MAKUSANYO YA KODI YA PANGO LA ARDHI YAONGEZEKA MARADUFU
HomeJamii

MAKUSANYO YA KODI YA PANGO LA ARDHI YAONGEZEKA MARADUFU

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu Kayandabila akiongea na watumishi wa wizara hiyo katika m...

RAIS ASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI MJINI ZANZIBAR LEO
RAIS DKT MAGUFULI APATA CHAKULA CHA MCHANA NA VIJANA WALIOKIMBIZA MWENGE MWAKA HUU IKULU ZANZIBAR
UHURU FM WALIPOLIAMSHA DUDE VIWANJA VYA MWEMBEYANGA, TEMEKE, KATIKA TAMASHA LA 'GUSA MAISHA YAKE' KUMUENZI BABA WA TAIFA HAYATI MWALIMU NYERERE


Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu Kayandabila akiongea na watumishi wa wizara hiyo katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi na kuwataka waongeze jitihada za makusanyo ya kodi ya pango la ardhi.

Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Yamungu Kayandabila wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi.


Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Yamungu Kayandabila wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi.


Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Yamungu Kayandabila wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu Kayandabila katikati, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Dkt. Moses Kusiruka kushoto na Mjumbe Baraza kuu la Wafanyakazi Serikalini (TUGHE) kulia, wakiimba wimbo wa mshikamano kwa wafanyakazi.


Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu Kayandabila katikati, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Dkt. Moses Kusiruka kushoto na Mjumbe Baraza kuu la Wafanyakazi Serikalini (TUGHE) kulia, wakiimba wimbo wa mshikamano kwa wafanyakazi.


Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakiimba wimbo wa mshikamano kwa wafanyakazi wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi.

Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakiimba wimbo wa mshikamano kwa wafanyakazi wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi.

………………………………………………………

Na Hassan Mabuye, Kitengo cha Mawasiliano, Wizara ya Ardhi.

Serikali imefanikiwa kukusanya jumla ya kiasi cha shilingi bilioni 76 cha makusanyo ya kodi ya pango la ardhi hadi kufikia tarehe 13 Mei 2017 kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa.

Akiongea katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Yamungu Kayandabila amesema kiwango cha makusanyo ya kodi ya ardhi hakijawahi kufukiwa ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo kwa sasa Wizara ya Ardhi imeisha kusanya kiasi cha shilingi bilioni 76 cha kodi ya pango la ardhi.

Juhudi za kukusanya kodi ya pango la ardhi kwa viwanja vilivyopimwa zinaendelea vizuri licha ya changamoto iliyopo hususan muamko wa wananchi katika kulipa kodi, amesema Dkt. Kayandabila.

“Ni matumaini yangu kuwa katika kipindi kilichobaki Wizara itafikia lengo la kukusanya kiasi cha makusanyo ya kodi ya pango la ardhi kilichowekwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ambacho ni kiasi cha shilingi bilioni 111.7”. Amesema Dkt. Kayandabila.

Amesema, Serikali kuanzia mwezi julai, 2017 kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi itaanza kukusanya kodi ya pango la ardhi kwenye viwanja na mashamba yasiyopimwa. Lengo la utaratibu huu ni kuongeza wigo wa mapato yatokanayo na kodi ya pango la ardhi.

Utaratibu huu utawafanya wananchi wote wanaomiliki ardhi waweze kulipa kodi. Hata hivyo, ni vema ieleweke kuwa uamuzi huu hauna lengo ya kupunguza juhudi za Wizara katika kupanga, kupima na kumilikisha ardhi kwa wananchi, isipokuwa utaratibu huu unajenga dhana ya uwajibikaji kwa wananchi wote katika kulipa pango la ardhi kwenye maeneo yao.

Aidha, serikali imeanza Ujenzi wa mfumo wa kielektronic wa kumbukumbu za Ardhi (Integrated Land Management System) ambao umeanza kutekelezwa. Mfumo huo ukikamilika utasaidia sana kuwa na kumbukumbu sahihi za wamiliki wa ardhi na hivyo kurahisisha ukusanyaji wa kodi za Ardhi.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAKUSANYO YA KODI YA PANGO LA ARDHI YAONGEZEKA MARADUFU
MAKUSANYO YA KODI YA PANGO LA ARDHI YAONGEZEKA MARADUFU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgr35K-slsUNIM5VCYJy2cfIhyphenhyphenf6s8bxENc1dQxq8HGPt-mgksaUGsKlvdk2pV7BPaYzvQ62wpIjnzwNX7QaIKt8F_5Nqj-rpgiOlWU7j7UD_CT9Jqz8tjZ_A_vy981OI0DNh-8f3-Qf5I/s640/TIB1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgr35K-slsUNIM5VCYJy2cfIhyphenhyphenf6s8bxENc1dQxq8HGPt-mgksaUGsKlvdk2pV7BPaYzvQ62wpIjnzwNX7QaIKt8F_5Nqj-rpgiOlWU7j7UD_CT9Jqz8tjZ_A_vy981OI0DNh-8f3-Qf5I/s72-c/TIB1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/05/makusanyo-ya-kodi-ya-pango-la-ardhi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/makusanyo-ya-kodi-ya-pango-la-ardhi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy