MHE. MGALU AONYA MATAPELI MIRADI YA REA
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akielezea mikakati ya serikali katika kupeleka umeme katika maeneo yaliyopo pembezoni mwa miji kwa wananchi wa kata ya Bomba Mbili iliyopo katika wilaya ya Ilala nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
HomeJamii

MHE. MGALU AONYA MATAPELI MIRADI YA REA

Na Greyson Mwase, Dar es Salaam Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu ametoa onyo kwa matapeli wanaojitokeza kwa kujifanya maafisa wa W...

RAIS DKT MAGUFULI ASITISHA UBOMOAJI WA NYUMBA 17,000 TUANGOMA JIJINI DAR
CHAMA CHA MAENDELEO YA MAKETE (MDA) WAPATA VIONGOZI WA KUDUMU
MSHINDI WA SHILINGI MILIONI 30 YA DROO YA JUMAPILI YA JACKPOT YA TATU MZUKA AKABIDHIWA FEDHA ZAKE


Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu ametoa onyo kwa matapeli wanaojitokeza kwa kujifanya maafisa wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kuwatoza wananchi fedha kama malipo ya kuunganishiwa huduma ya umeme.
Mgalu aliyasema hayo mwishoni mwa wiki  katika  mikutano aliyoifanya wakati wa ziara  yake katika  katika kata za Bomba Mbili, Mbondole,  Kiboga, Zogoali,  Kigezi Buyuni na Chanika zilizopo katika wilaya ya  Ilala nje kidogo ya Jiji la  Dar es Salaam.
Lengo la ziara yake lilikuwa ni kutembelea maeneo  ambayo hayajafikiwa  na miundombinu ya umeme, kuzungumza na wananchi na kuweka mikakati ya  namna ya kumaliza changamoto hizo kwa kushirikiana na REA na  Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)
Awali, wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa kata husika walilalamika kuwepo kwa  tabia ya baadhi ya watu ambao wamekuwa wakijitambulisha kwao kama maafisa kutoka REA na  TANESCO na kuwachangisha  fedha nyingi  ili wawaunganishie huduma ya umeme kinyume na taratibu.
Walisema kuwa baada ya kufanya malipo kwa watu hao walishangaa kuona wametoweka na fedha hizo pasipo kuwapatia huduma ya aina yoyote.
Akifafanua kero hiyo, Mgalu alitoa wito kwa wananchi kutoa  taarifa katika vyombo vya usalama pindi watu wasiofahamika wanapojitokeza na kudai michango kwa ajili ya kuwaunganishia huduma ya umeme.
Aliongeza kuwa wakandarasi kabla ya kuanza kazi ya kuweka miundombinu ya umeme katika kata husika, wanatakiwa kujitambulisha kwa viongozi wa mtaa ili waweze kutambulishwa kwa wananchi.
Alisema kuwa katika kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma ya umeme Serikali imetoa punguzo kubwa ambapo kila mwananchi aliyepo ndani ya miradi ya REA atatakiwa kuchangia  gharama ya shilingi 27,000 tu.
Vilevile aliwataka wananchi kujiandaa kwa kuunganishiwa na huduma ya umeme kupitia REA kwa kutandaza nyaya za umeme kwenye nyumba zao kupitia wakandarasi wanaotambulika na TANESCO.
Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara akifafanua jambo kwenye mkutano wa Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu na wananchi wa kata ya Bomba Mbili iliyopo katika wilaya ya Ilala nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam mapema tarehe 24 Februari, 2017 


Sehemu ya wakazi wa kata Zogoali katika wilaya ya Ilala wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu.


Mmoja wa wakazi wa kata ya Bomba Mbili iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam, Dkt. Isaya Madama akitoa kero yake mbele ya Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kushoto) akinukuu maswali mbalimbali yaliyokuwa yanauliuzwa na wakazi wa kata ya Bomba Mbili iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akisalimiana na sehemu ya wakazi wa kata ya Zogoali iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam, mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara katika kata hiyo.











Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MHE. MGALU AONYA MATAPELI MIRADI YA REA
MHE. MGALU AONYA MATAPELI MIRADI YA REA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgeWhW1x1WKWmPipZ0Rt02FOn-XRrvmo5NoD0OOx7MFd-9kNgm6Uvoy9bSgmj8IFjHQB0pKiELRpFW-Iq0yMDuVbD9DJGd3gKtsRHTyDikk3TYTiFDNnrUGN9yrTggpzm2liJ9u0HFHpY8/s640/Picha+Na+2.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgeWhW1x1WKWmPipZ0Rt02FOn-XRrvmo5NoD0OOx7MFd-9kNgm6Uvoy9bSgmj8IFjHQB0pKiELRpFW-Iq0yMDuVbD9DJGd3gKtsRHTyDikk3TYTiFDNnrUGN9yrTggpzm2liJ9u0HFHpY8/s72-c/Picha+Na+2.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/02/mhe-mgalu-aonya-matapeli-miradi-ya-rea.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/02/mhe-mgalu-aonya-matapeli-miradi-ya-rea.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy