UFAFANUZI KUHUSU SHERIA MPYA YA TTCL KWA VYOMBO VYA HABARI
HomeJamii

UFAFANUZI KUHUSU SHERIA MPYA YA TTCL KWA VYOMBO VYA HABARI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO Telegram:  “MAWASILIANO” 3 Mtaa wa Moshi, Simu:...

PROF. MBARAWA AAHIDI KUKAMILIKA KWA UJENZI WA DARAJA LA MTO MARA
MPINA AMUAGIZA KATIBU MKUU UVUVI, KUHARAKISHA MCHAKATO WA KUTAIFISHA MELI YA KAMPUNI YA BUAH NAGA ONE.
MAMIA WAJITOKEZA KUMUAGA MWANAHABARI PATRICK MWILLONGO


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO


Telegram:  “MAWASILIANO” 3 Mtaa wa Moshi,
Simu: 255(0)26 2324518                                                                   S.L.P. 677,
Nukushi:  255(0)26 23211027 40470 DODOMA.
BaruaPepe: ps@mst.go.tz                                                                           17 Novemba, 2017
Tovuti: www.mwtc.go.tz

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


UFAFANUZI KUHUSU UPOTOSHAJI WA VICHWA VYA MAGAZETI KUHUSU SHERIA MPYA YA SHIRIKA LA MAWASILIANO TANZANIA, 2017


Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano) inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) iliyotolewa kwenye magazeti ya Mwananchi na Uhuru ya tarehe 15/11/2017. Gazeti la Mwananchi liliandika, “Serikali ‘yaiua’ rasmi TTCL na gazeti la Uhuru liliandika,“TTCL ‘bye’ ‘bye’. Vichwa hivi vya habari vimewachanganya wasomaji na kuleta taharuki kwa wateja na wafanyakazi wa TTCL, wadau wa Sekta ya Mawasiliano na wananchi kwa ujumla.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amewasilisha Muswada wa Sheria ya Shirika la Mawasiliano Tanzania katika mkutano wa Tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 14 Novemba, 2017 mjini Dodoma. Bunge lilijadili na kupitisha Muswada na kutungwa kuwa Sheria itakayoanzisha Shirika la Mawasiliano Tanzania. Madhumuni ya Muswada yalikuwa ni kuanzisha Shirika la Umma la Mawasiliano nchini kwa ajili ya kulinda usalama wa nchi, kukuza uchumi na kutoa huduma za mawasiliano kwa ubora unaotakiwa. Pia, kulipa Shirika la Mawasiliano jukumu la kusimamia miundombinu ya kimkakati ya mawasiliano nchini.


Sheria mpya itaiwezesha TTCL kutekeleza majukumu yake kama Shirika la Mawasiliano nchini. Hizi ni jitihada za Serikali kuimarisha TTCL na sio kuiua. TTCL bado ipo na itaendelea kutekeleza majukumu yake kama Shirika la Mawailiano nchini. Shirika litaendelea kutoa huduma kwa wananchi kwa ubora na ufanisi zaidi.


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,


Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

17 Novemba, 2017
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: UFAFANUZI KUHUSU SHERIA MPYA YA TTCL KWA VYOMBO VYA HABARI
UFAFANUZI KUHUSU SHERIA MPYA YA TTCL KWA VYOMBO VYA HABARI
https://lh6.googleusercontent.com/dKGjoIHk9IdoKr6bHpLTBGSPXx_2BPTHvoj-DbQgw9e8jJGF_UbDiyyUi1uADoSqW_cLWhJnEjeNqtU_nkSyHLhrYSRZ_Nbr0Xn0gneoHX2TZyf_WrePQT2gv3ZP3BdRs8HsAZUoZJ_0Fm4Zsw
https://lh6.googleusercontent.com/dKGjoIHk9IdoKr6bHpLTBGSPXx_2BPTHvoj-DbQgw9e8jJGF_UbDiyyUi1uADoSqW_cLWhJnEjeNqtU_nkSyHLhrYSRZ_Nbr0Xn0gneoHX2TZyf_WrePQT2gv3ZP3BdRs8HsAZUoZJ_0Fm4Zsw=s72-c
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/11/ufafanuzi-kuhusu-sheria-mpya-ya-ttcl.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/11/ufafanuzi-kuhusu-sheria-mpya-ya-ttcl.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy