RC MAKONDA AENDELEZA FARAJA KWA WAANDISHI WA HABARI.
HomeJamii

RC MAKONDA AENDELEZA FARAJA KWA WAANDISHI WA HABARI.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda , Leo amehaidi Kuijenga Nyumba ya Vyumba Vinnie (4) Familia ya Mwandishi (mpiga picha) wa M...

RC MAKONDA ATAJA MAMBO MAKUU MANNE KUKABILIANA NA UHALIFU JIJINI DAR ES SALAAM
MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA TAARIFA YA THBUB KWA VYOMBO VYA HABARI
WADAU WA JOTOARDHI WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM LEO


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda , Leo amehaidi Kuijenga Nyumba ya Vyumba Vinnie (4) Familia ya Mwandishi (mpiga picha) wa Magazeti ya Serikali TSN wanaochapisha Magazeti ya Habari Leo na Daily News,  na SpotLeo, Marehemu Athumani Hamis ambae amezikwa katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam.


Ahadi hiyo Imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TSN Dkt. Yonaz kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda ambae aliombwa kuisadia familia ya Marehemu ambayo ina watoto Wanne wanaosoma huku wakiwa wanaishia kwenye Nyumba ya kupanga kutokana na Baba yao kuugua kwa zaidi ya Miaka 10 na hivyo kushindwa kufanya kazi.


Dkt. Yonaz amesema Mhe Makonda kwa kutambua mchango wa tasnia ya Habari hususani waandishi wa Habari amekubali kujenga Nyumba hiyo kama kielelezo cha Kumuenzi Marehemu Athumani ambae katika uhai wake alikuwa Mpigapicha mahiri wa Magazeti ya Serikali nchini.


Hatua hii imepokelewa kwa furaha na baadhi ya waandishi wa habari ambao wamesema kitendo cha Makonda kukubali kuijengea nyumba familia ya marehemu Athumani mbali na kuwafuta machozi ya huzuni, bali kimekuwa ni fundisho tosha kwa baadhi ya waandishi ambao walikuwa wakimchukia Mhe Paul Makonda pasipo sababu za msingi, na kukifananisha kitendo hiki na ukamilifu wa maandiko katika vitabu vitakatifu yanayotutaka 'Twapende Adui zetu'


Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Paul Makonda (katikati) akizungumza na Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali TSN Ltd Dkt. Jimmy Yonaz kulia na kaka wa Marehemu Athuman Hamis Dkt. Ibrahim Msengi nyumbani kwa marehemu Sinza Kijiweni jijini Dar es salaam.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RC MAKONDA AENDELEZA FARAJA KWA WAANDISHI WA HABARI.
RC MAKONDA AENDELEZA FARAJA KWA WAANDISHI WA HABARI.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj9277CBQh_ZGJgB2Ynlcytf6AaQ29tIVhrOiMr3kUf2KHLS55PxiPw2_qidyCHLfeo9q5u2VzjgRb-7rNdO9TgYV6ZgfpiI-xupej7UKCaJAVyXjm19zezGvGLOgq9rZ6f9PpG9kUpKuEg/s640/IMG_20180105_124859-768x576.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj9277CBQh_ZGJgB2Ynlcytf6AaQ29tIVhrOiMr3kUf2KHLS55PxiPw2_qidyCHLfeo9q5u2VzjgRb-7rNdO9TgYV6ZgfpiI-xupej7UKCaJAVyXjm19zezGvGLOgq9rZ6f9PpG9kUpKuEg/s72-c/IMG_20180105_124859-768x576.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/01/rc-makonda-aendeleza-faraja-kwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/rc-makonda-aendeleza-faraja-kwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy