SWEDEN YAUNGA MKONO MAPAMBANO YA SERIKALI DHIDI YA UFISADI RUSHWA
HomeJamii

SWEDEN YAUNGA MKONO MAPAMBANO YA SERIKALI DHIDI YA UFISADI RUSHWA

 Balozi wa Sweden Nchini Katarina Rangnitt ameunga mkono jitihada za serikali ya awamu wa Tano katika mapambano dhidi ya ru...

KIPINDI CHA CLOUDS 360 CHARUKA MUBASHARA KUTOKA NGORONGORO
RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA VIFO VYA ASKARI 8 WALIOUAWA KIBITI PWANI
WAZIRI MKUU: AHITIMISHA HOJA YA BAJETI YAKE BUNGENI; AAGIZA KUTOLEWA TAARIFA ZA AJIRA KILA ROBO MWAKA
 Balozi wa Sweden Nchini Katarina Rangnitt ameunga mkono jitihada za serikali ya awamu wa Tano katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi kama hatua ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za kijamii kwa viwango vinavyotakiwa kote nchini.

Balozi huyo wa Sweden nchini Katarina Rangnitt amesema hayo 3 March 2017 baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Balozi Katarina Rangnitt amesisitiza kuwa serikali ya Sweden inafurahishwa sana na jitihada hizo za serikali ambazo zinalenga kukomesha vitendo hivyo vya rushwa na mapambano dhidi ya umaskini ili kusaidia wananchi kuishi maisha mazuri kwa kupata huduma bora zikiwemo za afya,maji na elimu kwa ubora unaotakiwa.

Balozi huyo amesema kuwa Sweden itaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kwa kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo Tanzania Bara na Zanzibar kama hatua ya kujenga na kuendeleza mahusiano mazuri yaliyopo.

Kuhusu mabadiliko ya tabia ya nchi na masuala ya usawa wa kijinsia, Balozi huyo amesema kuwa nchi yake ipo mstari wa mbele kuhakikisha jitihada za utunzaji wa mazingira zinaimarishwa hivyo serikali ya Sweden ipo tayari kushirikiana kikamilifu na Tanzania katika kukabiliana tatizo hilo.

Kwa upande wake, Makamu  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan imeipongeza na kuishukuru nchi ya Sweden kwa ufadhili wake katika bajeti ya kuu serikali na kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo hasa kwenye sekta za nishati,elimu, tafiti na afya.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amemhakikishia balozi huyo wa Sweden nchini kuwa serikali ya awamu ya Tano itaendelea kupambana ipasavyo na vitendo vya rushwa, kuondoa ukiritimba katika sekta mbalimbali nchini hatua ambazo zitasaidia serikali kupata wawekezaji wengi kutoka mataifa mbalimbali Duniani kuja kuwekeza hapa nchini.

Amesisitiza kuwa ili kufikia malengo ya kuwa na Tanzania ya Viwanda Serikali itaendelea kushirikiana ipasavyo na sekta binafsi ili kuhakikisha malengo hayo yanafikiwa kwa haraka.

Ameeleza kuwa Tanzania na Sweden zina mahusiano ya muda mrefu tangu miaka 1930 hivyo ni muhimu kwa mahusiano hayo yakadumishwa na kuendelezwa kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa Tanzania na Sweden.

Kuhusu uhifadhi wa mazingira na usawa wa kijinsia,Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania ipo tayari kushirikiana na Sweden katika mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira na masuala ya usawa wa kijinsia.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amemweleza balozi huyo kuwa milango ya ofisi yake ipo wazi muda wote hivyo kama ana jambo zuri na lenye manufaa kwa taifa au anakwazwa na jambo lolote basi afike ofisi kwake ili wajadiliane na kuona namna ya kutafutia ufumbuzi.
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, (kushoto), akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini Katarina Rangnitt Ikulu jijini Dar es Salaam Machi 3, 2017.(PICHA NA VPO)
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SWEDEN YAUNGA MKONO MAPAMBANO YA SERIKALI DHIDI YA UFISADI RUSHWA
SWEDEN YAUNGA MKONO MAPAMBANO YA SERIKALI DHIDI YA UFISADI RUSHWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcF4pR5UvoP8T9cvk4LqLIil2wmpheoWQ3uE8rK7nuSA9OsShZxYXkcFD5Ip-i-yUKUFlRAdiTu6-2FK8M7kdmO4eMfLecgzDYDdMraPrccx_jGmtu8-z8Lp3sLHTZbgbAJA1fn-wPs5A/s640/IMG-20170303-WA0028.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcF4pR5UvoP8T9cvk4LqLIil2wmpheoWQ3uE8rK7nuSA9OsShZxYXkcFD5Ip-i-yUKUFlRAdiTu6-2FK8M7kdmO4eMfLecgzDYDdMraPrccx_jGmtu8-z8Lp3sLHTZbgbAJA1fn-wPs5A/s72-c/IMG-20170303-WA0028.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/sweden-yaunga-mkono-mapambano-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/sweden-yaunga-mkono-mapambano-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy