MNUFAIKA WA AIRTEL FURSA BAADA  YA KUPIGWA TAFU NA AIRTEL FURSA
HomeJamii

MNUFAIKA WA AIRTEL FURSA BAADA YA KUPIGWA TAFU NA AIRTEL FURSA

 Mnufaika wa Airtel FURSA bidhaa zake ziko sokoni mikoa zaidi ya mitano Mradi wa Airtel Fursa umeendelea kufanikiwa kwa kuendele...

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT. JUMA MALEWA APOKELEWA KWA KISHINDO MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA
MAYROSE PAMOJA NA BAADHI YA WATANZANIA WAISHIO MAREKANI KATIKA KAMPENI YA KUINUA MAADILI KITAIFA 2017, MARYLAND MAREKANI
MAKAMU WA RAIS MHE.SAMIA AHUDHURIA MKUTANO WA JOPO LA KUWAWESHA WANANKE KIUCHUMI-DUBAI.


 Mnufaika wa Airtel FURSA bidhaa zake ziko sokoni mikoa zaidi ya mitano

Mradi wa Airtel Fursa umeendelea kufanikiwa kwa kuendelea kuwezesha vijana nchini ambapo mmoja kati ya waliowezeshwa mwaka jana Bi Threria Maliatabu mkazi wa Mbagala jijini Dar es Saalam ameelezea jinsi mradi huo ulivyomuwezesha kukuza kipato na kupata mafanikio ya kuanza kujenga nyumba yake binafsi, kujinunulia shamba la eka 2 huku akiwaasa vijana wenzake nchni na wale wote waliowezeshwa na Airtel FURSA kuchangamkia fursa hizi pindi zinapotokea.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es saalam , Bi Maliatabu ambaye anajishughulisha na biashara ya uchoraji wa picha za sanaa alisema “ najivunia sana kuwa mmoja kati ya vijana walioshikwa mkono na Airtel Fursa kwa sababu program hii imeweza kunitoa kutoka niliopokuwa hadi kufika kwenye haya mafanikio niliyo nayo leo. 

 Kwakweli nimekuwa na mafanikio makubwa sana ikiwemo kuboresha kiwango cha bidhaa zangu , nimefanikiwa kuanza ujenzi wa nyumba yangu ya vyumba vinne na pia nimeweza kukunua shamba la eka 2 Mkuranga mkoa wa pwani. lengo langu ni kuanzisha shughuli za kilimo ili kutanua wigo wa biashara yangu lakini pia kuendelea na shughuli yangu ya uchoraji nayoifanya kwa sasa”

Aidha Maliatabu alifafanua kuhusu changamoto mbalimbali katika biashara ikiwemo masoko ya nje , usafiri wa kusambaza bidhaa zake huku akieleza kuwa baadhi ya changamoto hizi ameshaanza kuzishughulikia na kuomba wadau mbalimbali kuweza kumsaidia.
“Nimeweza kuongeza masoko yangu na kufikia masoko ya Zanzibar, Moshi , Arusha na Dar, na kwa sasa niko katika mchakato wa kupeleka bidhaa zangu nchini Sweeden na Italy. Mipango hii ikikamilika kwakweli nitakuwa nimefurahi kufikia malengo yangu na naamini nitafanya vizuri zaidi na kukuza kipato changu zaidi. Natoa wito kwa vijana wenzangu kujituma na kufanya kazi kwa bidiii na kutafuta fursa mbalimbali na kujikita kwenye ujasiriamali badala ya kusubiri ajira ambazo zimekuwa ni changamoto”.
Akiongea kuhusu mafanikio haya, Meneja Huduma kwa Jamii, Bi Hawa Bayumi alisema , tunafarijika na kujisikia fahari kuona jinsi gani program hii imeweza kuwainua vijana hawa wajasiriamali wenye nia ya kukuza kipato na kufikia malengo yao. Theresia Maliatabu ni mfano wa kuigwa, alipowezeshwa alijiongeza na kufanya kazi kwa juhudi kubwa na maarifa. Nawaasa vijana wajitume na kuchangamkia fursa kama hizi zinapojitokeza wazitumie vizuri ili kuleta tija kwenye maisha yao, familia zao na taifa kwa ujumla.”
Theresia Maliatabu ni moja kati ya vijana waliochagulia kuwa kati ya wafanyabiashara wadogo wadogo watakaonufaika na mpango wa Airtel FURSA na kupatiwa vitendea kazi zikiwemo , ubao wa kuchorea, vifaa vya kuchorea na computer, mafunzo ya ujasiriamali na kutengenezewa kipindi maalumu cha Television kilichoonyesha safari yake katika biashara ambavyo vimemsaidia kukuza biashara yake. Airtel kupitia mpango wake wa Airtel fursa imewezesha vijana takibribani 5000 kwa kuwapatia mafunzo ya ujasirimali na baadhi yao kupata vitendea kazi ili kuboresha biashara zao.
Theresia Maliatabu, mnufaika wa mradi wa Airtel Fursa akimsikiliza mteja wakati alipohudhuria maonyesho ya bidhaa na kuonyesha kazi ya uchoraji wa picha za Sanaa anazozifanya hivi karibuni.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MNUFAIKA WA AIRTEL FURSA BAADA YA KUPIGWA TAFU NA AIRTEL FURSA
MNUFAIKA WA AIRTEL FURSA BAADA YA KUPIGWA TAFU NA AIRTEL FURSA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDSOXmLJ83wIlkFWkBumaJeYZKUUh0vkJ8pcknjfkk2hyphenhyphenWRXb9t9lNAyd7-cuMW-g9T-tVk_YiXjN7hBRBlmPgm4tKsGAqq59ljGyW_XRAJwN7APBo6QeIDAFGsA1av9JVhbmVMp8kIsg/s640/unnamed.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDSOXmLJ83wIlkFWkBumaJeYZKUUh0vkJ8pcknjfkk2hyphenhyphenWRXb9t9lNAyd7-cuMW-g9T-tVk_YiXjN7hBRBlmPgm4tKsGAqq59ljGyW_XRAJwN7APBo6QeIDAFGsA1av9JVhbmVMp8kIsg/s72-c/unnamed.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/05/mnufaika-wa-airtel-fursa-baada-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/mnufaika-wa-airtel-fursa-baada-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy