CHINA NA TANZANIA KUONGEZA NGUVU KATIKA KUPUNGUZA UMASIKINI NCHINI
HomeJamii

CHINA NA TANZANIA KUONGEZA NGUVU KATIKA KUPUNGUZA UMASIKINI NCHINI

Na Adili Mhina. Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China (IPRCC) imeahidi kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano baina yake na Wizara ...

WAFURIKA OFISI YA RC MAKONDA KUDAI HAKI
WAZIRI MKUU AKIWA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU, DKT. SALIM AHMED SALIM MJINI ADDIS ABABA
SERIKALI YASISITIZA UWAZI SHUGHULI ZA MADINI


Na Adili Mhina.

Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China (IPRCC) imeahidi kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano baina yake na Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Tume ya Mipango kwa lengo la kuongeza kasi ya maendeleo na kupunguza umaskini nchini.


Uamuzi huo umefikiwa katika kikao cha wataalamu kutoka Wiraza ya Fedha na Mipango kupitia Tume ya Mipango wakiongozwa na Kaimu Katibu Mtendaji Bw. Maduka Kessy na ujumbe kutoka taasisi hiyo kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.


Akizungumza katika kikao hicho kiongozi wa ujumbe kutoka China Bw. Xia Gengsheng alieleza kuwa maeneo mapya yanayotarajiwa ni pamoja na kuanzisha vituo vingingine vya mfano vya kilimo katika vijiji mbalimbali hapa nchini.


Bw. Xia alieleza kuwa wameamua kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano kutokana na mafanikio yaliyojitokeza katika juhudi za kupambana na umaskini nchini hususan katika kutoa elimu ya kilimo kwa wakulima kupitia kuanzishwa kwa Kijiji cha mfano cha Peapea Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro.


“Ndugu Kaimu Katibu Mtendaji naomba nikuhakikishie kwamba tutaanzisha vijiji vingine vya mfano kama kile cha Peapea na kutoa fursa kwa wananchi wengi zaidi kujifunza mbinu bora za kilimo ili waweze kuendesha kilimo chenye tija na waondokane na umaskini,” alieleza Bw. Xia.


Eneo jingine la ushirikiano litakalo anzishwa ni masuala ya utafiti ambapo IPRCC kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Tume ya Mipango na taasisi zingine itawezesha kufanyika kwa tafifi katika kuchochea maendeleo na kutafuta mbinu mbalimbali za kupunguza kasi ya umaskini.


Kwa upande wake Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bw. Maduka Kessy alieleza kuwa ushirikiano kati ya Tume ya Mipango na Taasisi ya IPRCC ambao umedumu kwa zaidi ya miaka sita umekuwa na faida kubwa katika kukabiliana na umaskini kwa watanzania.


Alielezea kuwa kwa kipindi hicho Tume ya Mipango na IPRCC wamefanikiwa kuendesha programu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuratibu mazungumzo ya kisera juu ya mageuzi ya kilimo vijijini na kupunguza umaskini, kuanzishwa kwa kituo cha mfano katika kupunguza umaskini kwa wakulima wadogo Kilosa Mkoani morogoro.


Aliongeza kuwa ushirikiano kati ya Tume ya Mipango na IPRCC umefanikisha uratibu wa programu za kuwajengea uwezo watanzania kwa kutoa udhamini wa masomo katika ngazi za uzamili na uzamivu katika fani za maendeleo vijijini pamoja na kuandaa mafunzo mbalimbali yanayohusu mageuzi ya kilimo kwa maafisa kilimo pamoja na wakulima wenyewe.


Pamoja na mambo mengine, Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini ya China imekuwa ikisaidia kutoa msaada wa kitaaalamu ambapo wataalamu wa kilimo kutoka China wamekuwa wakitoa mafuzo kwa wakulima mkoani Morogoro.

Kaimu Katibu Mtendaji, Wizara ya Fedha na Mipango – Tume ya Mipango Bw. Maduka Kessy (wa tatu kutoka kushoto, mwenye tai nyekundu) na kiongozi wa ujumbe kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China, Bw. Xia Gengsheng (wanne kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wataalamu kutoka China na viongozi wa Tume ya Mipango.

Wataalamu kutoa Tume ya Mipango wakiwa katika kikao na Ujumbe kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China (hawapo pichani).

Ujumbe kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China wakiwa katika kikao na wataalamu wa Wizara ya Fedha na Mipango – Tume ya Mipango (hawapo pichani) katika ofisi za Tume ya Mipango, jijini Dar es Salaam.

Kaimu Katibu Mtendaji, Wizara ya Fedha na Mipango – Tume ya Mipango Bw. Maduka Kessy (katikati), Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Biashara za Kimataifa na Mahusiano ya Uchumi Bw. Paul Sangawe (kulia) na Kaimu Naibu Katibu Mtendaji anayesimamia Klasta ya Huduma za Jamii na Idai ya Watu, Tume ya Mipango, Bw. Ibrahim Kalengo (kushoto) wakimsikiliza mjumbe (hayupo pichani) kutoka China wakatika wa kikao.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: CHINA NA TANZANIA KUONGEZA NGUVU KATIKA KUPUNGUZA UMASIKINI NCHINI
CHINA NA TANZANIA KUONGEZA NGUVU KATIKA KUPUNGUZA UMASIKINI NCHINI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjq8x56NiA4t8z5_bF8k2LHhRCdwijGkzvsa8LZ1wyYSXX7SfYsU4w-TGS1RmPxqMfiHYuWMRqbPNzn2VrkxGwablIUDCjVx_lU6yjn77uekrJCns3efAatIzLN1jMrCOw7tDwS96D0dUU/s640/1-11.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjq8x56NiA4t8z5_bF8k2LHhRCdwijGkzvsa8LZ1wyYSXX7SfYsU4w-TGS1RmPxqMfiHYuWMRqbPNzn2VrkxGwablIUDCjVx_lU6yjn77uekrJCns3efAatIzLN1jMrCOw7tDwS96D0dUU/s72-c/1-11.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/09/china-na-tanzania-kuongeza-nguvu-katika_5.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/09/china-na-tanzania-kuongeza-nguvu-katika_5.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy