Bunge ya Miundombinu kuwa watatekeleza utoaji elimu ya matumizi bora ya barabara na kudhibiti maeneo yenye ajali nyingi katika mikoa yao ili jamii katika mikoa hiyo zinufaike na uwepo wa barabara za  lami.
Kamati ya Bunge ya Miundombinu iko katika ziara ya kutembelea miundombinu inayosimamiwa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano katika mikoa ya Singida, Tabora na Kigoma ili kujifunza na kushauri namna bora ya kuendeleza miundombinu hapa nchini na hivyo kuwezesha malengo ya Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 kutekelezeka.
(Imetolewa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini)




Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sektayaujenzi) Mhe. Elias John Kwandikwa (wa nne kushoto), akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara( TANROADS), mkoa wa Tabora Eng. Damian Ndabalizi wa tano kushoto wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ilipokagua barabara ya Manyoni-Itigi-Tabora KM 259 inayojengwa kwa kiwango cha lami.



Meneja wa Wakala wa Barabara( TANROADS), mkoa wa Tabora Eng. Damian Ndabalizi wa tano kushoto akifafanua jambo kwa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu ilipokagua barabara ya Manyoni-Itigi-Tabora KM 259 inayojengwa kwa kiwango cha lami.



Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi) Mhe. Elias John Kwandikwa (wa tatu kushoto), akisisitiza jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ilipokagua barabara ya Manyoni-Itigi-Tabora KM 259 inayojengwa kwa kiwango cha lami.



Muonekano wa barabara ya Nyahua –Tabora KM 85 ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami umekamilika ambayo ni sehemu ya barabara kuu ya Manyoni-Itigi-Tabora KM 259

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TANROADS YATAKIWA KUILINDA MIUNDOMBINU YAKE
TANROADS YATAKIWA KUILINDA MIUNDOMBINU YAKE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEihQtOi_9G9i3GBRMonvVJcNnP1tDIpFxDneh6k6lLOoYbzjn4ST1RBBGR2Pn8kusStkgl_-eVQBrTr02caSbmwRQTsBzGEsxrMsiDwyDAw2kg9a4xyeDQIxoC22taLGfgpaTIKsd3EcsI/s640/1+%25282%2529.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEihQtOi_9G9i3GBRMonvVJcNnP1tDIpFxDneh6k6lLOoYbzjn4ST1RBBGR2Pn8kusStkgl_-eVQBrTr02caSbmwRQTsBzGEsxrMsiDwyDAw2kg9a4xyeDQIxoC22taLGfgpaTIKsd3EcsI/s72-c/1+%25282%2529.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/03/tanroads-yatakiwa-kuilinda-miundombinu.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/03/tanroads-yatakiwa-kuilinda-miundombinu.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy