WAZIRI NAPE AENDELEA NA ZIARA YAKE KWA VYOMBO VYA HABARI ATOA RAI WANAHABARI KUISAIDIA SERIKALI KATIKA MKAKATI WAKE WA KUJENGA UCHUMI WA KATI

Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye akizungumza na uongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Mlimani Media wakati alipofanya ziara kujionea utendaji kazi wake na changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao. Wapili kushoto, ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abass

NA BEATRICE LYIMO-MAELEZO
SERIKALI imevitaka vyombo vya habari nchini kuwa chachu ya mabadiliko katika kipindi hiki ambacho nchi inaelekea katika uchumi wa kati.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye katika ziara yake kwa vyombo vya habari vya Clouds, Mlimani na Azam, ziara inayolenga kuimarisha mahusiano yaliyopo baina ya Serikali na vyombo vya habari nchini.
“Serikali ya Awamu ya Tano imejikita katika ajenda mbalimbali ikiwemo kutoka katika hali ya uchumi tuliona nao sasa kuelekea uchumi wa kati hivyo vyombo vya habari vinatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha suala hili linawafikia na kuleta uelewa kwa wananchi”alisema Mhe. Nnauye.
Waziri Nape alisisitiza kuwa, kumekuwa na mitazamo tofauti katika vichwa vya wananchi au jamii kwa ujumla kuhusu suala zima la kuelekea uchumi wa kati, hivyo ni jukumu la vyombo vya habari nchini kuweza kuwaelewesha nini maana halisi ya uchumi unaolengwa kuufikiwa.
“tumesikia ya kwamba uchumi wa nchi umekuwa kwa asilimia saba, mwananchi wa kawaida hawezi kuwa na uelewa wa kujua ni vipi uchumi wa nchi unakuwa, hivyo  vyombo vya habari vina mchngo mkubwa katika kuifanya jamii kuwa uelewa juu ya ukuaji wa uchumi” alisisitiza waziri Nape.
Mbali na hayo Waziri Nape amesema kuwa vyombo vya habari ni chanzo cha wananchi kuwa kitu kimoja katika kulinda amani ya nchi na utamaduni uliopo, hivyo vina budi kuzidi kutunza utamaduni uliopo pamoja na kuwafanya wananchi kupenda utamaduni wao.
Waziri Nape alisisitiza kuwa vyombo vya habari viifanye jamii kwa ujumla kuwa na utamadumi hasa wa utamaduni wa ulipaji wa kodi katika nyanja tofauti na kuwa wazalendo kwa maendeleo ya nchi.
“sisi kama wanahabari na vyombo vya habari kwa ujumla tunatakiwa kutengeneza vijana ambao kwao kulipa kodi ni fahari, vijana ambao kazi kwao ni heshima pamoja na kutengeneza vijana ambao hujivunia uzalendo wa nchi yao"Alisema Waziri Nape.
Hata hivyo Waziri Nape ameahidi kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya Serikali na vyombo vya habari nchini katika nyanja tofauti ikiwemo utoaji wa habari muhimu za utekelezaji wa Serikali katika kuleta maendeleo nchini.
 
HomeJamii

WAZIRI NAPE AENDELEA NA ZIARA YAKE KWA VYOMBO VYA HABARI ATOA RAI WANAHABARI KUISAIDIA SERIKALI KATIKA MKAKATI WAKE WA KUJENGA UCHUMI WA KATI

Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye akizungumza na uongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Mli...

JUKWAA LA BIASHARA MKOANI SIMIYU
RC RUKWA AKUTANA NA WADHIBITI UBORA WA SHULE KUJUA CHANZO CHA KUSHUKA KWA ELIMU RUKWAB
WAZIRI MKUU AKABIDHIWA KAZI YA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na uongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Media group wakati alipofanya ziara kujionea utendaji kazi wake na changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao. Kulia kwake, ni Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiangalia jinsi habari zinavyoandaliwa wakati wa ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari kwenye studio za Azm TV


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiangalia sehemu mbalimbali za studio za Mlimani Tv na Redio iliyo chini ya Mlimani Media wakati alipofanya ziara kujionea utendaji kazi wake na changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao.


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiangalia sehemu mbalimbali za studio za Mlimani Tv na Redio iliyo chini ya Mlimani Media wakati alipofanya ziara kujionea utendaji kazi wake na changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao.
 



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiangalia sehemu mbalimbali za studio za Azam Tv na Redio iliyo chini ya Uhuru Production wakati alipofanya ziara kujionea utendaji kazi wake na changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao.




Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiangalia sehemu mbalimbali za studio za Azam Tv na Redio iliyo chini ya Uhuru Production wakati alipofanya ziara kujionea utendaji kazi wake na changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao.



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiangalia sehemu mbalimbali za studio za Azam Tv na Redio iliyo chini ya Uhuru Production wakati alipofanya ziara kujionea utendaji kazi wake na changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao.



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiangalia sehemu mbalimbali za studio za Azam Tv na Redio iliyo chini ya Uhuru Production wakati alipofanya ziara kujionea utendaji kazi wake na changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI NAPE AENDELEA NA ZIARA YAKE KWA VYOMBO VYA HABARI ATOA RAI WANAHABARI KUISAIDIA SERIKALI KATIKA MKAKATI WAKE WA KUJENGA UCHUMI WA KATI
WAZIRI NAPE AENDELEA NA ZIARA YAKE KWA VYOMBO VYA HABARI ATOA RAI WANAHABARI KUISAIDIA SERIKALI KATIKA MKAKATI WAKE WA KUJENGA UCHUMI WA KATI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPzBuN0PS96IJ6GKCnfUx6drUEqZ0ND6ASiy0nOu0UgsBCWyoWdaO-PpjOBGaYQaTJKnOHIRpQVtIIW-puu6go8sKV-_dWdpT9O2qXV291aQu5zgh_rF6YyCUCWYtF07rkqjqqBFKXAA4/s640/Pix+2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPzBuN0PS96IJ6GKCnfUx6drUEqZ0ND6ASiy0nOu0UgsBCWyoWdaO-PpjOBGaYQaTJKnOHIRpQVtIIW-puu6go8sKV-_dWdpT9O2qXV291aQu5zgh_rF6YyCUCWYtF07rkqjqqBFKXAA4/s72-c/Pix+2.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/01/waziri-nape-aendelea-na-ziara-yake-kwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/01/waziri-nape-aendelea-na-ziara-yake-kwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy