WAFANYABIASHARA NA WAJASIRIAMALI WANAWAKE WATAKIWA KUJENGA UTHUBUTU WA KUTENDA KUJIKWAMUA KIUCHUMI
  Mmoja wa wawezeshaji wa mkutano wa jukwaa la Wajasiriamali na Wafanyabiashara Wanawake ulioandaliwa na Taasisi ya Dominion Leadership Connect akizungumza na wajumbe wa jukwaa lililofanyika Novemba 23, 2017 Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuwajengea uwezo Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake kukabiliana na changamoto mbali katika fursa za kiuchumi.


HomeBiashara

WAFANYABIASHARA NA WAJASIRIAMALI WANAWAKE WATAKIWA KUJENGA UTHUBUTU WA KUTENDA KUJIKWAMUA KIUCHUMI

Na Ismail Ngayonga MAELEZO DAR ES SALAAM 25.11.2017 WAFANYABIASHARA na Wajasiriamali Wanawake nchini wametakiwa kuwa na uthubutu...

WAZIRI MPINA ATOZA FAINI YA MILIONI 180 VIWANDA VYA KUCHAKATA MINOFU YA SAMAKI, AWASIMAMISHA KAZI VIGOGO WATATU KITENGO CHA UDHIBITI WA USALAMA NA UBORA WA MAZAO YA UVUVI
CCM WILAYA YA GEITA WALAANI JESHI LA ZIMA MOTO KUWATOZA FEDHA KUBWA WACHIMBAJI BILA YA KUWAPATIA RISITI
MKAZI MWINGINE WA TEMEKE MIKOROSHINI AIBUKA NA KITITA CHA MILIONI 50 ZA TATUMZUKA.

Na Ismail Ngayonga
MAELEZO
DAR ES SALAAM
25.11.2017

WAFANYABIASHARA na Wajasiriamali Wanawake nchini wametakiwa kuwa na uthubutu wa kutenda na kufikia malengo waliyojiwekea kwa kutumia fursa zilizopo ili kujiletea maendeleo ya kiuchumi katika jamii inayowazunguka.

Wito huo huo umetolewa (juzi) Novemba 23, 2017 Jijini Dar es Salaam na Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Mwajuma Magwiza wakati wa mkutano wa Jukwaa la Mwanamke Mjasiriamali na Ubunifu liliondaliwa na Taasisi ya Dominion Leadership Connect.
Magwiza alisema Wanawake ndio kundi kubwa katika jamii ya Watanzania na wanapaswa kutambua kuwa hakuna njia ya mkato katika kuyafikia mafanikio yao kiuchumi na badala yake wajihangaishe katika kutatua changamoto zilizopo ili kupata mafanikio katika shughuli mbalimbali za kila ikiwemo biashara na ujasiriamali..
“Serikali imefungua milango ya ushirikiano kwa kuanisha fursa za kujikwamua kiuchumi kwa Wafanyabiashara na Wajasiriamali wanawake, zipo taratibu zilizoanishwa katika kuzifikia fursa hizo na hivyo ni wajibu wetu kuachana na mazoea ya utamaduni ulijiongezeka katika jamii yetu” alisema Magwiza.
Kwa mujibu wa Magwiza alisema Serikali inatambua changamoto mbalimbali zinazowakabili Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake nchini ikiwemo ukosefu wa mtaji ya biasharara, ambapo hata hivyo halmashauri mbalimbali nchini zimeanza kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kutenga asilimia 5 ya bajeti zao kwa ajili ya kusaidia vikundi vya Wanawake na Vijana.
Aidha Magwiza aliwataka Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake kutambua kuwa mtaji sio kigezo cha kukwama katika kujiletea maendeleo yao na badala yake watumie majukwaa yao kuwa chachu ya mabadiliko ya kifikra na hatimaye kufikia malengo waliyojiwekea.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya GIBR FARM, Hadija Jabir alisema safari ya mabadiliko ya kiuchumi kwa Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake nchini itapata mafanikio makubwa iwapo jamii hiyo itaunganisha nguvu ya pamoja katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowazunguka.
Aliongeza kuwa ili mafanikio hayo yaweze kupatikana ni wajibu wa Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake walielezane ukweli na uwazi uliopo katika kubaini fursa na kutumia rasilimali zilizopo ili ziweze kuwaletea maendeleo ya haraka.
“Safari ya kujikwamua kiuchumi huwa ngumu katika ngazi za awali, kwa upande wetu kampuni ya GIBR FARM inayojihusisha na uzalishaji wa mbogamboga na matunda, tumefanikiwa kupanua wigo wa soko na sasa tunauza bidhaa zetu katika nchi za Sweden, Italy na Ujerumani” alisema Hadija.
Naye Mwanzilishi wa Kampuni ya uzalishaji kuku ya GOKUKUZ, Bulla Boma alisema kumekuwepo na changamoto ya fursa za masoko katika mauzo ya bidhaa kwa Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake hususani waliopo katika mfumo usio rasmi, hatua inayowafanya wengi wao kukatishwa tamaa wakiwa katika ngazi za awali.
Hata hivyo alisema kutokana na kupanua wigo wa ushirikano na mawasiliano na Wafanyabishara na Wajasiriamali wakubwa waliopo nchini, kampuni yake kwa sasa imejiwekea malengo ya kupanua wigo wa bidhaa hiyo katika soko la kimataifa.
Kongamano hilo lilibeba kauli mbiu ya “Mwanamke Mjasiriamali na Ubunifu” lililenga katika kuhamasisha Wafanyabiashara na Wajasiriamali wanawake nchini kuibua na kutumia fursa za kiuchumi ili kuweza kuwaletea maendeleo yao katika jamii.

Baadhi ya Wafanyabiashara na Wajasirimali Wanawake wakifuatilia mkutano wa jukwaa la Wajasiriamali na Wafanyabiashara Wanawake ulioandaliwa na Taasisi ya Dominion Leadership Connect lililolenga kuwajengea uwezo na Wajasiriamali wa kukabiliana na changamoto mbali katika fursa za kiuchumi. Mkutano huo ulifanyika Novemba 23 2017.



 Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Mwajuma Magwiza akuzungumza na Wajasiriamali na Wafanyabiashara Wanawake wakati wa mkutano wa jukwaa la Wafanyabiashara Wanawake lililoandaliwa na Taasisi ya Dominion Leadership Connect lililofanyika jana Novemba 23, 2017 Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuwajengea uwezo Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake kukabiliana na changamoto mbali katika fursa za kiuchumi.



 Baadhi ya Wafanyabiashara na Wajasirimali Wanawake wakifuatilia mkutano wa jukwaa la Wajasiriamali na Wafanyabiashara Wanawake ulioandaliwa na Taasisi ya Dominion Leadership Connect lililolenga kuwajengea uwezo na Wajasiriamali wa kukabiliana na changamoto mbali katika fursa za kiuchumi. Mkutano huo ulifanyika Novemba 23 2017.



Mgeni rasmi katika mkutano wa jukwaa la Wajasiriamali na Wafanyabiashara Wanawake, Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Mwajuma Magwiza akiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa jukwaa hilo mara baada ya kumalizika ikwa mkutano huo uliofanyika Jijini Dar es Salaam Novemba 23, 2017 


 Mwanzilishi wa Tamasha la Nyamachoma, Carol Ndosi akizungumza na Wajasiriamali na Wafanyabiashara Wanawake wakati wa mkutano wa jukwaa la Wafanyabiashara Wanawake lililoandaliwa na Taasisi ya Dominion Leadership Connect lililofanyika Novemba 23, 2017 Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuwajengea uwezo Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake kukabiliana na changamoto mbali katika fursa za kiuchumi.






Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAFANYABIASHARA NA WAJASIRIAMALI WANAWAKE WATAKIWA KUJENGA UTHUBUTU WA KUTENDA KUJIKWAMUA KIUCHUMI
WAFANYABIASHARA NA WAJASIRIAMALI WANAWAKE WATAKIWA KUJENGA UTHUBUTU WA KUTENDA KUJIKWAMUA KIUCHUMI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEibhAk0mak0b8amplGgvK9DrG6jGJ_cwnW-M51Q7JNMTzo1bgXuOHwBI8Sst0STOrlYPsORvYgB9vx6ygxsyuW6ArgxYOlBzWnUh4SKvi6hK4xatHGzR66zXKLsKKmefZNEUNIgYhMeQUU/s640/1..JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEibhAk0mak0b8amplGgvK9DrG6jGJ_cwnW-M51Q7JNMTzo1bgXuOHwBI8Sst0STOrlYPsORvYgB9vx6ygxsyuW6ArgxYOlBzWnUh4SKvi6hK4xatHGzR66zXKLsKKmefZNEUNIgYhMeQUU/s72-c/1..JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/11/wafanyabiashara-na-wajasiriamali.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/11/wafanyabiashara-na-wajasiriamali.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy