TAARIFA YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KWA VYOMBO VYA HABARI
HomeJamii

TAARIFA YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KWA VYOMBO VYA HABARI

                            JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA    WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI ...

BOTI YA MV MKONGO YASAFIRISHWA KUELEKEA UTETE PWANI
RC MAKONDA AKABIDHIWA MWENGE WA UHURU UKITOKEA MKOANI LINDI
RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM


             
             JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
   WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI


Simu ya maandishi: “ZIMAMOTO KUU”
Simu Nambari:  +255-22-2181093
Telefax:          + 255-22-2184569
Tovuti : www.frr.go.tz

 


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kufuatia  uwepo na muendelezo wa matukio ya moto katika maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo  shule za bweni, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linatoa tahadhari kwa Wanafunzi, Wakuu  wa Shule, Wamiliki na Wananchi kwa ujumla kuchukua tahadhari kwa kuwa makini katika matumizi ya vifaa vya umeme.
Msemaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkaguzi (INSP) Joseph Mwasabeja amesema, kutokana na matukio haya ya moto kutokea mara kwa mara katika Jamii yetu hususani katika Shule za Bweni hasa Shule za Sekondari na kusababisha uharibifu wa miundombinu kama vile mali, majengo na wakati mwingine majeraha au vifo kwa wanafunzi wetu. Mara nyingi matokeo ya majanga haya huleta hasara na sintofahamu kwa Wananchi na Taifa kwa ujumla.
Amesema, uchunguzi wa moto ( Fire Investigation) umebaini sababu za matukio hayo ni matumizi mabaya ya umeme yanayofanywa na wanafunzi kwa kujiunganishia nyaya za umeme wenyewe bila ya kuwa na weledi ili wapate sehemu za kuchaji simu na heater za kuchemshia maji kwa kificho kwasababu wanafunzi hawaruhusiwi kuwa na simu wala heater pindi wanapokuwa Shuleni.
Aidha, majanga ya moto yamekuwa yakitokea katika jamii yetu, kwasababu moto ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Pia ni wazi kuwa na vyanzo vingi vya moto ni sisi wenyewe (binadamu) kutokana na uzembe au hujuma.
Ili kupunguza matukio haya Jeshi letu limeanzisha ( Fire Klabu) kwa Shule za Msingi na Sekondari, hatua itakayosaidia kuwapa  Elimu Stahiki ya kukabiliana na majanga ya moto na hatimaye kuwa na mabalozi wa Zimamoto na Uokoaji katika Shule na makazi yao.
Wito wangu kwa wamiliki wa Shule walipokee jambo hili kama ukombozi kwao ili kupunguza majanga na madhara ya moto pindi unapotokea katika Shule zao. Pia amewataka Wamiliki wa Shule kuzingatia maelekezo na ushauri unatolewa na Jeshi letu juu ya Kinga na Tahadhari dhidi ya majanga ya Moto.


“Vilevile niwaombe wananchi wote kuwa wepesi katika kutoa taarifa pindi wanapopata majanga ya moto na majanga mengine kwa kupiga namba 114 ili Askari wetu waweze kufika kwa wakati na kuokoa Maisha na Mali. Alisema huku akiwashauri wananchi kuwa na Vifaa vya kuzimia moto (Fire Extinguisher). ’’
Imetolewa na;


Joseph Mwasabeja – Mkaguzi Msaidizi (INSP)
Msemaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Makao Makuu

20 Marchi, 2018

Joseph Mwasabeja – Mkaguzi Msaidizi (INSP)
Msemaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Makao Makuu


Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TAARIFA YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KWA VYOMBO VYA HABARI
TAARIFA YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KWA VYOMBO VYA HABARI
https://docs.google.com/drawings/u/0/d/ssMWIq6AA4a7NhShhK10KSQ/image?w=263&h=88&rev=1&ac=1
https://lh3.googleusercontent.com/8vZUF5fRgoq-ijp9WUWjVQ99HuLZXT9bf4sIvD98kCdfiqN60r81SbB6K2ufcOaSsnd16Ag7jJmK1cRGpfC08iROEm6vKDQcPIxTfKFlVPxVlF7Bo-5aW7SbcU6wHvyZvDmLdsqup3rQDTh8wA=s72-c
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/03/taarifa-ya-jeshi-la-zimamoto-na-uokoaji.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/03/taarifa-ya-jeshi-la-zimamoto-na-uokoaji.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy