DKT. KALEMANI ATAKA KASI, MIRADI YA UBORESHAJI UMEME DAR ES SALAAM


Meneja Mradi wa TEDAP kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Emmanuel Manirabona (katikati) akieleza kuhusu  hatua ya ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Kurasini kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kulia) katika ziara yake aliyoifanya katika vituo vya kupozea Umeme jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndugulile.
HomeJamii

DKT. KALEMANI ATAKA KASI, MIRADI YA UBORESHAJI UMEME DAR ES SALAAM

Na Greyson Mwase, Dar es Salaam Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani ametaka wakandarasi wanaofanya kazi ya kukamilis...


Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani ametaka wakandarasi wanaofanya kazi ya kukamilisha ujenzi wa vituo vya kupozea umeme jijini Dar es Salaam kuongeza kasi ili kuondoa tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika baadhi ya maeneo  ya jijini Dar es Salaam
Dkt. Kalemani aliyasema  hayo katika nyakati tofauti  tarehe 18 Septemba, 2017 katika ziara yake ya kukagua  mradi wa uboreshaji umeme wa jiji la Dar es Salaam unaohusisha ujenzi wa vituo vya kupozea Umeme  vilivyopo katika maeneo ya Mbagala, Gongo la Mboto, Kurasini na kituo kipya cha Kigamboni.
Akiwa katika kituo cha kupooza umeme cha Gongo la Mboto, Dkt. Kalemani  aliagiza mradi  huo kukamilika ndani ya siku 14 ikiwa ni pamoja na kubadili wasimamizi wa mradi kutokana na waliopo sasa kufanya kazi kwa kususasua.
Katika hatua nyingine, akiwa katika kituo cha Kurasini Naibu Waziri Kalemani aliagiza kubadilishwa kwa kundi la wataalam kwenye ujenzi huo na kuelekeza kazi hiyo ikamilike ndani ya siku Tano
“Ninawaagiza wote kwa pamoja kufanya kazi usiku na mchana ili kazi ikamilike kwa wakati, wananchi wamechoka na taarifa za kukatiwa umeme za mara kwa mara, lazima mpambane” alisema Dkt. Kalemani.
Alisema Serikali ya Awamu ya Tano imeweka mikakati ya kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma ya Umeme wa uhakika na kwa gharama nafuu na kuvutia Wawekezaji nchini.
Naye Mbunge wa Kigamboni aliyekuwepo kwenye ziara hiyo, Faustine Ndugulile alimshukuru Naibu Waziri kwa ujio wake na kueleza kuwa tatizo la kukatika  kwa Umeme mara kwa mara katika maeneo ya Mbagala, Gongo la Mboto, Kigamboni, Kurasini limekuwa ni la muda mrefu na kupelekea wananchi kukata tama.
Alisema wananchi katika maeneo husika wanahitaji Umeme katika shughuli za uzalishaji mali na kujiongezea kipato na kuongeza kuwa hata Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linahitaji mapato kutoka katika maeneo husika.



Meneja Mradi wa TEDAP kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Emmanuel Manirabona (katikati) akimwongoza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kulia) kwenye ziara katika kituo cha kupoza Umeme cha Kurasini. Kushoto ni Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndugulile.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akitoa maelekezo katika ziara hiyo. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka.

Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndugulile akieleza jambo katika ziara hiyo.
Mafundi wakiendelea na ujenzi katika kituo cha kupozea umeme cha Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam

Mafundi wakiendelea na ujenzi katika kituo cha kupozea umeme cha Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.


Meneja wa Vituo vya Kupozea Umeme nchini, Mhandisi Izahaki Mosha akieleza hatua ya ujenzi wa kituo cha kupozea Umeme cha Kigamboni katika ziara hiyo.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: DKT. KALEMANI ATAKA KASI, MIRADI YA UBORESHAJI UMEME DAR ES SALAAM
DKT. KALEMANI ATAKA KASI, MIRADI YA UBORESHAJI UMEME DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgg-igdIJZU64QZ2eLoI8tbC8IB27FC4HcP8WOGsqpCeZ2dPU3CN3MdXoxgh0VWc-RxtO0zV-31mBwdL7A5gKzW2vV82PY1GPAPBqsdYaJDpsAA5tW0EWmgFqrXABslrwNCEJe6Xf5jzoQ/s640/Picha+Na+2.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgg-igdIJZU64QZ2eLoI8tbC8IB27FC4HcP8WOGsqpCeZ2dPU3CN3MdXoxgh0VWc-RxtO0zV-31mBwdL7A5gKzW2vV82PY1GPAPBqsdYaJDpsAA5tW0EWmgFqrXABslrwNCEJe6Xf5jzoQ/s72-c/Picha+Na+2.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/09/dkt-kalemani-ataka-kasi-miradi-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/09/dkt-kalemani-ataka-kasi-miradi-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy