TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA -WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA
HomeJamii

TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA -WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ipo salama na imara na kwamba mtu yeyote atakayejaribu kutaka kuvuruga amani atachu...

KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA SIHABA NKINGA AZINDUA MPANGO WA UHAKIKI WA NGO’S NCHINI.
RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA RAIS WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA MAENDELEO LA JAPAN (JICA) IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO
DREAMS INITIATIVES PROVIDES SAFE SPACE FOR ADOLESCENT GIRLS IN SHINYANGA AIMING AT PREVENTION OF RISKY HIV BEHAVIORS


 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ipo salama na imara na kwamba mtu yeyote atakayejaribu kutaka kuvuruga amani atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Septemba 13, 2017) alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Bw. Mousa Farhang jijini Dar es Salaam.

“Hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote kutoka popote atakayejaribu kuvuruga amani yetu. Nawaomba wananchi muwe makini na muendelee kuidumisha amani yetu.”Amesema kwa sasa Serikali ipo katika mapambano dhidi ya vitendo vya ufisadi, rushwa, biashara haramu ya dawa za kulevya pamoja na wahujumu uchumi.

Waziri Mkuu amesema licha ya Tanzania kuwa ni nchi ya amani na yenye utulivu wa kisiasa, wameendelea kuwahamasisha wananchi wake kudumisha mshikamano.Amesema mbali ya kuimarisha amani nchini, pia Serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji jambo ambalo litawawezesha watakaokuja kuwekeza nchini kupata tija.

Hivyo ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchini Iran ili waje kuwekeza kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya kuchakata mazao ya kilimo.Pia amewakaribisha raia wa Iran kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko nchini Tanzania kama mlima wa Kilimanjaro, fukwe, mali kale na mbuga za wanyama.

Kwa upande wake, Balozi Farhang ameipongeza Serikali kwa kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi na kupambana na dawa za kulevya na ufisadi.Balozi huyo amesema Serikali ya Irani ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi pamoja na vitendo vingine vya kihalifu.

Balozi Farhang ametumia fursa hiyo kuiomba Serikali ya Tanzania ifungue Ofisi ya Ubalozi nchini Iran ili kuimarisha uhusiano huo, ambapo Waziri Mkuu amekubali.Pia Bw. Farhang amesema aliwahi kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti na Ngorongoro na kusema kwamba ni maeneo mazuri ambayo hajawahi kuyaona tangu azaliwe.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMATANO, SEPTEMBA 13, 2017.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na Balozi wa Iran. Mousa Farhang nakufanya mazungumzo ya kikazi leo Septemba 13/2017.Ofisini kwake Magogoni Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na Balozi wa Iran. Mousa Farhang nakufanya mazungumzo ya kikazi leo Septemba 13/2017.Ofisini kwake Magogoni Dar es salaam. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ipo salama na imara na kwamba mtu yeyote atakayejaribu kutaka kuvuruga amani atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Septemba 13, 2017) alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Bw. Mousa Farhang jijini Dar es Salaam.

“Hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote kutoka popote atakayejaribu kuvuruga amani yetu. Nawaomba wananchi muwe makini na muendelee kuidumisha amani yetu.”Amesema kwa sasa Serikali ipo katika mapambano dhidi ya vitendo vya ufisadi, rushwa, biashara haramu ya dawa za kulevya pamoja na wahujumu uchumi.

Waziri Mkuu amesema licha ya Tanzania kuwa ni nchi ya amani na yenye utulivu wa kisiasa, wameendelea kuwahamasisha wananchi wake kudumisha mshikamano.Amesema mbali ya kuimarisha amani nchini, pia Serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji jambo ambalo litawawezesha watakaokuja kuwekeza nchini kupata tija.

Hivyo ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchini Iran ili waje kuwekeza kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya kuchakata mazao ya kilimo.Pia amewakaribisha raia wa Iran kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko nchini Tanzania kama mlima wa Kilimanjaro, fukwe, mali kale na mbuga za wanyama.

Kwa upande wake, Balozi Farhang ameipongeza Serikali kwa kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi na kupambana na dawa za kulevya na ufisadi.Balozi huyo amesema Serikali ya Irani ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi pamoja na vitendo vingine vya kihalifu.

Balozi Farhang ametumia fursa hiyo kuiomba Serikali ya Tanzania ifungue Ofisi ya Ubalozi nchini Iran ili kuimarisha uhusiano huo, ambapo Waziri Mkuu amekubali.Pia Bw. Farhang amesema aliwahi kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti na Ngorongoro na kusema kwamba ni maeneo mazuri ambayo hajawahi kuyaona tangu azaliwe.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMATANO, SEPTEMBA 13, 2017.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA -WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA
TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA -WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhlFmCAqLcZ9XiGekyviI0BSr2hBn1IrvLJQhREEcIkn5V5yHqaX5Zq3N_6zmYYuPytiD5i7C5JekkMBDJRJz4kFbAJKyzAUadiMAdTOb6MdV8ziPVQxihNun7RC4mcEVXeEQx05T9Hwqi4/s640/IMGL3837.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhlFmCAqLcZ9XiGekyviI0BSr2hBn1IrvLJQhREEcIkn5V5yHqaX5Zq3N_6zmYYuPytiD5i7C5JekkMBDJRJz4kFbAJKyzAUadiMAdTOb6MdV8ziPVQxihNun7RC4mcEVXeEQx05T9Hwqi4/s72-c/IMGL3837.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/09/tanzania-ipo-salama-na-imara-waziri.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/09/tanzania-ipo-salama-na-imara-waziri.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy