THBUB YATOA ZUIO UHAMISHAJI WANANCHI LOLINDO

- Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Kitalu Na. 8, Mtaa wa Luthuli S.L.P 2643, DAR ES SALAAM Simu: +255 22 2135747/8; 213...




-
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
Kitalu Na. 8, Mtaa wa Luthuli
S.L.P 2643, DAR ES SALAAM
Simu: +255 22 2135747/8; 2137125; 2135222
Faksi: +255 22 2111281
Tovuti: www.chragg.go.tz

Septemba 5, 2017
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

THBUB yatoa zuio la kusitisha operesheni ya kuwahamisha na kuwachomea wananchi wa Loliondo makazi yao

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jana (Septemba 4, 2017) ilitoa zuio la muda (interim order) kusitisha operesheni ya kuwaondoa kwa nguvu wananchi katika maeneo wanayoishi na kuwachomea makazi (maboma) yao huko Loliondo Wilaya ya Ngorongoro ili kulinda haki za pande zote.

Tume imechukua hatua hiyo kwa mamlaka iliyonayo kwa mujibu wa Ibara ya 130(1) (f) na (h) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Kifungu cha 25(1) (d) cha Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (Sura ya 391) ya Sheria za Tanzania.

Hatua hii imefikiwa kufuatia Tume kupokea malalamiko ya wananchi walioathiriwa na zoezi hilo kutoka Tarafa ya Loliondo Wilayani Ngorongoro, ambapo imeanza kufanyia uchunguzi malalamiko hayo.

Kwa mujibu wa taarifa za wananchi hao katika operesheni hiyo iliyoanza Agosti 12, 2017 na inayotekelezwa kwa pamoja na uongozi wa Wilaya ya Ngorongoro, askari wa wanyamapori kutoka Hifadhi ya Taifa Serengeti (SENAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na Jeshi la Polisi wilayani Ngorongoro kumekuwepo na uvunjwaji wa haki za binadamu na misingi ya utawala bora.

Wananchi hao wanadai kuwa wameondolewa kwa nguvu katika vijiji vyao halali vinavyotambuliwa kisheria, wamechomewa makazi yao moto isivyo halali na kuchukuliwa mifugo yao.

Pamoja na zuio hilo Tume imeziandikia mamlaka husika kuzitaka ziwasilishe kwake nyaraka zote zinazoonesha uhalali wa zoezi la kuwaondoa wananchi kwa kuwachomea makazi yao na kukamata mifugo yao.

Imetolewa na:
(SIGNED)

Bahame Tom Nyanduga
Mwenyekiti

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Septemba 5, 2017

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: THBUB YATOA ZUIO UHAMISHAJI WANANCHI LOLINDO
THBUB YATOA ZUIO UHAMISHAJI WANANCHI LOLINDO
https://lh4.googleusercontent.com/SZrQOrgoZ0gR3X2uJDqoPG2GXr5chpOEM_4fQbJCARpDMa-VnZArlIgt0M76IlumH4hg7oNmdj5LinguvzY7UZLzOGvg0HFuuzEXovxBsn6mfm86f-uFrV93_IpUVCYcRjdRbG8KlVk-PAiMOQ
https://lh4.googleusercontent.com/SZrQOrgoZ0gR3X2uJDqoPG2GXr5chpOEM_4fQbJCARpDMa-VnZArlIgt0M76IlumH4hg7oNmdj5LinguvzY7UZLzOGvg0HFuuzEXovxBsn6mfm86f-uFrV93_IpUVCYcRjdRbG8KlVk-PAiMOQ=s72-c
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/09/thbub-yatoa-zuio-uhamishaji-wananchi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/09/thbub-yatoa-zuio-uhamishaji-wananchi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy