MPINA ABAINI MADUDU MRADI WA MABADILIKO YA TABIA NCHI, FEDHA ZAHOFIWA KUTAFUNWA
HomeJamii

MPINA ABAINI MADUDU MRADI WA MABADILIKO YA TABIA NCHI, FEDHA ZAHOFIWA KUTAFUNWA

Naibu Waziri Mpina (katikati) akiwa na ujumbe wake, akisisita jambo wakati wa ukaguzi wa mradi wa upandaji na utunzaji mikoko kati...

WAZIRI TIZEBA AZUNGUMZIA FAIDA ZA MAHUSIANO NA FAO, JOSÉ GRAZIANO DA SILVA MKURUGNEZI MKUU ALIPOKABIDHI VIFAA VYA KUSAIDIA KUFUATILIA MAGONJWA YA MIFUKO YANAYOWEZA KUABUKIZWA KWA BINADAMU DAR ES SALAAM
RAIS MAGUFULI KUPOKEA TAARIFA YA UCHUNGUZI WA MADINI YA TANZANITE NA ALMASI KESHO IKULU DAR
MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA MAKAO MAKUU YA KAMISHENI YA KISWAHILI YA AFRIKA MASHARIKI

Naibu Waziri Mpina (katikati) akiwa na ujumbe wake, akisisita jambo wakati wa ukaguzi wa mradi wa upandaji na utunzaji mikoko katika Delta ya Rufiji Kaskazini.
 
 Naibu Waziri Mpina  (katikati) na Ujumbe wake katika picha wakitembea kukagua mikoko iliyopandwa katika Delta ya Kaskazini Rufiji.
 
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina na ujumbe wake wakiwa katika boti  wakielekea katika ukaguzi wa upandaji na utunzaji wa Mikoko, pamoja na uharibifu wa Mazingira katika Delta ya Rufiji Kaskazini.
 
Naibu Waziri Mpina akiwaasa wasimamizi wa mradi wa upandaji na utunzaji mikoko katika delta ya Kaskazini Rufiji hawapo pichani wamueleze ukweli kuhusu matumizi ya fedha na hali halisiya mradi kabla ya kwenda kukagua upandaji, utunzaji wa mikoko na uharibifu wa mazingira.
NA EVELYN MKOKOI -RUFIJI 
NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina amebaini madudu katika matumizi ya sh. milioni 396 za ufadhili wa Mfuko wa nchi maskini zaidi duniani (LDCF) chini ya mkataba wa dunia mabadiliko ya tabianchi katika utekelezaji wa mradi wa upandaji na uendelezaji wa mikokokatika delta ya kaskazi mto Rufiji.
Katika mradi huo matumizi ya zaidi ya sh. milioni 364  mchanganuo wake
hauridhishi huku vikundi vinavyodaiwa kulipwa fedha hizo vikikana kulipwa na kusema hawakuwa na mkataba bali walifanya kazi kama vibarua kwa posho ya sh. 10000 kila wanapomaliza kazi na hawakuwa na mkataba.
Kutokana na hatua hiyo Mpina amemuagiza Mkaguzi wa ndani Ofisi ya Makamu wa Rais, Mwatano Maganga kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja anafanya uhakiki wa matumizi ya fedha hizo za mradi na kuelekeza hatua za kuchukua kwakuwa.
vielelezo alivyokabidhiwa na Msimamizi wa mradi kutoka Halmashauri ya
Rufiji Sabastian Gaganijas vina mashaka. “Naagiza ukaguzi ufanyike, lazima kuna ubadhilifu umefanyika katika utekelezaji wa mradi, baada ya ukaguzi makini, tutajua ukweli na kubaini hatua gani zitachukuliwa.” Alisisitiza Mpina.
1000 zilizodaiwa zimepandwa ni udanganyifu wa wazi.
Hata hivyo, baada ya zoezi zima la kukagua Delta hiyo yenye kilomota zaidi ya 5 Naibu Waziri Mpina, alisema amesikitishwa na jutekelezaji wa  mradi huo unaotumia  fedha za wafadhili zaidi ya sh.milioni 396 kuwa na madudu na amejionea mwenyewe  kuwa, mradi hauna usimamizi na kusema kuwa,  kuna dalili ya fedha hizo kutumika ndivyo sivyo kwakuwa hata hekta 792 kati ya 
“Huu ni uhuni ambao haukubali kwa serikali hii awamu ya tano tuliposema
hapa kazi tu tulimaanisha kuwa hatuwezi kudanganywa watu wamezoea kuona  Waziri hawezi kuja kwenye mazingira kama haya nimejionea mwenyewe mikoko iliyopandwa haendani na thamani ya matumizi ya fedha hizo na sehemu kubwa imevamiwa na kupandwa mpunga badala ya mikoko,”alisema.
Alisema katika mchanganuo aliokabidhi na msimamizo wa mradi fedha hizo
zaidi ya  sh.milioni  364 zimedaiwa matumizi yake ni pamoja na kulipa
vikundi 28 vilivyokabidhiwa mradi ambavyo sasa havipo.
Alisema cha kushangaza katika fedha hizo kipo kikundi kimelipwa zaidi ya
milioni 30 kwa kupanda hekta 3 huku kingine kikilipwa milioni 3 kwa hekta
hizo hizo.

Baadhi ya wakazi wa rufiji wakizungumza katika ziara ya Naibu Waziri Mpina, wametoa changamoto zao katika kukabiliana na uharibifu huo wa Mazingira   na kuiomba Serikali kuongeza usimamizi madhubuti katika mradi huo ili kukubaliana na uharibifu huo wa hifadhi hiyo ya mikoko,
Awali Imeelezwa na mtaalam wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu  wa Rais Bw. Cretus Shengena kuwa, uharibifu huo waMikoko unaweza kusababisha kupotea kwa uoto asili na baiyonuwai katika eneo hilo kama udhibiti wa dhati usipo chukuliwa kwa haraka kuinusuru eneo hilo la Delta ya Rufiji kaskazini.

Mradi huo wa hifadhi ya taifa ya Delta ya Rufiji kaskazini unafadhiliwa na Mfuko wa kundi la nchi maskini zaidi duniani (LDCF) kupitia Shirika la umoja wa Mataifa ya Mazingira chini ya usimamizi wa Ofisi ya Makamu wa Rais.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MPINA ABAINI MADUDU MRADI WA MABADILIKO YA TABIA NCHI, FEDHA ZAHOFIWA KUTAFUNWA
MPINA ABAINI MADUDU MRADI WA MABADILIKO YA TABIA NCHI, FEDHA ZAHOFIWA KUTAFUNWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhze5BVUTF-eWOD9BMzSZyaA7QH4NJkY8y3SjoLUqApwYNUYDMWu7itNntk2KpM0xs1OLnK3A8gsC3hduGy8DEn54vLZuk9IZWO7xK_gzgz9ioksOmtGyzu9NffKxZdXw2euYQTDFT4x-A/s640/unnamed+%252826%2529.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhze5BVUTF-eWOD9BMzSZyaA7QH4NJkY8y3SjoLUqApwYNUYDMWu7itNntk2KpM0xs1OLnK3A8gsC3hduGy8DEn54vLZuk9IZWO7xK_gzgz9ioksOmtGyzu9NffKxZdXw2euYQTDFT4x-A/s72-c/unnamed+%252826%2529.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/mpina-abaini-madudu-mradi-wa-mabadiliko.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/mpina-abaini-madudu-mradi-wa-mabadiliko.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy