WAZIRI MKUU AUNGANA NA WANASONGEA KUOMBOLEZA KIFO CHA MAREHEMU LEONIDAS GAMA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisaini kitabu cha maombolezo, Nyumbani kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Songea, Leonidas Gama. Waziri Mkuu aliungana na wanafamilia pamoja na wananchi wa Songea katika kijiji cha Lukuyi Wilayani Songea leo Novemba 25/2017 katika kuomboleza msiba


HomeJamii

WAZIRI MKUU AUNGANA NA WANASONGEA KUOMBOLEZA KIFO CHA MAREHEMU LEONIDAS GAMA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameungana  na wanafamilia, wananchi wa Songea katika kuomboleza kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo la Songea,...

WATUHUMIWA 267 WAKAMATWA JIJINI DAR ES SALAAM KWA MAKOSA MBALIMBALI.
TAARIFA KUHUSU MISHENI YA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA SADC TROIKA NCHINI JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO (DRC)
TTB TANZANIA KUITUMIA ISRAEL KATIKA KUTANGAZA VIVUTIO VYAKE VYA UTALII NCHINI


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameungana na wanafamilia, wananchi wa Songea katika kuomboleza kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo la Songea, Bw. Leonidas Gama, nyumbani kwa marehemu Likuyu wilayani Songea.

Bw. Gama   amefariki dunia jana (Ijumaa, Novemba 24, 2017) katika Hospitali ya Peramiho mkoani Ruvuma alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu anatarajiwa kuzikwa Jumatatu, Novemba 27, 2017 katika kijiji cha Likuyu wilayani Songea.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali, Waziri Mkuu amesema kifo hicho ni pigo kwa Serikali kwa sababu marehemu alishirikiana nayo vizuri tangu akiwa mtumishi wa umma na hata baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa Jimbo la Songea.

Waziri Mkuu amesema msiba huo umeleta mtikisiko mkubwa kwa sababu baada ya kurudi nchini kutoka India alikokuwa akipatiwa matibabu aliwaeleza kuwa hali yake kwa sasa ni nzuri. ”Ametuachia pengo kubwa ambalo hatuna namna ya kuliziba.”

Ameongeza kuwa alipokea taarifa za msiba huo kwa huzuni na mshtuko mkubwa kwa sababu siku mbili kabla ya Waziri Mkuu kuanza ziara yake mkoani Ruvuma, Bw. Gama alimpigia simu na kumjulisha kwamba yeye anatangulia Songea kumpokea.

“Kifo ni mipango ya Mwenyezi Mungu na kwamba Bw. Gama ametangulia nasi tutafuata, hivyo wajibu wetu sote ni kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema. Gama alikuwa kiongozi na mwanga wa maendeleo.”

Pia Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwaomba wanafamilia, mke wa marehemu na watoto na wananchi wa jimbo la Songea waendelee kuwa watulivu na wavumilivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wetu.”

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Bibi Christine Mndeme alimshukuru Waziri Mkuu kwa kutenga muda wake na kwenda kuwafariji wafiwa licha ya majukumu mengi na makubwa aliyonayo.

Awali msemaji wa familia Bw. Issa Fusi alimshukuru Waziri Mkuu pamoja na viomgozi mbalimbali waliojitokeza na kuwafariji baada ya kutokea kwa msiba huo.”Kaka yetu tulimpenda sana kazi ya Mungu haina makosa.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 

JUMAMOSI, NOVEMBA 25, 2017.


Waziri Mkuu Kassim, Majaliwa leo Novemba 25/2017 ameungana na wanafamilia, wananchi wa Songea katika kuomboleza kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo la Songea, Bw. Leonidas Gama, nyumbani kwa marehemu Likuyu wilayani Songea.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MKUU AUNGANA NA WANASONGEA KUOMBOLEZA KIFO CHA MAREHEMU LEONIDAS GAMA
WAZIRI MKUU AUNGANA NA WANASONGEA KUOMBOLEZA KIFO CHA MAREHEMU LEONIDAS GAMA
https://i.ytimg.com/vi/jeTZrdfAHiE/hqdefault.jpg
https://i.ytimg.com/vi/jeTZrdfAHiE/default.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/11/waziri-mkuu-aungana-na-wanasongea.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/11/waziri-mkuu-aungana-na-wanasongea.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy