MFUMUKO WA BEI WA MWEZI JANUARI 2017 UMEONGEZEKA KWA ASILIMIA 0.8

Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo, akizungumza katika mkutano na waandishi w...




Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa kuhusu mfumuko wa bei wa mwezi Januari 2017 jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Meneja Idara ya Takwimu za Ajira na Bei, Ruth Minja.

Waandishi wa habari wakichukua taarifa hiyo.
Wanahabari wakiwa kazini.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale

MFUMUKO wa Bei wa mwezi Januari 2017 unaopimwa kwa kipimo cha mwezi umeongezeka kwa asilimia 0.8 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 0.7 ilivyokuwa mwezi Desemba 2016.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wakati akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

"Fahirisi za bei zimeongezeka hadi 105.92 mwezi Januari 2017 kutoka 1-05.04 mwezi Desemba 2016" alisema Kwesigabo.

Alisema kuongeza kwa fahirisi za bei kumechangiwa na kuongezeka kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula.

Alitaja baadhi za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa fahirisi ni pamoja na mahindi kwa asilimia 6.3, ndizi za kupika kwa asilimia 5.8, magimbi kwa asilimia 5.3 na viazi vitamu kwa asilimia 6.5.

Alisema kwa upande mwingine baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilichochangia kuongezeka kwa fahirisi ni pamoja na mkaa kwa asilimia 3.2 na majokofu kwa asilimia 2.4.

Kwesigabo alisema thamani ya shilingi ya Tanzania hupima badiliko la uwezo wa shilingi ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma zilezile za mlaji ambazo shilingi ya Tanzania ingeweza kununua katikavipindi tofauti.

"Ikiwa fahirisi za bei za Taifa zinaongezeka, uwezo wa shilingi ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma hupungua" alisema Kwesigabo.

Alisema uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma umefikia shilingi 94 na senti 42 mwezi Januari, 2017 ikilinganisha na shilingi 95 na senti 20 ilivyokuewa mwezi Desemba 2016.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)



COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MFUMUKO WA BEI WA MWEZI JANUARI 2017 UMEONGEZEKA KWA ASILIMIA 0.8
MFUMUKO WA BEI WA MWEZI JANUARI 2017 UMEONGEZEKA KWA ASILIMIA 0.8
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXCFSZy2gt_gu1tLof3iiDXLfpkB-0qw-hs5s74T2c7Gs4zInn7qFfpz_erKJYWdpyfe7efs7uxlBGRtg6dHKiRA-fm76-U6WJUj8-PRyq5Eu9EL8AzVbndKKezXTVDQITmTaJcMLt9lKQ/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXCFSZy2gt_gu1tLof3iiDXLfpkB-0qw-hs5s74T2c7Gs4zInn7qFfpz_erKJYWdpyfe7efs7uxlBGRtg6dHKiRA-fm76-U6WJUj8-PRyq5Eu9EL8AzVbndKKezXTVDQITmTaJcMLt9lKQ/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/mfumuko-wa-bei-wa-mwezi-januari-2017.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/mfumuko-wa-bei-wa-mwezi-januari-2017.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy