NA WAMJW-DAR ES SALAAM HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH) imepokea msaada wa vifaa vipya kwa ajili ya vyumba viwili vya upasuaji wa ...
NA WAMJW-DAR ES SALAAM
HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH) imepokea msaada wa vifaa vipya kwa ajili ya vyumba viwili vya upasuaji wa watoto wenye thamani ya shilingi Bilioni 1.5 kutoka Taasisi binafsi ya Archie Wood Foundation ya Scotland ili kufanya huduma hiyo kupatikana kw urahisi nchini.
Akizungumza katika uzinduzi wa vyumba vya upasuaji kwa watoto uliofanyika leo jijini Dar es salaam Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa msaada huo umeonyesha jinsi gani Wahisani wana ushirikiano na Serikali katika kuleta maendeleo hasa katika sekta ya afya nchini.
“ Kutokana na Wahisani kujitokeza mara kwa mara katika kushirikiana na Serikali yetu kwenye sekta ya afya tumepunguza asilimia 40 ya wagonjwa wanaokwenda nje kwa ajili ya matibabu na lengo letu ni kupunguza asilimia 70 mpaka kufikia 2025”alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy ameongeza kuwa Wazazi na walezi wawe msatari wa mbele kuwakatia watoto wao bima ya afya ijulikanayo kama Toto Afya kwa gharama ya shilingi elfu 54 ili kuokoa gharama zingine zisizo na lazima kwa ajili ya kupata matibabu.
Mbali na hayo Waziri Ummy asisitiza Uongozi na Wataalam wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kujiridhisha kwa kina ndipo kutoa Rufaa kwa wagonjwa wanaohitajika kutibiwa nje ya nchi wakati wa uzinduzi wa vyumba viwili vya upasuaji wa watoto .
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Prof. Laurence Museru amesema kuwa kutokana na msaada wa vifaa hivyo Hosiptali hiyo inatimiza idadi ya vyumba viwili vya upasuaji vilivyokamilika kwa ajili ya upasuaji wa watoto.
“Tulikua tunafanya upasuaji kwa watoto wadogo mara tatu kwa wiki kutokna na ufinyu wa vifaa lakini kutokana na vifaa hivi tutafanikiwa kufanya upasuaji mara kumi kwa wiki” alisema Prof. Museru.
COMMENTS