Askari wa wanyama pori wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Ndg. Majid Kijaji (kushoto) akimfafanulia Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa n...
Askari wa wanyama pori wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Ndg. Majid Kijaji (kushoto) akimfafanulia Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (wa kwanza kulia) kuhusu fuvu la Fisi alipotembelea hifadhi hiyo iliyoko mkoani Arusha leo tarehe 29/12/2017 kama juhudi za kuhamasisha utalii wa ndani nchini.

Kaimu Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Bi. Mery Kirombo (wa kwanza kulia) akimpatia maelezo mafupi kuhusu hifadhi hiyo Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) muda mfupi kabla ya kuanza kwa safari ya kuhamsisha utalii katika hidadhi hiyo leo tarehe 29/12/2017 mkoani Arusha. Katikati ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Ndg. Godifrey Mngereza. Safari hiyo iliandaliawa na Taasisi ya Mtandao wa Wasanii wa Musiki wa Njili hapa Nchini (TAGOANE)

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (wa pili kulia waliokaa nyuma) akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Tengeru English Medium katika eneo la Ngurudoto Crater alipotembelea hifadhi ya Taifa ya Arusha (Arusha National Park) iliyoko mkoani Arusha leo tarehe 29/12/2017. Kushoto kwake ni msanii wa maigizo Kingwnedu na kulia kwake ni Rais wa TAGOANE Dkt. Godwin Maimu , taasisi ya TAGOANE ndiyo iliyo ratibu safari hiyo ya siku moja ya kuhamasisha utalii wa ndani nchini.

Afisa Utalii na Masoko wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Ndg. Nicholaus Mahimbi (kulia) akimfafanulia Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) kuhusu mabaki ya fuvu la Nyati lililopo katika eneo la Ziwa Dogo la Momella wakati Mhe. Shonza alipotembela hifadhi hiyo iliyoko mkoani Arusha leo tarehe 29/12/2017 kama juhudi za kuhamasisha utalii wa ndani nchini.

Askari wa wanyama pori wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Ndg. Agustino Kombwa (wa kwanza kulia) akimpa maelekezo ya namna ya kupanda mlima Meru Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (wa kwanza kushoto)alipotembela hifadhi hiyo iliyoko mkoani Arusha leo tarehe 29/12/2017 kama juhudi za kuhaasisha utalii wa ndani nchini.Kulia kwake ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Ndg. Godfrey Mngereza na Dkt. Godwin Maimu Rais wa taasisi ya TOGOANE. Taasisi ya TAGOANE ndiyo iliyo ratibu safari hiyo.
(PICHA NA OCTAVIAN KIMARIO-WHUSM
COMMENTS