SERIKALI KUCHIMBA MABWAWA YA MAJI ILI KUPUNGUZA UHABA WA MAJI NCHINI
HomeJamii

SERIKALI KUCHIMBA MABWAWA YA MAJI ILI KUPUNGUZA UHABA WA MAJI NCHINI

Na Husna Saidi. SERIKALI imesema imeandaa mpango kabambe wa uchimbaji wa mabwawa ya kutiririsha maji ya mvua katika baadhi y...

WANAWAKE WA BAM INTERNATIONAL WAPIGWA MSASA WALIPOADHIMISHA SIKUKUU YA KIMATAIFA YA MWANAMKE DUNIANI
ECOBANK TANZANIA KUFADHILI WANANFUNZI WA SHULE ZA SERIKALI
KATIBU MKUU SIHABA NKINGA AZINDUWA MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI


Na Husna Saidi.

SERIKALI imesema imeandaa mpango kabambe wa uchimbaji wa mabwawa ya kutiririsha maji ya mvua katika baadhi ya maeneo nchini ili kupunguza hadha ya ukosefu wa maji kwa wananchi.

Hayo yamebainishwa leo Bungeni Mjini Dodoma na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo na Wazirti katika kikao cha Bunge la bajeti linaloendelea Mjini Dodoma.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema katika kutekekeleza mpango wa Serikali kumtua “Mama ndoo kichwani” Serikali imedhamiria kupunguza umbali mrefu wanaotumia wananchi kutafuta maji, ambapo imepanga kuchimba mabwawa makubwa ya maji katika  maeneo ambayo yana mtiririko wa maji.

“Tutaendelea kutoa maelekezo kwa Watendaji wetu kuhamasisha wananchi kutumia fursa ya misimu wa mvua ili kujiwekea akiba ya maji ambayo yatawasaidia wakati wa kipindi cha kiangazi hususani katika maeneo ambayo yana uhaba wa maji”.

Kwa mujibu wa Majaliwa alisema katika Bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Serikali imeandaa mpango maalum wa uchimbaji wa mabwawa ya maji sambamba na kufanya ukarabati wa mabwawa ambayo yameharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Aidha Waziri Mkuu Majaliwa alizitaka Halamashauri zote nchini kuhakikisha zinatumika vyema mabwawa na mifereji iliyokuwa katika maeneo ili kuweza kuvuna maji ya mvua na kuyahifadhi kwa msimu huu wa mvua na ujao.

Majaliwa aliongeza kuwa Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya kukarabati miundombinu ya mabwawa yote nchini ili kuhakikisha halmashauri zote nchini zinakuwa na utoshelevu wa huduma ya maji kwa wananchi wake.
Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akijibu maswali Mbalimbali ya Wabunge katika kikao cha Ishirini na mbili cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 11, 2017.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI KUCHIMBA MABWAWA YA MAJI ILI KUPUNGUZA UHABA WA MAJI NCHINI
SERIKALI KUCHIMBA MABWAWA YA MAJI ILI KUPUNGUZA UHABA WA MAJI NCHINI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhR4kMy4D9c1g6dyzTAlAqAzn11DOoP5XW1mL2MQ5R0_QHaC-T561cZHwBZxBwX9kcXEnk-Unm19mNB8LGkPOB8cQ1RXm-lNCkCEgSJUpgkYdfMcZviMDPV0hH8Sucp7hwzvOE2Rlw7zkwV/s640/6409-Waziri+Majaliwa.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhR4kMy4D9c1g6dyzTAlAqAzn11DOoP5XW1mL2MQ5R0_QHaC-T561cZHwBZxBwX9kcXEnk-Unm19mNB8LGkPOB8cQ1RXm-lNCkCEgSJUpgkYdfMcZviMDPV0hH8Sucp7hwzvOE2Rlw7zkwV/s72-c/6409-Waziri+Majaliwa.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/05/serikali-kuchimba-mabwawa-ya-maji-ili.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/serikali-kuchimba-mabwawa-ya-maji-ili.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy