ENEO LA LEBANON SOKO LA SAMAKI LA FERRY JIJINI DAR ES SALAAM KINARA KWA UKATILI WA KIJINSIA
HomeJamii

ENEO LA LEBANON SOKO LA SAMAKI LA FERRY JIJINI DAR ES SALAAM KINARA KWA UKATILI WA KIJINSIA

Mwenyekiti wa Soko la Kimataifa la Samaki la Ferry, Ali Bunda akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), Dar es Salaam juzi wakati...

MAMIA WAMUAGA RUBANI NA MTENDAJI MSTAAFU WA WAKALA WA NDEGE ZA SERIKALI MAREHEMU KENAN MHAIKI
PSPF YAWAPIGA MSASA WATUMISHI OFISI YA RAS DAR ES SALAAM
CHAWABATA CHAPINGA MANISPAA YA ILALA KUKAGUA LESENI ZA WAUZA VILEO USIKU JIJINI DAR ES SALAAM



Mwenyekiti wa Soko la Kimataifa la Samaki la Ferry, Ali Bunda akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), Dar es Salaam juzi wakati akitoa taarifa ya kupungua kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo, baada ya kupata mafunzo kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG). Bunda alilitaja eneo la Lebanon katika soko hilo kuwa ni hatari kwa ukatili wa kijinsia hasa kwa watoto.


Katibu Mkuu wa Soko la Temeke Sterio, Omari Mangilile, akizungumzia kupungua kwa ukatili katika soko hilo.




Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa Soko la Temeke Sterio AP 1248 Koplo Chaurembo Shomari, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), Dar es Salaam jana, kuhusu kampeni zilizofanywa na Shirika la Equality for Growth (EfG) za kupinga ukatili wa jinsia katika soko hilo kuwa zimesaidia kupunguza makosa hayo ambapo kwa mwezi Septemba mwaka jana yalikuwa 21 lakini sasa hakuna kabisa.


Mfanyabiashara katika Soko la Temeke Sterio, Robert Kalawila akizungumza na wanahabari.




Mwezeshaji Sheria Soko la Ferry, Fatma Ally akizungumza.


 

Mfanyabiashara katika Soko la Temeke Sterio, Mariam Juma 'maarufu Mama Kondo' akizungumzia kupungua kwa vitendo hivyo.




Mwezeshaji wa kisheria katika Soko la Temeke Sterio, Augenia Gwamakombe (katikati), akizungumza. Wengine ni wafanyabiashara wenzake.




Mfanyabiashara Tamasha Amri akizungumza.




Mfanyabiashara katika Soko la Temeke Sterio, Vicky


Mbogela akichangia jambo.




Mfanyabiashara, Lushenia Emanuel akijieleza kwa wanahabari.


Muonekano wa Soko la Samaki la Kimataifa la Ferry.



Na Dotto Mwaibale


ENEO la Lebanon katika Soko la Kimataifa la Samaki la Ferry jijini Dar es Salaam limeelezwa kuwa ni kinara kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia hasa kwa watoto.


Hayo yalielezwa na Mwenyekiti wa soko hilo Ali Bunda alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati akitoa taarifa ya kupungua kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo baada ya kupata mafunzo kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG).


"Vitendo vya ukatili wa kijinsia vimepungua kwa kiasi kikubwa katika maeneo mengine ya soko letu lakini changamoto kubwa ipo eneo la Lebanon huko ukipita usiku unaweza kulia kutokana na vitendo vinavyofanyika" alisema Bunda.


Alisema katika eneo hilo kila vitendo vichafu vimekuwa vikifanyika kwani hivi karibuni kuna mwanaume mmoja alikamatwa baada ya kubambwa akimnajisi mtoto wa kiume lakini alipofikishwa kituo cha polisi mtoto huyo aliomba mwanaume huyo asipelekwe mahakamani kwani alikuwa ni msaada mkubwa kwake kutokana na kupewa fedha za chakula na mahitaji mengine.
 

"Kauli ya mtoto huyo ilimshitua kila mtu aliyekuwepo kituoni hapo ambapo pamoja na kuomba aachiwe polisi waliendelea kumshikilia ili sheria ichukue mkondo wake" alisema Bunda.


Katibu Mkuu wa Soko la Temeke Sterio, Omari Mangilile alisema ushirikiano baina ya wafanyabiashara, viongozi wa soko pamoja na Shirika hilo na Jeshi la Polisi Kituo cha Chang'ombe kumesaidia kupunguza vitendo vya ukatili wa jinsia katika soko hilo.

Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa Soko la Temeke Sterio AP 1248 Koplo Chaurembo Shomari alisema kampeni zilizofanywa na EfG kupinga ukatili huo zimesaidia kupunguza makosa hayo ambapo kwa mwezi Septemba mwaka jana yalikuwa 21 lakini hadi kufikia sasa yamepungua na kufikia mawili na katika baadhi ya miezi mingine yakiwa hayapo kabisa.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: ENEO LA LEBANON SOKO LA SAMAKI LA FERRY JIJINI DAR ES SALAAM KINARA KWA UKATILI WA KIJINSIA
ENEO LA LEBANON SOKO LA SAMAKI LA FERRY JIJINI DAR ES SALAAM KINARA KWA UKATILI WA KIJINSIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiGmeBvyGKoEwardub-Kw7M4Jcwh_ef8W2lZFAinVMnACXyfiVpvLwfywohUi0wSR2npMoiEylXLqQj9HKwbmRe55lnhWUgbJI9SkDGypahGGNyLAKvVTz448BdZliUv4E2vemwhEmKJsfX/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiGmeBvyGKoEwardub-Kw7M4Jcwh_ef8W2lZFAinVMnACXyfiVpvLwfywohUi0wSR2npMoiEylXLqQj9HKwbmRe55lnhWUgbJI9SkDGypahGGNyLAKvVTz448BdZliUv4E2vemwhEmKJsfX/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/04/eneo-la-lebanon-soko-la-samaki-la-ferry.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/eneo-la-lebanon-soko-la-samaki-la-ferry.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy