RAIS MAGUFULI AGOMA KUUFUTA MWENGE WA UHURU
HomeJamii

RAIS MAGUFULI AGOMA KUUFUTA MWENGE WA UHURU

Rais Magufuli akihutubia. RAIS John Magufuli ambaye leo Oktoba 14, 2017 ni Mgeni Rasmi kwenye Maadhimisho ya Kumbukum...

DKT. SHEIN AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI MJINI ZANZIBAR
WASHINDI WA AFYABANDO KWENYE DROO YA PILI WAPATIKA LEO
WANANCHI KIBAMBA KIBWEGERE UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM WALILIA ULINZI


Rais Magufuli akihutubia.

RAIS John Magufuli ambaye leo Oktoba 14, 2017 ni Mgeni Rasmi kwenye Maadhimisho ya Kumbukumbu ya kifo cha Rais wa kwanza wa Tanzania Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Kilele cha Mbio za Mwenge amesema amejisikia faraja kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo ikiwa ni mara yake ya kwanza kushiriki maadhimisho hayo tangu awe Rais.

Aidha, Magufuli amemuelezea Hayati Mwl. Nyerere kama kiongozi shupavu alipeginani maslahi ya wanyonge na kupambana na wakoloni katyika kufanikisha kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika, Zanzibar na nchi nyingine za Afrika.

Amesema Nyerere alianza harakati za siasa mwaka 1953 baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa Chama cha TAA ambacho baadaye kilizaa TANU huku akiwa Mwalimu wa Shule ya Sekondari ambayo kwa sasa inaitwa Pugu Sekondari ambapo baadaye aliacha kazi hiyo ya kiufundisha na kujikita kwenye siasa za ukombozi.

Magufuli piua amesema iwapo Mwl. Nyerere angekuwa kiongozi mwenye tamaa au mbinafs, basi angechukua fukwe zote za Msasani, jijini Dar es Salaam na kuzifanya ziwe za mali yake, lakini hakufanya hivyo kwa sababu ya uzalendo mkiubwa aliokuwa nao.

Rais amesisitiza kuwa kamwe hatokukubali mbio za Mwenge wa Uhuru zifutwe katika kipindi chake cha uongozi, kwani mwenge huo una manufaa makubwa kwa Taifa ikiwemo kuzindua miradi mbalimbali za maendelo pamoja na kuwa nembo muhimu kwa Taifa letu.

Amesema wanaotaka mwenge huo ufutwe huenda hawajui historia ya nchi hii na kwamba kama wanaweza kukubali fimbo na kombe la dunia vikaletwa nchini na wakavipokea basi mbio za mwenge ni muhimu zaidi kuliko wanavyodhani.

Akizungumzia hali ya uchumi wa nchi, rais amekanusha wanaodai kuwa uchumi umeshuka huku akieleza kuwa uchumi wa Tanzania unazidi kupanda hukui mfumuko wa bei ukishuka na matokeo yake yanaonekana kwenye bidhaa pamoja na kushuka bei zake. Pia ameeleza kuongezeka kwa viwanda na wawekezaji wa kibiashara hapa nchini.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RAIS MAGUFULI AGOMA KUUFUTA MWENGE WA UHURU
RAIS MAGUFULI AGOMA KUUFUTA MWENGE WA UHURU
https://i.ytimg.com/vi/P1tpsDBjwQQ/hqdefault.jpg
https://i.ytimg.com/vi/P1tpsDBjwQQ/default.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/10/rais-magufuli-agoma-kuufuta-mwenge-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/10/rais-magufuli-agoma-kuufuta-mwenge-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy