RAIS MUSEVENI KUWASILI NCHINI JUMAMOSI
HomeJamii

RAIS MUSEVENI KUWASILI NCHINI JUMAMOSI

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO Rais wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Museveni anatarajiwa kufanya ziara ya siku mbili nchini ...

VYOMBO VYA HABARI VYAHIMIZWA KUWA NA WATUMISHI WA KUTOSHA MKOANI DODOMA
FURSA NYINGINE YA SCHOLARSHIP YAJA: SHULE ZA SEKONDARI ZATAKIWA KUTUMA MAOMBI SASA KUSHIRIKI MAONYESHO YA SAYANSI YA YST 2018!
AGAPE YAKABIDHI BAISKELI KWA VIJANA 15 WALIOHITIMU MAFUNZO YA HISA SHINYANG



Na. Immaculate Makilika- MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Museveni anatarajiwa kufanya ziara ya siku mbili nchini kuanzia Jumamosi wiki hii.

Taarifa hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiao wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuendeleza uhusiano mzuri uliopo baina ya Uganda na Tanzania, pamoja na kujadili masula mbalimbali ya kikanda, kimataifa na sekta mbalimbali za ushirikiano kati ya nchi hizi mbili hususani katika sekta za nishati, biashara na uchukuzi.

“ Mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Uganda yameendelea kuimarika katika miaka ya hivi karibuni, ambapo mwaka 2016 Tanzania ilifanya mauzo nje kwa Nchi hiyo ya kiasi cha shilingi bilioni 66.849, ikilinganishwa na shilingi bilioni 78.31 za mwaka 2015” alisema Waziri Mahiga.

Aliongeza kuwa Uganda ni muhimu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo haina Bandari na hivyo inategemea Tanzania kwa ajili ya kupitisha mizigo yake.

Nchi ya Uganda imezidi kuwa na umuhimu kufuatia uamuzi wa kupitisha bomba la mafuta nchini Tanzania, kutoka Kabaale –Hoima, Uganda hadi Bandari ya Tanga, ambapo bomba hilo lina urefu wa kilimeta 1443 na kipenyo cha inchi 24.Bomba hilo la mafuta litakalokamilika mwaka 2020 limnatarajiwa kupatia nchi hizi mbili fursa mbalimbali.

“ Utekelezaji wa mradi huu utafungua fursa za ajira kwa watanzania, kuchochea shughuli za kiuchumi kwa mikoa inayopita bomba hilo, pamoja na kufungua ukanda wa biashara wa kaskazini mwa Tanzania na Uganda pamoja na kuimarisha uhusiano katika soko la Afrika Mashariki” alifafanua Waziri Mahiga.

Katika hatua nyingine, Waziri Mahiga alisema kuwa kuhusu mgogoro wa nchini Burundi, kumekuwepo na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Rais Museveni pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin Mkapa ili kuhakikisha amani inarejea nchini humo.

Katika ziara hiyo ya Rais Museveni nchini, atapokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Johm Magufuli ambapo atatembelea Bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kuangalia maboresho yaliyofanywa katika bandari hiyo, pamoja na Kiwanda cha kutengeneza Juisi cha Azam kilichopo Vingunguti jijini Dar es salaam.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RAIS MUSEVENI KUWASILI NCHINI JUMAMOSI
RAIS MUSEVENI KUWASILI NCHINI JUMAMOSI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQLTYpw-_L-B-ahFIeeoUceX5Xbjdh-1_FtSN1MMWXgdc14Vyl3zrR1BC8J_2gBn4mdIjXW_mT5wZFe8sjp9FlcdP7Kn_sgPb5151026BC2x0J-brXfYkEkOBR7rcQOjYtGV_q0iHQrgg/s320/CVVRuxTR.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQLTYpw-_L-B-ahFIeeoUceX5Xbjdh-1_FtSN1MMWXgdc14Vyl3zrR1BC8J_2gBn4mdIjXW_mT5wZFe8sjp9FlcdP7Kn_sgPb5151026BC2x0J-brXfYkEkOBR7rcQOjYtGV_q0iHQrgg/s72-c/CVVRuxTR.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/rais-museveni-kuwasili-nchini-jumamosi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/rais-museveni-kuwasili-nchini-jumamosi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy