SERIKALI YAJIPANGA KUBORESHA MFUMO WA USIMAMIZI WA MASHAURI YA WATOTO KATIKA NGAZI YA JAMII NCHINI
Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga akisaini Mwongozo wa Kitaifa Kuhusu Mafunzo ya Usimamizi Jumuishi wa Mashauri ya Watoto kwa Wasimamizi wa Mashauri ya watoto Ngazi ya Jamii sanjari na Kitini cha Wasimamizi wa Mashauri ya watoto Ngazi ya Jamii Kuhusu Mfumo Jumuishi wa Kitaifa wa Kuhudumia Mashauri ya Watoto Ofisini kwake Mjini Dodoma ukiwa umeandaliwa na Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI, Shirika la JSI na kufadhiliwa na USAID leo Novemba 01, 2017. 
HomeJamii

SERIKALI YAJIPANGA KUBORESHA MFUMO WA USIMAMIZI WA MASHAURI YA WATOTO KATIKA NGAZI YA JAMII NCHINI

Na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW Serikali ya Tanzania imedhamiria kuboresha na kulinda ustawi wa watoto wote Tanzania na kupunguza...

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA MAKAMU MWENYEKITI WA SHIRIKISHO LA VIWANDA CHINA NA MABALOZI
PROF. MBARAWA AITAKA BODI YA DMI KUBORESHA MIUNDOMBINU
UN YAENDELEA KUHAMASISHA VIJANA KUTAMBUA MALENGO 17 YA DUNIA (SDGS)



Na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

Serikali ya Tanzania imedhamiria kuboresha na kulinda ustawi wa watoto wote Tanzania na kupunguza athari zinazotokana na VVU, umasikini, vifo vya wazazi  ulemavu, utelekezaji wa watoto, ndoa, mimba za utotoni na  ukatili dhidi ya watoto.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga mjini Dodoma wakati akisaini Mwongozo wa Kitaifa kuhusu Mafunzo ya Usimamizi Jumuishi wa Mashauri ya Watoto kwa Wasimamizi wa Mashauri ya watoto Ngazi ya Jamii.

Katibu Mkuu Sihaba Nkinga amesema kuwa Mwongozo huu una lengo la kutekeleza  Mpango wa Taifa wa Pili wa Huduma Kwa Watoto Walio Katika Mazingira Hatarishi (2013-2017) unaolenga kuboresha ustawi na ulinzi wa watoto kwa kulinda haki zao, kuzuia na kupunguza matukio hatarishi na yenye madhara kwa watoto.  

“Mwongozo huu utatusaidia kupambana na changamoto zinazowakabili watoto wetu katika kulinda Haki, ustawi na ulinzi wao” alisema Bibi Sihaba.

Kwa upande wake Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabikira Mushi amesema kuwa wasimamizi wa Mashauri ya Watoto Ngazi ya Jamii watapatiwa mafunzo kuhakikisha mashauri  ya dharura yanashughulikiwa haraka na mashauri yote ya ulinzi yanapewa rufaa kwa katika mifumo iliyopo kwa uangalizi wa Afisa Ustawi wa Jamii.

Ameongeza kuwa Mafunzo hayo yanalenga kuwaandaa Wasimamizi wa Mashauri ya Watoto Ngazi ya Jamii kuelewa na kuzingatia ipasavyo hatua za uratibu wa Mashauri ya Watoto kwa kuanzia na utambuzi wa tukio wa mtoto aliyefanyiwa unyanyasaji au ukatili hadi kutoa msaada stahiki kwa Mtoto aliye katika mazingira hatarishi katika jamii zetu.

Mwongozo huu utasaidia kuandaa Mfumo wa Usimamizi Jumuishi wa Kitaifa kuhusu Mashauri ya watoto katika ngazi ya Jamii ambao utawezesha uratibu kwa kuunganisha wasimamizi wa ustawi wa jamii, ulinzi, na kutoa huduma zinazohusiana na maambukizi ya VVU kwa kuunganishwa na Mifumo iliyopo katika ngazi za Serikali za mitaa.

Mwongozo wa Kitaifa kuhusu Mafunzo ya Usimamizi Jumuishi wa Mashauri  ya Watoto kwa Wasimamizi wa Mashauri ya watoto Ngazi ya Jamii umeratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na OR-TAMISEMI kwa hisani ya Shirika la USAID/PEPFAR.



Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii, Rabikira Mushi akisaini Mwongozo wa Kitaifa Kuhusu Mafunzo ya Usimamizi Jumuishi wa Mashauri ya Watoto kwa Wasimamizi wa Mashauri ya Watoto Ngazi ya Jamii sanjari na Kitini cha Wasimamizi wa Mashauri ya watoto Ngazi ya Jamii Kuhusu Mfumo Jumuishi wa Kitaifa wa Kuhudumia Mashauri ya Watoto Ofisini kwake Mjini Dodoma ambao umeandaliwa na Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI, Shirika la JSI na kufadhiliwa na USAID leo Novemba 01, 2017.

Baadhi ya vitabu vya Mwongozo wa Kitaifa Kuhusu Mafunzo ya Usimamizi Jumuishi wa Mashauri ya Watoto kwa Wasimamizi wa Mashauri ya Watoto Ngazi ya Jamii na Kitini cha Wasimamizi wa Mashauri ya watoto Ngazi ya Jamii Kuhusu Mfumo Jumuishi wa Kitaifa wa Kuhudumia Mashauri ya Watoto ambavyo vimesainiwa rasmi katika Ofisi ya Wizara Mjini Dodoma. 

Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga (aliyekaa) akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kusaini Mwongozo wa Kitaifa wa Mafunzo ya Usimamizi Jumuishi wa Mashauri ya Watoto kwa Wasimamizi wa Mashauri ya watoto Ngazi ya Jamii kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Shirika la JSI John Stephen, wa pili kulia ni Afisa Ustawi wa Jamii BW. Philbert Kawemama, wa tatu kulia ni Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabikira Mushi, kushoto ni Mshauri wa Ustawi wa Jamii na ulinzi wa Mtoto kutoka JSI Bw. Peter Massesa, wa pili kushoto ni Afisa Ustawi na Ulinzi wa Mtoto Bi Christina Mdemu na wa tatu kushoto ni Mwanasheria wa Wizara Bw. January Kitunsi. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW) 









Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI YAJIPANGA KUBORESHA MFUMO WA USIMAMIZI WA MASHAURI YA WATOTO KATIKA NGAZI YA JAMII NCHINI
SERIKALI YAJIPANGA KUBORESHA MFUMO WA USIMAMIZI WA MASHAURI YA WATOTO KATIKA NGAZI YA JAMII NCHINI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghVATGflOSXIULxyeUMONGMfea2w7rQeSYZivJWROBJktKdEhsuVQx19atfF0f20fQKuCTki55tbh_ORhS9-xWIWwAvmEGECTVBj0Cq2-nan-xEr6REEY80RVHxX6xoki5hu7k0cSielE/s640/Pix+1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghVATGflOSXIULxyeUMONGMfea2w7rQeSYZivJWROBJktKdEhsuVQx19atfF0f20fQKuCTki55tbh_ORhS9-xWIWwAvmEGECTVBj0Cq2-nan-xEr6REEY80RVHxX6xoki5hu7k0cSielE/s72-c/Pix+1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/11/serikali-yajipanga-kuboresha-mfumo-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/11/serikali-yajipanga-kuboresha-mfumo-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy