TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Meneja wa Kiwanja cha Ndege Mwanza, Bi. Easter Madale (kushoto), alipokagua maendeleo ya upanuzi wa kiwanja hicho mkoani Mwanza leo.

HomeJamii

TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ametoa wiki mbili kwa Mamlaka ya Viwanja Ndege Nchini (TAA), kukusanya ...

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YAKUTANA NA WATAALAM WA MFUMO WA TAARIFA ZA KIJIOGRAFIA (GIS) UTAKAOTUMIKA KUPUNGUZA GHARAMA ZA UKUSANYAJI TAKWIMU
TANZANIA NA KOMORO ZAAHIDI KUENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO
MUHAS WATAKIWA KUWEKA MAKAZI YA KUDUMU OLOLOSOKWAN


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ametoa wiki mbili kwa Mamlaka ya Viwanja Ndege Nchini (TAA), kukusanya fedha za madeni ambayo inadai kutoka kwa watoa huduma mbalimbali katika viwanja vyote vya ndege ili ziweze kutumika kuendeleza miundombinu.

Kauli hiyo ametoa jijini Mwanza, baada kukagua maendeleo ya upanuzi wa kiwanja cha ndege na hali ya uendeshaji katika kiwanja hicho ambapo amebaini kuwa kuna madeni ambayo yanaweza kulipika na kuweza kurahisisha shughuli za kiuendeshaji ikiwemo kujenga uzio ili kuongeza usalama kiwanjani hapo.

"Nataka TAA mkusanye madeni yote mnayodai, fedha hizi zikipatikana zinaweza kutumika kujenga uzio kwa ajili ya kulinda usalama wa uwanja ili wananchi wasiweze kuvamia na pia usalama wa ndege zinazoruka na kutua", amesisitiza Prof. Mbarawa.

Amefafanua kuwa kama Taasisi hizi zikikusanya madeni na watoa huduma wakalipa kodi kwa wakati kutasaida Serikali kuboresha maendeleo ya miundombinu.

Kuhusu maendeleo ya upanuzi wa kiwanja hicho. Prof. Mbarawa amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi ambapo kwa sasa umefikia asilimia 60.

Ameongeza kuwa ujenzi huo unategemewa kumalizika mwezi Julai mwaka huu na utagharimu kiasi cha shilingi takribani bilioni 94.

Aidha amesema Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la abiria mara miradi inayoendelea kukamilika.

Naye Msimamizi wa Kiwanja hicho ambaye ni Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Mwanza, Mhandisi Joseph Mwami,  amesema kazi zinazoendelea kwa sasa ni pamoja na ujenzi wa jengo la kuongoza ndege, eneo la maegesho na njia za kuruka na kutua ndege

Mhandisi Mwami, amefafanua kuwa njia ya kuruka na kutua ndege katika kiwanja hicho imeongezwa urefu wa mita 500 ili kuifanya kufikia urefu wa KM 3.5 ili kuwezesha ndege kubwa za kimataifa kuweza kutua na kuruka katika kiwanja hicho.

Katika hatua nyingine Waziri Prof Mbarawa amekagua na kuridhishwa na ujenzi wa barabara ya Mwaloni-Pasiansi-Airport yenye urefu wa KM 5.3 kwa kiwango cha lami ambapo ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika mwezi mei mwaka huu na utagharimu kiasi cha shillingi bilioni 9.5.

"Nimekagua na niwapongeze Kampuni ya wazawa ya Nyanza Road kwa kazi nzuri mliyofanya katika ujenzi kwa barabara hii", amesema Prof Mbarawa.
Waziri Prof. Mbarawa ametoa wito kwa wananchi kutunza na kulinda miundombinu hiyo kwa manufaa ya kuongeza tija na maendeleo kwao kwan inapunguza msongamano wa magari kwa kiasi kikubwa na Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kugharamia utekelezaji wa miradi hiyo.
Waziri Prof Mbarawa yuko mkoani mwanza kwa ziara ya siku akiwa na lengo la kukagua utekelezaji wa miundombinu ya sekta ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano




Meneja wa Kiwanja cha Ndege Mwanza, Bi. Easter Madale (wa pili kulia), akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia), eneo ambalo litajengwa uzio wa kiwanja hicho, mara baada ya kukagua maendeleo ya upanuzi wa kiwanja hicho mkoani Mwanza leo.



Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari, kuhusu mipango ya Serikali ya kuendeleza kiwanja cha Ndege Mwanza kwa kuiboresha miundombinu ili kiwanja hicho kiwe cha Kimataifa, wakati alipokagua maendeleo ya upanuzi wa kiwanja hicho.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia), akikagua maendeleo ya ujenzi barabara ya Pasiansi hadi Airport KM 4.6 inayojengwa kwa kiwango cha lami, mkoani Mwanza.



Muonekano wa sehemu ya barababara ya Pasiansi hadi Airport KM 4.6, inayojengwa kwa kiwango cha lami, mkoani Mwanza.




Muonekano wa eneo la kuegesha ndege ambalo ni moja ya utekelezaji wa mradi wa upanuzi na uboreshaji wa kiwanja cha ndege cha Mwanza.




Muonekano wa jengo la kuongozea ndege katika kiwanja cha ndege cha Mwanza, ambapo ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 80, na linajengwa na kampuni ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG).

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano)


Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE
TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEglP8hoyA1L9DD9BoAa8wFuo43zacEbEyR52nmhGWg0SSjbsViuKQ8-hj6Dl2VTpNtS1paIBxD4K6BWpRPoS1Dz3oIVn52sGL5QpA9C7DalvP8qlcf61i6zF_ySYUvTA00o0ySMizPTpiY/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEglP8hoyA1L9DD9BoAa8wFuo43zacEbEyR52nmhGWg0SSjbsViuKQ8-hj6Dl2VTpNtS1paIBxD4K6BWpRPoS1Dz3oIVn52sGL5QpA9C7DalvP8qlcf61i6zF_ySYUvTA00o0ySMizPTpiY/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/02/taa-yapewa-wiki-2-kukusanya-madeni-yote.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/02/taa-yapewa-wiki-2-kukusanya-madeni-yote.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy