Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mim...
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akihutubia wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mimi na Wewe uliofanyika
kwenye uwanja wa Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Kisonge, mkoa wa
Mjini Magharibi, Zanzibar. 
Bila kujali mvua iliyokuwa inanyesha wananchi walijitokeza na kumsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mimi na Wewe kwenye uwanja wa Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Kisonge, mkoa wa mjini Magharibi, Zanzibar. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi,Wafadhili waliochangia kufanikisha kampeni ya Mimi na Wewe inaleta tija kwa wananchi wa mkoa wa Mjini Magharibi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Bila kujali mvua iliyokuwa inanyesha wananchi walijitokeza na kumsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mimi na Wewe kwenye uwanja wa Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Kisonge, mkoa wa mjini Magharibi, Zanzibar. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi,Wafadhili waliochangia kufanikisha kampeni ya Mimi na Wewe inaleta tija kwa wananchi wa mkoa wa Mjini Magharibi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa ahadi hiyo mjini Unguja wakati anazindua kampeni maalum ya MIMI NA WEWE inayolenga kuhamasisha wananchi kuungana pamoja katika kutoa misaada ya hali na mali ili kuboresha huduma za kijamii katika sekta za afya, elimu,mazingira,maji safi na salama, matumizi bora ya ardhi na kusaidia watu wasiojiweza.
Makamu wa Rais katika hotuba yake kwa mamia ya wananchi waliohudhuria uzinduzi wa kampeni hiyo amekemea vikali tabia ya ubinafsi kwa baadhi ya viongozi inayosababisha wananchi kutopatiwa taarifa muhimu za maendeleo yao hali inayopelekea uduni katika uchangiaji wa shughuli za maendeleo.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kuwa ni muhimu kwa viongozi katika maeneo mbalimbali kujenga tabia ya kuweka wazi mapato na matumizi ya fedha wanazopata na jinsi zilivyotumika ili kuwapa moyo wananchi katika kuchangia kwenye shughuli za maendeleo kwa sababu watakuwa na imani kuwa fedha zao walizochanga zinatumika vizuri.
“Maendeleo endelevu ni lazima yazingatie Utu na heshima ya mtu, mshikamano wa dhati na mafungamano ya Kijamii,” Amesisitiza Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais pia amehimiza wadau mbalimbali wa maendeleo hasa sekta binafsi na wananchi kwa ujumla kujenga moyo wa kujitolea na kutoa misaada ili kuhakikisha taifa linasonga mbele kimaendeleo kuliko kutegemea wafadhili wa nje ya nchi tu.
Ameeleza kuwa kampeni ya Mimi na Wewe ina umuhimu wa kipekee kwani inakusudia kuwaomba na kuwahamasisha wananchi hasa wa Zanzibar kuchangia kwa hali na mali katika kusaidia wananchi wenzao ambao hali zao za maisha bado ni duni ili kutimiza malengo ya mapinduzi kujenga maisha bora na usawa kwa kila mtu.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi kuweka kando itikadi zao za kisiasa hasa wa Zanzibar na wajenge Zanzibar imara yenye upendo, umoja na mshikamano ili kuharakisha juhudi za maendeleo.
Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud amesema wameamua kuanzisha kampeni hiyo maalum ili kurejesha moyo wa kusaidiana miongoni wa Wazanzibar hatua ambayo itasaidia maradufu uboreshaji wa huduma za kijamii kwa wananchi.
Mkuu huyo wa mkoa wa Mjini Magharibi amesema mkoa huo ndio unaongoza kwa kuwa na wananchi wengi kwa Zanzibar ambao wanafikia zaidi ya laki Tano hivyo idadi hiyo kubwa ya watu inahitaji rasilimali nyingi kwa ajili ya kuhudumia wananchi hao kitu ambacho bado ni changamoto kubwa inayohitaji ushirikiano ili kuipatia ufumbuzi.
Amesema anaimani kubwa kuwa kampeni maalum ya Mimi na Wewe itawaibua wadau wa maendeleo na wananchi wenyewe katika kutoa misaada mbalimbali ikiwemo kujitolea katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo jambo ambalo litasaidia kubadili maisha ya wananchi maskini kwa kuwasaidia kupata kipato kwa ajili ya kujiendeleza kiuchumi.
COMMENTS