WAHANDISI WA TANESCO WAPAMBANA USIKU NA MCHANA KUREJESHA UMEME KATIKA HALI YAKE YA KAWAIDA MIKOA YA MTWARA NA LINDI
HomeJamii

WAHANDISI WA TANESCO WAPAMBANA USIKU NA MCHANA KUREJESHA UMEME KATIKA HALI YAKE YA KAWAIDA MIKOA YA MTWARA NA LINDI

  Mhandisi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), akifanyia matengenezo moja ya mashine za kufua umeme kwenye kituo cha kufua...

WAZIRI MKUU AKABIDHIWA KAZI YA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA
CSSC YAFIKISHA MIAKA 25 TANGU KUANZISHWA IKIWA
WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AZINDUA MAZOEZI YA KITAIFA MKOANI DODOMA LEO




WAHANDISI WA TANESCO WAPAMBANA USIKU NA MCHANA KUREJESHA UMEME KATIKA HALI YAKE YA KAWAIDA MIKOA YA MTWARA NA LINDI
 Mhandisi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), akifanyia matengenezo moja ya mashine za kufua umeme kwenye kituo cha kufua umeme Mtwara, leo Oktoba 14, 2017
 Wahandisi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), akifanyia matengenezo moja ya mashine za kufua umeme kwenye kituo cha kufua umeme Mtwara, leo Oktoba 14, 2017

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, Mtwara
WAHANDISI na mafundi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), wanapambana usiku na mchana kuzifanyia matengenezo mashine za kufua umeme, ili kuondoa tatizo la kukosekana kwa umeme kwa vipindi virefu kila siku kwenye mikoa ya Mtwara na Lindi.

 Akizungumza mjini hapa leo Oktoba 14, 2017, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, anayeshughulikia Uzalishaji, Mhandisi Kaitwa Bashaija, (pichani juu), amesema kwa sasa Wahandisi na mafundi wa shirika hilo wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana ili kutengeneza mitambo hiyo na hivyo kuhakikisha tatizo hilo linapatiwa ufumbuzi kwa haraka.

K-VIS BLOG ilishuhudia mafundi hao wakifanyakazi ya kurekebisha mitambo hiyo katika kituo cha kuzalisha umeme wa kutumia gesi asilia mkoani Mtwara leo Oktoba 14, 2017.

“Mitambo hii ina kiasi cha mika 10 tangu ifungwe, na kadiri miaka inavyokweda ndivyo ongezeko la uhitaji wa umeme hususan mkoani Mtwara linazidi kuongezeka kutokana na kukua kwa shughuli za kiuchumi,” Alisema Mhandisi Bashaija.

Alisema, miaka michache iliyopita baadhi ya mitambo iliweza kuzimwa na bado hali ya umeme ilikuwa imara.Wiki iliyopita Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani aliagiza TANESCO kufanya juhudi za ziada kuhakikisha tatizo la umeme mkoani Mtwara na Lindi linapatiwa ufumbuzi wa haraka.

Kutokana na hali hiyo Naibu Mkurugenzi huyo wa TANESCO, alisema kuwa kwa sasa wana mipango ya muda mfupi na mrefu katika kuhakikisha wanaimarisha miundombinu ya umeme katika mikoa ya kusini.

Kwa upande wake Meneja wa Kituo cha Kuzalisha Umeme wa kutumia gesi asilia cha Mtwara, Mhandisi Mkulungwa Chinumba, alisema kuwa licha ya changamoto hiyo kwa sasa bado mitambo iliyopo ina uwezo mkubwa wa kuzalisha umeme katika mikoa hiyo.

“Pamoja na hali hii lakini kwa sasa tunakwenda vizuri kiasi ila si sana maana umeme kuna wakati unarudi na kukatika. Na tunaamini tutafanikiwa kurudi katika hali ya kawaida na kikubwa tunawaomba wananchi wa mikoa ya Mtwara na Lindi kutuvumilia kwani nasi tunajua umuhimu wa umeme katika shughuli za uzalishaji.” Alitoa rai Mhandisi Chinumba.


 Meneja wa Kituo cha Kuzalisha Umeme wa kutumia gesi asilia cha Mtwara, Mhandisi Mkulungwa Chinumba, akizungumzia hatua zinazoendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha tatizo hilo linapatiwa ufumbuzi wa haraka.




 Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari walipotembelea kituo cha kuzalisha umeme wa gesi asilia mkoani Mtwara Oktoba 14, 2017.






 Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayeshughulikia zualishaji umeme, Mhandisi Costa
 Msanifu gazeti wa gazeti la Mwananchi, Bi. Lilian Timbuka akiuliza swali.
 Meneja wa Kituo cha Kuzalisha Umeme wa kutumia gesi asilia cha Mtwara, Mhandisi Mkulungwa Chinumba, akizungumzia hatua zinazoendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha tatizo hilo linapatiwa ufumbuzi wa haraka. Kulia ni Mhandisi Bashaija.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAHANDISI WA TANESCO WAPAMBANA USIKU NA MCHANA KUREJESHA UMEME KATIKA HALI YAKE YA KAWAIDA MIKOA YA MTWARA NA LINDI
WAHANDISI WA TANESCO WAPAMBANA USIKU NA MCHANA KUREJESHA UMEME KATIKA HALI YAKE YA KAWAIDA MIKOA YA MTWARA NA LINDI
https://i.ytimg.com/vi/L7nzODmOo2E/hqdefault.jpg
https://i.ytimg.com/vi/L7nzODmOo2E/default.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/10/wahandisi-wa-tanesco-wapambana-usiku-na.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/10/wahandisi-wa-tanesco-wapambana-usiku-na.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy