MKUU WA WILAYA YA UBUNGO AZINDUWA KAMPENI YA SIKU 16 KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA
HomeJamii

MKUU WA WILAYA YA UBUNGO AZINDUWA KAMPENI YA SIKU 16 KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, Kisare Makori akihutubia washiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni ya Siku 16 za kupin...

YALIYOJIRI KATIKA ZIARA YA KAMISHNA WA UHAMIAJI ZANZIBAR, MKOA WA KASKAZINI PEMBA
TANESCO "YALIA" NA WAHARIBIFU WA MAZINGIRA MITO INAYOLISHA BWAWA LA MTERA
YANAYOJIRI KATIKA ZIARA YA KIKAZI YA BALOZI MAHIGA NCHINI CHINA


Mkuu wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, Kisare Makori akihutubia washiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilizoandaliwa na TGNP Mtandao.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi. Grace Kisetu akihutubia washiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilizoandaliwa na TGNP Mtandao.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi. Grace Kisetu (kushoto) akihutubia washiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilizoandaliwa na TGNP Mtandao. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, Kisare Makori.

Wanafunzi walioshiriki katika uzinduzi wa kampeni ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia wakiwasilisha mrejesho wa tafiti.



MKUU wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, Kisare Makori leo amezinduwa kampeni ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilizoandaliwa na TGNP Mtandao, zikiwa na ujumbe wa kutambua mchango wa klabu za jinsia katika harakati za kupinga ukatili wa jinsia.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Makori alisema kiwango cha ukatili wa kijinsia nchini na duniani bado ni kikubwa, kwani taarifa ya afya ya uzazi na mtoto na viashiria vya malaria Tanzania ya mwaka 2015/16 inaonesha kuwa wanawake wanne kati ya 10 wamewahi kukumbana na ukatili wa kimwili tangu wakiwa na umri wa miaka 15.

Alisema takwimu hizo zinaonesha kuwa asilimia 42 waliowahi kuolewa wamekumbana na ukatili wa wenza wao ama wa kimwili au ukatili unaohusiana na kingono. "Hivyo basi nawaomba Watanzania wenzangu katika maeneo yenu pazeni sauti na kufanya kwa vitendo kupinga masuala ya ukatili wa kijinsia unaowakumba sana wanawake na watoto," alisisitiza Mkuu wa Wilaya, Bw. Makori.

Awali akizungumza kabla ya hotuba ya mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi. Grace Kisetu alisema lengo kuu la kampeni za mwaka huu kwao ni kushirikisha mawazo na uzoefu wa shule katika harakati za kumlinda mtoto wa kike ndani na nje ya shule dhidi ya ukatili wa kijinsia.

Alisema mengine ni pamoja na kutambua mchango wa klabu za jinsia katika harakati za kupinga ukatili wa kijinsia, kutumia michezo au sanaa katika kuwezesha kampeni za kupambana na ukatili wa kijinsia, elimu ya afya ya uzazi kwa vijana.



[caption id="attachment_83196" align="aligncenter" width="500"] 'MC' katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, Degratius Temba akiongoza hafla hiyo iliyoandaliwa na TGNP Mtandao na kufanyika Mabibo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi walioshiriki katika uzinduzi wa kampeni ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilizoandaliwa na TGNP Mtandao uliofanyika Mabibo jijini Dar es Salaam.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MKUU WA WILAYA YA UBUNGO AZINDUWA KAMPENI YA SIKU 16 KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA
MKUU WA WILAYA YA UBUNGO AZINDUWA KAMPENI YA SIKU 16 KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA
http://s3-us-west-2.amazonaws.com/thehabari.com/wp-content/uploads/2017/12/12170343/IMG_0691-500x490.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/12/mkuu-wa-wilaya-ya-ubungo-azinduwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/12/mkuu-wa-wilaya-ya-ubungo-azinduwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy