Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akiangalia bidhaa ya mafuta ya kupikia w...
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akiangalia bidhaa ya mafuta ya kupikia wakati alipotembelea Kikundi cha wanawake wajasiriamali cha Ndimila kilichopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga alipofanya ziara ya siku mbili ya kuamsha ari ya wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akitia saini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alipofanya ziara ya siku mbili ya kuamsha ari ya wananchi kufanya shughuli za maendeleo ili kuchangia azma ya kufikia uchumi wa kati na wa viwanda.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Bonifasi Kasululu akiwasilisha Taarifa ya Mkoa kwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara yake alipofanya ziara ya siku mbili ya kuamsha ari ya wananchi kushiriki kazi za maendeleo ili kuchangia azma ya kufikia uchumi wa kati na wa viwanda.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akiangalia bidhaa ya majani ya kutengeneza chai maarufu kwa jina la Mchaichai wakati alipotembelea Kikundi cha wanawake wajasiriamali cha Victory kilichopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga alipofanya ziara ya siku mbili ya kuamsha ari ya wananchi kufanya shughuli za maendeleo.
Mwakilishi wa Ofisi ya Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Bw. Yolla Ludege akitoa maelezo kuhusu taratibu za kuwakagua na kuwapa vibali wanawake wajasiliamali kutengenza bidhaa zao wakati wa ziara ya siku mbili ya Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) iliyolenga kuamsha ari ya wananchi kufanya shughuli za maendeleo.
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda vidogo (SIDO) mkoa wa Rukwa Bw. Emmanuel Makere akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa wananwake wajasiliamali wa Mkoa wa Rukwa kuhusu majukumu ya Shirika katika kuwawezesha wanawake kiuchumi.
Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Rukwa Bi. Ndionusia Njuyuwi akisoma taarifa kuhusu utekelezaji wa uanzishwaji na uwezeshaji wa vikundi vya wanawake kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake(WDF).
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akizungumza na wanawake wajasiliamali walioshiriki kikao cha siku moja Mkoa wa Rukwa wakati wa ziara yake iliyolenga kuamsha ari ya wananchi kufanya shughuli za maendeleo.
Baadhi ya wanawake wajasiliamali wa Mkoa wa Rukwa wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) wakati wa ziara yake kuamsha ari ya wananchi kufanya shughuli za maendeleo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akitoa motisha kwa Vikundi ‘walelewa’ na kuwaunganisha kwa ‘Vikundi Mlezi’ ili waweze kusaidia katika kuboresha biashara zao wakati wa ziara yake ya siku mbili Mkoani Katavi kuamsha ari ya wananchi kufanya kazi na kuboresha huduma ya afya kwa wananchi.
(PICHA NA WAMJW)
COMMENTS