ALIYEJIHITA  NABII "MTATA" MIKONONI MWA POLISI HUKO DODOMA
  
Mchungaji Tito (pichanijuu), ambaye kwa takriban wiki nzima ameibua mjadala mkubwa mionhgoni mwa Watanzania, kufuatia video inayomuonyesha akiwa na wanawake wawili mmoja akimtambulisha kuwa mkewe na mwingine msichana wa kazi (house girl) huku akiwapiga busu amekamatwa leo Januari 23, 2018 mkoani Dodoma.
Awali Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Sheria wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Marlin Komba amesema hamtambui mtu anayejiita nabii Tito na kwamba hajasajili kanisa lake katika ofisi ya msajili wa taasisi za dini, na kwamba Serikali imeona vitendo anavyovifanya ‘nabii’ huyo kupitia mitandao ya kijamii na imeanza kuchukua hatua.“Ninachoweza kusema ni kwamba hakuna mtu anayezuiwa kuongea hapa nchini, mwache aongee anavyoweza ila Serikali imeshaona anachokifanya na yanayoendelea mitandaoni hatua zinachukuliwa dhidi yake,” amesema Komba.Kauli hii imekuja kufuatia kusambaa kwa video mbalimbali zikimuonyesha ‘nabii’ huyo akitoa mafundisho yake huku akinywa vilevi pamoja na kufanya matendo ambayo ni kinyume cha maadili ya dini, jambo ambalo limeonekana kuwakera wadau wengi wa dini.Kwa upande wao viongozi mbalimbali wa dini wameonyeshwa kukerwa na kulaani vitendo anavyovifanya mtu huyo anayejiita ‘nabii’ na kusisitiza kuwa hakuna dini inayoruhusu hayo.Askofu Msaidizi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Mchungaji Chediel Lwiza amesema kuwa, kutokana na vitendo anavyofanya, mtu huyo hapaswi kujiita mtumishi wa Mungu.“Huyo hawezi kuwa mtumishi wa Mungu na wala hafanyi huduma ya kanisa. Ni vyema watu kama hawa wafuatiliwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao. Natumaini Wizara ya Mambo ya Ndani ambayo ndani yake ina ofisi ya msajili wa taasisi za dini itafanya kazi yake,” amesema Mchungaji Lwiza.Naye Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Rajab Katimba amesisitiza Serikali na viongozi wa dini kuingilia kati suala hilo na kueleza kuwa, hakuna kitabu chochote cha dini kinachohamasisha ulevi na ukosefu wa maadili.“Hilo suala linakwenda tofauti na dini na mila na desturi zetu pia. Dini zinatakiwa kuleta amani na kuhamasisha watu waheshimiane si kuzungumza mambo yanayokiuka maadili yetu. Naona ipo haja ya viongozi wa dini na Serikali kuingilia suala hili na waende mbali zaidi kwa kuongea naye huenda hafahamu anachokifanya,” amesema Rajab Katimba.
HomeJamii

ALIYEJIHITA NABII "MTATA" MIKONONI MWA POLISI HUKO DODOMA

   Mchungaji Tito  (pichanijuu), ambaye kwa takriban wiki nzima ameibua mjadala mkubwa mionhgoni mwa Watanzania, kufuatia vi...

MAHAFALI YA 32 YA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).
RAIS MAGUFULI AELEKEA ADDIS-ABABA ETHIOPIA KUHUDHURIA MKUTANO WA 28 WA WAKUU WA NCHI ZA UMOJA WA AFRIKA AU
WALIOTAFUNA ZAIDI YA SH. BILIONI 1 ZA USHIRIKA WASHUGHULIKIWE-WAZIRI MKUU MAJALIWA

Mchumgaji anayedaiwa kufanya udhalilishaji katika mahubiri yake anaswa na Polisi mkoani Dodoma, Hapa Mkuu wa Jeshi la. Polisi nchini IGP Saimon Sirro akimsikiliza

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: ALIYEJIHITA NABII "MTATA" MIKONONI MWA POLISI HUKO DODOMA
ALIYEJIHITA NABII "MTATA" MIKONONI MWA POLISI HUKO DODOMA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_46515zn9m_pvaYQm7OGv7c8bgvkp_wxBYQZSmyoAhbVd5IuQFlNmWZdiW-k8ypGbTC-Q47j20MmneijXf9FjMY6TPnsfg_6Rb8zTZZpz-2lkNMNwINUJCkVvnF6Ou8PboS5an2G-mIg9/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_46515zn9m_pvaYQm7OGv7c8bgvkp_wxBYQZSmyoAhbVd5IuQFlNmWZdiW-k8ypGbTC-Q47j20MmneijXf9FjMY6TPnsfg_6Rb8zTZZpz-2lkNMNwINUJCkVvnF6Ou8PboS5an2G-mIg9/s72-c/1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/01/aliyejihita-nabii-mtata-mikononi-mwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/aliyejihita-nabii-mtata-mikononi-mwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy